Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi kuchangia hoja iliyo mbele yetu jioni ya leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu utajikita katika kujibu hoja zilizotolewa na Msemaji wa Kambi ya Upinzani juu ya role iliyochukuliwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania kipindi cha uchaguzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Msemaji wa Kambi ya Upinzani alianza kwa kusema kwamba Zanzibar imetekwa na Jeshi la Tanganyika tangu kipindi cha uchaguzi wa kwanza hadi wa pili na majeshi yako Zanzibar in full combat kana kwamba nchi iko katika vita. Naomba nimueleze Mheshimiwa Msemaji wa Kambi ya Upinzani kwamba hakuna Jeshi la Tanganyika. Nitawaomba Waheshimiwa Wabunge kwa kufuata Katiba ya nchi, jeshi ni moja na ni Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa maana ya kujibu swali la kuwa kwenye combat, naomba nimuelimishe Mheshimiwa kama ifuatavyo. Kazi kubwa tatu za Jeshi ni ulinzi wa mipaka, ulinzi wa amani na kutoa msaada kwa mamlaka za kiraia au vyombo vingine vya ulinzi na usalama wanapohitajika kufanya hivyo. Hili suala ni la Kimataifa wakati wa uchaguzi majeshi yote yanakuwa standby. Ndiyo maana jeshi linakuwa kwenye combat kwa sababu ni kipindi cha standby, cha tahadhari. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hawaishii kuwa standby tu hata major installations katika nchi zinalindwa na jeshi wakati wa uchaguzi. Bandari, viwanja vya ndege, redio na televisheni na sehemu ambazo ni za uzalishaji mkubwa wa umeme na kadhalika, wakati huo vinalindwa na jeshi kwa sababu ya kuweka tahadhari. Kwa hiyo, hiyo ndiyo sababu kwa nini walikuwa kwenye combat na hii ni ya Kimataifa unaweza uka-check nchi yoyote wakati wa uchaguzi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la pili alilolizungumzia Mheshimiwa alisema Jeshi la Tanganyika linatumika kuulazimsha Muungano. Kama nilivyosema awali kwanza hakuna Jeshi la Tanganyika. (Makofi)
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Hata hivyo, niseme kwamba Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania ni kielelezo cha Muungano wenyewe. Toka tulipoungana mwaka 1964, jeshi limekuwa ni moja, Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania pande zote mbili. Kwa hiyo, hakuna suala la kulazimisha utawala, ni suala la kwamba jeshi liko Zanzibar kwa madhumuni ya kulinda mipaka ya nchi yetu kwa ujumla. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa alisema katika uchaguzi wa marudio, Serikali ya Muungano ilipeleka majeshi na silaha Zanzibar ili kuhakikisha kuwa malengo yao ya kuendelea kuitawala Zanzibar kimabavu yanaendelea.
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Niwaeleze Waheshimiwa kwamba Jeshi toka mwaka1964 lina vikosi vyake Zanzibar. Vikosi hivyo kwa taarifa yenu si kwamba havina silaha siku zote silaha zipo. Tuna haja gani ya kupeleka wanajeshi, tuna haja gani ya kupeleka silaha wakati wa uchaguzi wakati miaka yote viko kule. Tunachosema jeshi liko kule kwa madhumuni ya kulinda mipaka yetu na kuleta amani si vinginevyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, anasema JWTZ limepata heshima kubwa katika medani za Kimataifa kwa nidhamu na uhodari wake wa kulinda amani katika nchi nyingine lakini Serikali ya Jamhuri ya Muungano imekuwa ikilitumia jeshi hili vibaya kwa kulipeleka Zanzibar kwenda kusaidia kufanya ghilba…
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Ya uchaguzi na hivyo kujikuta kwamba linashiriki katika uvunjifu wa amani badala ya kuleta amani. Mimi ninachosema ni kwamba, kwanza namushukuru kwa kuelewa kwamba jeshi letu lina sifa ya Kimataifa ya ulinzi wa amani. Nchi zote duniani zinalisifia jeshi letu kwa sababu ya weledi na nidhamu. Narudia kusema liko pale Zanzibar kwa madhumuni ya kulinda amani, kulinda mipaka yetu na sovereignty ya nchi hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa aliendelea kusema kwamba Jeshi la Wananchi wakati wa uchaguzi lilikuwa likifanya uandikishaji wa wapiga kura katika makambi yao nje na utaratibu wa uandikishaji wa wapiga kura. Mimi nasema Mheshimiwa tumwogope Mungu.
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, haijawahi kutokea na wala haitatokea watu kuandikishwa katika makambi ya jeshi.
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Si kweli na kama unao ushahidi nitapenda niuone na hilo naweza nikakuhakikishia, jambo hili halipo kabisa. (Makofi)
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, aliendelea kusema kwamba Serikali ilieleze Bunge ni kwa nini inatumia vibaya Jeshi la Wananchi wa Tanzania katika masuala ya kisiasa.
Mimi ndiyo nasema sasa kwamba nyie ndiyo mnaliingiza jeshi katika masuala ya siasa. Jeshi halijawahi kutumika kisiasa hata siku moja na mara zote nasema ni vyema Waheshimiwa Wabunge tukazungumza siasa zetu bila kuliingiza jeshi. Kwa sababu Jeshi la Wananchi wa Tanzania linafanya kazi nzuri ya kulinda amani na nakuambieni kukosa kuwa na Jeshi la Tanzania katika uchaguzi huu pale Zanzibar pasingekalika.
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Si kweli na kama unao ushahidi nitapenda niuone na hilo naweza nikakuhakikishia, jambo hili halipo kabisa. (Makofi)
(Hapa baadhi ya Wabunge walikuwa wakiongea bila mpangilio)
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, aliendelea kusema kwamba Serikali ilieleze Bunge ni kwa nini inatumia vibaya Jeshi la Wananchi wa Tanzania katika masuala ya kisiasa.
Mimi ndiyo nasema sasa kwamba nyie ndiyo mnaliingiza jeshi katika masuala ya siasa. Jeshi halijawahi kutumika kisiasa hata siku moja na mara zote nasema ni vyema Waheshimiwa Wabunge tukazungumza siasa zetu bila kuliingiza jeshi. Kwa sababu Jeshi la Wananchi wa Tanzania linafanya kazi nzuri ya kulinda amani na nakuambieni kukosa kuwa na Jeshi la Tanzania katika uchaguzi huu pale Zanzibar pasingekalika.
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja.