Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kwa dakika zangu tano nitachangia mambo machache katika Mpango huu wa mwaka 2018/2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la kwanza, sote tunajua tunaelekea kwenye uchumi wa viwanda kama kauli mbiu ya Serikali ilivyo, lakini hakuna namna yoyote kama walivyosema wachangiaji waliotangulia kwamba tuelekee kwenye uchumi wa viwanda bila kufanya mapinduzi ya kilimo. Kwa hiyo, ni muhimu sana kwanza tukaboresha kilimo chetu na hasa aina ya kilimo tunachokifanya. Tuna vyanzo vingi, tuna rasilimali nyingi lakini sasa ni namna gani tunatumia rasimali zile. Wamesema wachangiaji wengi, malalamiko ni mengi, wakulima wamelima mazao mengi lakini hayawezi kuendelezwa na kuweza kusafirishwa ili waweze kuimarisha uchumi wao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hoja yangu kwenye eneo hili ni kwamba tuangalie ni namna gani tunavyoweza kutumia rasilimali tulizonazo kuimarisha kilimo chetu nahasa kujenga mfumo wa kilimo cha umwagiliaji. Kanda ya Ziwa kuna Ziwa kwa mfano na maeneo mengine, lakini namna gani tunatumia rasilimali hii ya maji kuweza kutengeneza kilimo cha umwagiliaji tuweze kuzalisha mazao ambayo yanaweza kutumika kama rasilimali kwenye viwanda vyetu lakini hasa kuimarisha uchumi wa wanachi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ni eneo la afya. Tunapoelekea kwenye uchumi wa viwanda, tunapojenga mfumo wa kuimarisha uchumi wetu ni vizuri na ni muhumi sana tukaimarisha afya za watu wetu vilevile ili waweze kushiriki kwenye uchumi huu. Lakini namna gani sasa maeneo yetu na watui wetu tumewajengea mazingira ya kuimarisha afya zetu? Nimepitia mpango huu lakini sioni eneno lolote linaloongelea kuendelea kutoa elimu kwa watu wetu katika kujikinga na maradhi lakini na kuimarisha mazingira ya afya kwenye ngazi za msingi. Tumeongelea kuimarisha Hospitali za Rufaa na Hospitali nyingine za Mkoa lakini tunaweza tukapunguza msongamano kwenye hospitali hizi kama tutaimarisha vituo vya afya na zahanati kwenye maeneo yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tutawekeza nguvu kubwa sana kweye hospitali za level ya juu tukasahau maeneo ya chini, bado watu wetu wanapoteza sana maisha kule chini kwa sababau katika ngazi za msingi huku zahanati na vituo vya afya hazina uwezo, wataalam wa kutosha, vifaa vya kutosha kuweza kuimarisha afya zao. Vilevile hawana elimu ya kutosha kujikinga na maradhi. Kwa hiyo, kwenye mpango huu tuweke kipengele kinachojumuisha kutoa elimu na kuongeza package kwa ajili ya kujenga zahanati, kumalizia maboma yaliyojengwa huko nyuma ambayo hayajakamilika ili tuweze kuimarisha afya kwenye maeneo ya msingi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini eneno lingine ni eneno la mawasiliano, kwa sababu hatuwezi kuimarisha uchumi wetu kama mawasiliano kwenye maeneo yetu hayako vizuri. Wamesema wachangiaji waliotangulia, haiwezekani kwamba tujenge uchumi ulio imara kama mazao yanayolimwa hayawezi kusafirishwa kutoka point moja kwenda point nyingine. Maeneo yetu mengine bado hayako vizuri sana kimawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Mpango huu inaonesha kwamba kuna kuimarisha usafiri kwenye maziwa yetu, lakini bado hatujaimarisha sana Shirika la Meli (MSL). Tungeweza kuimarisha Shirika hili tukaweza kuwapa uwezo wa kutosha, watajenga mfumo mzuri sana wa mawasiliano kwenye maziwa yetu na kwa maana hiyo sasa watu walioko visiwani na maeneo mengine yaliyoko pembezoni wanaweza sasa kusafirisha mazao yao kwenda kwenye masoko na hivyo kuimarisha uchumi wa watu wao kimsingi kwenye maeneo yake yaliyo pembezoni. Vile vile kuweka mfuatano wa usafiri wa mazao na watu kwenye mazingira yetu. Bila kufanya hivyo bado huu wimbo wa ujenzi wa uchumi ulioimara utakuw ana kasoro.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ningeshauri, pamoja na mambo mengine yote yaliyoongelewa kwenye mpango tuimarishe vilevile Shirika hili la Wakala wa Meli ili kuiweza kuwa na nguvu ya kutosha kuimarisha usafiri kwenye maeneo ya maziwa. Kwa mfano sehemu kama kutoa Ukerewe kuunganisha na sehemu ya nchi kavu, kuna matatizo makubwa sana ya usafiri wa meli, hali ambayo inafanya mazao mengi ya watu kutoka kwenye visiwa hivyo kupotea na kwa maana hiyo kuathiri uchumi wao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ambalo nilifikiri niliongelee, wamesema…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)