Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi hii jioni ya leo na mimi niweze kutoa mchango wangu katika mpango wa mwaka mmoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuanza naomba kwa kuongelea utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Kwanza nianze kwa kuishukuru Serikali kwa kulipa madeni ya wakandarasi wa miradi ya maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Meatu. Wakandarasi wamelipwa shilingi milioni 672 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maji. Nina amini watakapokamilisha wataenda kumtua ndoo mwanamke na vijiji vya Lubiga, Itinje, Mwandoya, Igobe, Mwanuzi, Mkoma, Mwamalole na Bukundi vitanufaika na miradi hii ya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni nipende pia kuongelea fedha za miradi ya maendeleo. Kumekuwa na upungufu wa kutokuletwa au kuchelewa kwa fedha za utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Hili ni tatizo katika takribani Halmashauri zote za nchi nzima. Miradi imekuwa ikitekelezwa nusu nusu au kwa kusuasua au kutekelezwa kwa kipindi kirefu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wamekuwa wakitekeleza hatua yao ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Hata hivyo Serikali imekuwa ama inaleta fedha kidogo za CDG ama kutokuleta kabisa fedha za CDG ama kutokuleta kabisa fedha za CDG na kusababisa miradi mingi kuwa viporo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano Halmashauri ya Wilaya ya Meatu mpaka sasa ipo miradi viporo ya miaka 10, tisa na nane. Halmashauri ya Wilaya peke yake kwa kipindi cha kuishia Juni, 2017 walikuwa na miradi ya viporo ya shilingi bilioni tano na walitenga shilingi milioni mia tano zikiwa ni fedha za CDG na mapato ya ndani kwa ajili ya kutekeleza. Kwa hiyo, nimshauri Mheshimiwa Waziri aweze kutenga fedha kwa ajili ya kukamilisha miradi iliyo viporo. Kama Halmashauri ya Wilaya ya Meatu peke yake tu inadai shilingi bilioni tano, na kwa mwaka mmoja tu imepanga milioni 500; kwa hiyo itachua miaka 10 kukamilisha miradi hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Meatu ilikuwa na tatizo la uvamizi wa wanyama pori katika makazi ya wananchi pamoja na mashamba ya wananchi na kusababisha vifo ama mavuno yao kuliwa na wanyamapori. Hata hivyo sioni jitihada yoyote inayofanywa na Serikali ya kuwafidia wananchi ambao mazao yao yalikuwa tayari kuvunwa lakini yakaliwa na wanyama poli. Naiomba Wizara pia iweke mpango wa kulipa fidia hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais alisema Mkuu wa Wilaya ambaye ataleta tatizo la njaa latika Wilaya yake ataonekana kwamba hatoshi; lakini sisi Wilaya ya Meatu wananchi wamejitahadi lakini wanyamapori wamekula mazao yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie kuhusu ukamilishaji wa Daraja la Mto Sibiti. Ni muda mrefu sasa wananchi wamekuwa na kiu ya kuona daraja hilo sasa limekamilika. Hata hivyo tangu Septemba, 2016 katika kikao cha ushauri wa Mkoa tulihaidiwa kwamba vyuma vya kufunga daraja hilo vinatengenezwa China, lakini mpaka leo ni mwaka wa zaidi vifaa hivyo havijafungwa na tulihaidiwa kwamba masika hii tutapita. Mimi binafsi nimekuwa mpitaji wa hiyo sioni dalili yoyote ya kukamilika kwa daraja hilo. Binafsi ninaona mradi unaenda pole pole. Kukamilika kwa daraja hilo kutainua uchumi wa Mkoa wa Simiyu hususani katika Wilaya ya Meatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu hata vifaa vya ujenzi vimekuwa vikipanda bei kutokana na mzunguko kwamba vipite Shinyanga ndipo vije Mkoani Simiyu, lakini kukamilika kwa daraja hili kutakuwa ni mkombozi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichangie kuhusu elimu ya bila malipo. Tunaishukuru Serikali kwa kuleta mpango wa elimu ya bila malipo. Hata hivyo mpango huu umesababisha ongezeko la udahili kwa wanafunzi na kusababisha upungufu wa miundombinu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wilaya ya Meatu kuna changamoto ya wanafunzi kutembea umbali mrefu mpaka kwenda kusoma na kusababisha mahudhurio kuwa hafifu. Kwa mfano shule ya sekondari Mwamaloe form one walianza wanafunzi 78, lakini waliohitimu ni wanafunzi ni 23. Moja ya sababu iliyosababisha ni umbali mrefu. Kwa hiyo, wanafunzi waliacha shule kwa ajili ya umbali mrefu. Kwa maana hiyo ninaomba shule ya bweni ya Wasichana ya Nyalanja ijengewe uwezo ikiwa ni kuongezewa mabweni pamoja...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)