Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimepitia sana kitabu cha Waziri Mpango, nisikitike tu kusema mambo mengi tunayoyaona ni yale yale, hakuna mambo mapya. Mheshimiwa Mpango nilitegemea ungekuja na mikakati mipya kuhusu suala la bandari. Tukizungumzia bandari, tumeambiwa bandari ikisimamiwa vizuri inaweza ikasaidia kuongeza Pato la Taifa hili tukaachana na kukimbizana na watu wanyonge, wafanyabiashara wadogo ambao hawana nguvu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bandari ilivyo hivi sasa ukiwauliza wafanyakazi wa bandari wanakwambia hawaijui siku yao wala saa. Bandari imegeuka kuwa siasa, viongozi mbalimbali wanakwenda na camera kwenda kutumbua viongozi wa bandari, wakurugenzi wa bandari. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mpango atuambie asione aibu, kama unahitaji kusaidiwa kwenye bandari usione aibu sema. Nchi zingine zenye bandari zinafanya nini zinafanikiwa, kwa nini Tanzania hatufanikiwi? Tafuta experts wa kusaidie tufanyaje bandari yetu iweze kusonga mbele ichangie Pato la Taifa. Kila siku Mheshimiwa Mpango wewe unazungumzia, ooh, kodi zitaongezwa kwenye sigara na kadhalika, kumbe tuna bandari ambayo ingeweza kusaidia hata hizi sigara ambazo tunasema zina madhara tukaachana nazo kwa sababu kuna siku Watanzania wataamka watalielewa neno “no smoking” na sijui mapato tutapata wapi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano Bandari ya Mtwara, yenye kina kirefu, lakini tumeifanyia kazi kwa kiasi gani? Leo tulikuwa tukisikia TRA wanatangaza mapato yao wamepata kiasi gani, lakini ukienda bandarini hakuna meli, meli utakayoikuta imebeba kokoto inapeleka Qatar kwenye kuandaa Kombe la Dunia. Kwa nini meli zisiwepo pale ambazo tunajua zime-import tunahakikisha tunapata mapato? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mpango usione aibu, tafuta namna ambayo utashauriwa na wataalam waweze kusaidia tufanyaje bandari ya Tanzania iweze kusaidia kuongeza pato na kuwapunguzia mzigo Watanzania ambao wanakimbizana huko, mtu unamkuta ana kamtaji kake ka laki mbili anaambiwa anunue EFD machine ya shilingi laki nane, hii ni ajabu sana. Kamtaji ka laki mbili, laki tano unaambiwa nunua EFD machine ya laki nane, are we serious? Bandari isimamiwe na ifanye kazi yake vizuri iokoe jasho na vilio vya Watanzania. (Makofi)

T A A R I F A . . .

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa siipokei, nilifikiri ananiambia kwamba bandari inafanya kazi kwa zaidi ya asilimia 100, ananiambia 40? Bandari tunayo miaka mingapi toka uhuru mpaka sasa hivi tunazungumzia bandari hiyo hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumze kuhusu fine za barabarani. Traffic wametoka kwenye lengo la kusaidia kupunguza ajali za barabarani, sasa hivi wamegeuka kama maofisa wa makusanyo wa TRA. Nikizungumza hayo wanaotoka Dar es Salaam wanaelewa, shida wanazokutana nazo watu wenye magari, traffic hivi sasa wanafungua mpaka bonnet kuhakikisha wanakusanya mapato na kila mwisho wa mwezi wanatoa tathmini, tumekusanya milioni kadhaa kwa sababu ya matatizo na makosa mbalimbali ya barabarani, hivi hii ni faida ni hasara? Hivi hili ni tatizo au? Kwa sababu huwezi ukasema umekusanya mapato kwa fine za barabarani maana yake hujafanya kazi yako ipasavyo. Tulitegemea wangekuja na taarifa kwamba ni namna gani wamepunguza ajali kutoka asilimia fulani kwenda asilimia fulani na siyo kutuletea mapato, hii sio kazi yao, ni kazi ya TRA hii. Kama tuna nia ya kukuza uchumi ni lazima tuangalie vitu hivi na sijui kama Mheshimiwa Mpango kwenye hili amewawekea traffic wapi maana wanaonekana nao wanafanya kazi ya kukusanya sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumze kuhusu habari ya viwanda. Nimesikia kwamba hivi sasa mikoa inatakiwa kuwa na viwanda 100. Hivi ni viwanda vipi? Tunasema mtu akiwa na cherehani tano tayari ni kiwanda, are we serious? Tuna viwanda vingapi ambavyo vimekufa hivi sasa havieleweki? Mkoa wa Morogoro wenyewe una viwanda zaidi ya 20 vime-collapse, hakuna ajira, wengi wanafugia mbuzi hivi sasa. Viwanda vya Morogoro watu walichukua wakafanya kama collateral kwenda kuchukulia mikopo kufanya shughuli zao zingine lakini viwanda vimekufa. Kwa nini tusivitazame viwanda hivi ambavyo tayari vipo ambavyo vilianzishwa kwa nguvu ya Mwalimu Nyerere? (Makofi)

T A A R I F A . . .

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa siikubali. Mimi nilifikiri angenieleza kwamba tayari viwanda vimeanza kufanya kazi. Hizi hadithi anazosema tumeanza kuzisikia siku nyingi tu. Kusema leo tutafufua, kesho tutafufua, watu wa Morogoro tulishazoea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niangalie kwenye sekta ya utalii. World Bank wanatuambia sekta ya utalii ikisimamiwa ipasavyo ina uwezo kabisa wa ku-cover budget yetu kwa mwaka. Hivi sasa tunajiuliza pamoja na vivutio tulivyonavyo, hifadhi tulizonazo lakini bado hakuna kitu ambacho tunaona kama vile tunafanya kwa malengo ya kuhakikisha sekta hii inanyanyuka na inachukua nafasi kusaidia Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia hoja zinazoendelea hivi sasa tunataka kuona Waziri anasimamia pale kwenye sekta ya utalii kutoa ushauri na kuangalia tufanyaje tuende mbele badala yake sasa Waziri anayepata nafasi yeye ana kazi ya kuangalia aliyetoka alifanya nini na vijembe. Aje na mkakati kwamba yeye atafanya nini kutupeleka wapi ili sekta hii itusaidie, si kufufua makaburi Mawaziri wengine wamefanya kitu gani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafikiri kuna mahali ambapo tumekosea, ni lazima tuwe na mipango mikakati ambayo itatusaidia ili sekta hii ya maliasili na utalii iende kuwasaidia Watanzania kama vile…

TAARIFA . . .

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, huyu naye ni Mjumbe mwenzangu kwenye Kamati mimi ninashangaa sana kwenye Kamati anasema vile huku leo anasema hivi. Yeye juzi hapa amesema Mheshimiwa Kigawangalla akae vizuri vinginevyo atatumbuliwa kama Mheshimiwa Maghembe au siyo, sasa sasa hivi anatupa taarifa ipi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, huwezi kuzungumza kukuza uchumi bila kuangalia jinsi ya kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja. Ukiangalia hali ilivyo hivi sasa huwezi kuwatoa watu ambao ni matajiri wanaoishi kama malaika useme waishi kama mashetani, haiwezekani, hivi vitu vyote vinategemeana. Sasa ifike mahali watu waangalie sekta binafsi zinafanya nini na Serikali ione ni jinsi gani ya kusaidia sekta hizi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa tunaona hasara ambazo zinapatikana kwa hivi sasa kwenye sekta nyingi. Kwa mfano, Club Bilicanas iliyokuwa inamilikiwa na Mheshimiwa Mwenyekiti Mbowe ilivunjwa kwa jazba na kadhalika lakini hivi sasa club ile magari yana-park; kulikuwa kuna migahawa, kuna Gazeti la Tanzania Daima, watu wangapi wamepoteza ajira? Wafanyakazi wangapi walikuwa wanategemea pale kuishi maisha yao? Leo hii kweli, taxi ndiyo zina-park pale? Hatuwezi kujenga uchumi kwa kuumiza watu.

T A A R I F A . . .

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi niulize kilimo cha green house kina conserve mazingira lakini watu wa Kagera wanaolima kwa jembe wameambiwa walime mpaka mtoni hawaharibu mazingira. (Makofi)

Kilimo cha green house ambacho kinatumia water drip, ni maji kidogo sana, lakini matokeo yake ni…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)