Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa fursa hii na nitaitumia vizuri, Insha-Allah. Nataka nianze kwa premises mbili, kwanza ni ile ambayo umeizungumza sasa hivi kwamba, mara nyingi ukichangia katika hali ya kukosoa unaonekana kana kwamba, unakosa uzalendo hivi. Kana kwamba, wewe unatoka kwenye sayari ya Mars umekuja hapa na huna haki ya kusemea. Ndiyo maana Msemaji wa mwisho akasema inafika mpaka unapewa majina.

Mheshimiwa Mwenyekiti, premises ya pili ninayotaka nisemee ni Serikali kuwa very defensive. Wakati mwingi Wabunge wakitoa michango mara nyingi utasikia, labda pengine hilo lililosemwa sasa hivi lingekuwa limetoka upande huu kungekuwa na miongozo kama kumi, kumi na tano, lakini pengine imetoka upande ule kuna stahamala kidogo. Naomba Serikali isikilize Wabunge, listen up, tusikilizeni mtakuwa na nafasi ya kusema na miongozo haisaidii kitu kwa sababu miongozo at the end of the day Watanzania wanatusikiliza na zile hoja zinabaki palepale tusiwakatize watu kwa miongozo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, nataka kusema kwamba, kama Watanzania kama Wabunge tuna- appreciate ambacho kinafanywa na Serikali, si kweli kwamba, kila kitu hatuoni. Tunaona na tunajua, lakini tuna wajibu wa kusemea. Kwa mfano, tunajua kwamba, kuna improvement kubwa ya doing business in Tanzania. Tumetoka nafasi ya 144, according to World Bank hata juzi tu tumekuja nafasi ya 52, which is very good na hiyo ni pongezi kwa Serikali kwa sababu, ina maana kwamba, tunaweza kuvutia watu kuleta mitaji yao kwa sababu it is easier to make business in Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, tuko proud kama Watanzania kwamba, kuna vitu vingi vinafanywa, maendeleo yetu ya kila aina, lakini tunapotofautiana ni kwamba, je, tunapaswa kuyafanya haya yote kwa wakati mmoja? Tunapotofautiana kama alivyosema Msemaji wa mwisho, tunapaswa kutumia resources gani katika kuyafanya haya kwa kipindi hiki? Hiyo ndiyo tofauti yetu kubwa inapokuja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kusoma kwenye mtandao kujitayarisha kwa presentation hii, sina hakika kama hii ni hakika statement ya World Bank or not lakini wanasema projection yetu wamei-down kidogo kutoka 7.1 ya growth mpaka 6.6. Kwa hivyo, matarajio ya kukua kwa uchumi hiki kipindi kinachokuja haitokuwa tena 7.1, itakuwa 6.6.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa Waziri hili aje alizungumzie na vitu gani vitafanya hiyo tushuke, wao wamesema hivyo. “there appears to have been an overall deterioration in business sentiment due to perceived risks resulting from unpredictability of policy actions related to the Government intensified efforts to collect revenue and it is anti- corruption drive.” Kwa maana hali ambayo Serikali na sera zetu za kukusanya kodi, Serikali na sera zetu za kupigana na rushwa kunaweza kufanya mapato katika mwaka unaokuja yakashuka kutoka 7.1 mpaka 6.6 maana yake nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, maana yake ni kwamba tunafanya vitu kwa nia nzuri ya kukusanya kodi, kuondoa rushwa lakini zina boomerang. Wale ambao wanajua maana ya boomerang ni kwamba kule Australia kuna ubao unachongwa unaurusha uende mbali kama usipotahadhari utarudi tena utakupiga wewe mwenyewe. Kwa hivyo, kuna makosa hapa tunayoyafanya na wenzetu wanaona kwamba makosa haya yanaweza kutu-cost. Kama ni suala la kupigana corruption na kupigana na suala la revenue ambalo kuna mashaka katika ukusanyaji wake, mimi kama Mheshimiwa Ally Saleh ningependa kuongeza haya pia yana athari katika uchumi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo hayo ni rule of law, political stability, usalama wa raia na Katiba. Mimi naamini hayo yana relation ya moja kwa moja baina ya uchumi na mambo haya ya utulivu wa kisiasa, utawala wa kisheria, usalama wa raia na Katiba yenyewe. Pengine ingekuwa kila kitu kipo vizuri theoretically hayo yote yamekaa sawa pengine FDI’s, uwekezaji kutoka nje ungekuwa mkubwa zaidi kuliko hali ilivyo hivi sasa, lakini tatizo letu nchi hii tuna tatizo la denial, tunakataa kwamba siasa yetu iko sawa hakuna kinachobadilika; raia wetu wako salama hakuna kinachobadilika, lakini vitu vingine vidogo tu, tunaona katika stock market za nchi nyingine; suala dogo tu linaweza likashusha stock market point tano au sita. Kwa hiyo, haya tusiyadharau nami nitaelezea kwa nini nayasemea hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, tunasema tuna utawala mzuri lakini inatokea mtu ambaye ameshutumiwa kwa rushwa, ambaye amesemwa waziwazi kwamba amenunua Madiwani anapandishwa cheo, mtu ambaye ameshtakiwa kwa kesi iko Mahakamani anachaguliwa nafasi kisha Serikali ina-enter nolle proseque. Wasiojua maana ya nolle ni kwamba Serikali kwenda Mahakamani kusema hatuendelei na mashtaka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, unamchagua mtu ambaye unajua kama ana kesi Mahakamani, unampa cheo kisha unakwenda kufuta mashtaka, what message are you sending? Definitely wa nje wanaona kumbe nchi hii ina utaratibu mbaya wa kisheria. Katika wakati ambao tunapigana na rushwa Serikali inakwenda ina-enter nolle kwa watu kadhaa, msururu wa watu ambao wana mashitaka ya rushwa, wameshakaa miaka mitano, sita, saba jela lakini je, is this a proper timing? Inaonesha nini katika suala la kwamba nchi hii inapigana na rushwa. Kwa hivyo tuna tatizo katika suala la rule of law. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maana hiyo unajiuliza Serikali what has it show kupigana na rushwa mpaka hivi sasa, kuna kesi gani ya conviction ambayo imeonekana kupigana na rushwa ambayo itamfanya mtu wa nje aseme kwamba nchi hii kweli inapigana na rushwa. Katika doing business je, mfumo wetu uko mzuri kiasi gani wa kuhakikisha kwamba hakuna rushwa kwa sababu hilo tatizo linalalamikiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo nataka kuzungumzia ni suala la political stability. Hapa Bungeni tumeshuhudia jinsi gani Chama kimoja kilivyogawanywa. Inafika wakati humu ndani hatuwezi kukaa na kushauriana kama Wabunge pamoja kwa sababu CUF imekatwa katikati. Una-send message gani kwa wengine huko nje kwamba wewe unaendesha siasa vizuri na unathamini mchango wa Wabunge. Ikiwa kama Wabunge wa CUF hawawezi kushirikiana kwa umoja wao unatarajia input gani upande wa CUF ije kwa Serikali ikusaidie? What do you gain?

T A A R I F A ....

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, siipokei kabisa taarifa kwa sababu Bunge limehusika na iko siku nilitaka nikueleze juu ya mgawanyiko huu ukaniambia kwamba nikisema utanipeleka Kamati ya Maadili. Kwa hiyo, Bunge limehusika katika hilo, tuache. Haijawahi kutokezea popote pale unaichukua Kamati Kuu nzima ya Chama unaipeleka Polisi kwenda kuihoji, tuna-send message gani kwa watu wengine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, chama gani kinaweza kikapelekwa chote Mahakamani wakati chama kina Principals wake, lakini unachotaka kufanya ni kuonesha kwamba unataka kuminya watu kujieleza na hilo hali-hog well na ujenzi wa uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, no, haya yote yanahusiana na mpango kwa sababu mpango hautotekelezeka, mikopo haitokuja, riba haitakuwepo na wananchi watakuwa, haya yanahusika na mpango moja kwa moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo asubuhi tulimsikia Waziri Mkuu hapa anasema kwamba Serikali hii itafanya suala la Katiba wakati Watanzania watakapomaliza matatizo yao. Kwanza siamini kama tutamaliza matatizo yetu kama Watanzania, shida ya maji, elimu na shida nyingine
zitaendelea kuwepo, lakini katiba ndiyo msingi wa huu mpango.

Mheshimiwa Spika, huwezi kuwa na Katiba ambayo wananchi wake wamegawanyika, mambo yake yanabishaniwa katika nchi halafu ukatarajia utakuwa na mpango mzuri wa kuzalisha lakini matokeo yake ndiyo kama haya ambayo tunayaona hivi sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuzungumzia pia kuhusiana na suala zima la Tanzania kama nchi. Najiuliza kama Mtanzania what are our best products, what are we marketing, branding yetu ipo kwenye kitu gani? Kama Mtanzania najiuliza mpaka sasa huwa nachachiwa. Katika production tume-specialize katika kitu gani ambacho tunaweza tukajivuna katika Afrika Mashariki na katika Afrika tukasema kama Sri Lanka wanauza chai basi brand yao ni dunia nzima, kama Israel wanauza vifaa vya umeme basi brand yao ni dunia nzima, mimi sioni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu hiyo basi naona Mpango wakati mwingine ndiyo mwenzetu mmoja alisema pale kwamba ni copy and paste ilivyokuja lakini ingekuwa angalau tunaji-specialize katika maeneo madogo ambayo yanatusaidia vizuri tungeweza kufanya vizuri sana kuliko ambavyo tupo tupo hivi sasa. We are master of all lakini vinginevyo sio vizuri. Kwa hiyo, hatuko vizuri sana, ningependekeza basi tuwe na utaratibu ambapo tuna major brands tunazitengeneza ili ziweze kuuzika kama nchi tuweze kumiliki soko la wenzetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la private sector. Amezungumza msemaji wa mwisho kwamba hawaonekani Serikali kama ina nia ya kuwashirikisha private sector kama inavyofaa, hayo ndiyo maoni yangu. Mfano mdogo tu nikitazama kule Zanzibar, pengine Zanzibar ni ndogo lakini unaona impact ya Said Salim Bakhresa, amejenga City na vitu gani vingine lakini huku upande wa Tanzania Bara na pengine hata Zanzibar kwa kiasi fulani ile kuwavuta wale wateja wa ndani siyo sana kama inavyotarajiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, tumekwenda kukopa nje na tumekopa commercially Swiss Bank na kwingine kote kwa maana kwamba mkopo ni mkubwa, lakini tunakwenda kukopa mkopo ambao unatakiwa ulipwe kwa asilimia tisa na tumeacha mkopo ambao pengine ungetaka ulipiwe asilimia moja. Mkopo ambao ungetaka ulipwe kwa muda mrefu zaidi tumekwenda kukopa mikopo ambayo inatakiwa ilipwe kwa muda mfupi zaidi, wakati tungeweza kutumia resources za ndani za watu wetu wakaweza ku- absorb baadhi ya zile fedha zikabakia ndani na matokeo yake wao wakiwa ni wawekezaji wa ndani ina maana kwamba yale matunda yanabakia ndani zaidi kuliko kwenda kukopa nje matokeo yake matunda yanakwenda nje zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hao wote wanaokuja hapa at the end of the day ni mabepari ambao kutengeneza faida kwao ndiyo jambo la muhimu kuliko kitu chochote kwa hivyo ni lazima watakuwa na masharti. Ndiyo hao ambao tukikosana nao wanatupeleka Paris au London kwenye Mahakama. Nashauri kwamba tungetazama eneo hilo tukafanya vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.