Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kwa kumshukuru Mungu kwa kunijalia afya njema na kuweza kunijaalia kuchangia. Naunga mkono Hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani na pia nawapongeze Mawaziri kwa kazi .

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu ni kwamba, hapo zamani za kale Tanzania hapakuwepo na migogoro ya ardhi hususan ya wakulima na wafugaji, lakini siku za karibuni migogoro ipo kila kona ya Tanzania. Sababu kubwa watu wamejua thamani ya ardhi kuwa ni mali. Ardhi ni rasilimali muhimu ambayo pia ni urithi na utajiri wa asili toka kwa Mwenyezi Mungu. Naishauri Serikali, ardhi yetu ipimwe, ipangiliwe isiwe nchi nzima ni viwanda, barabara, makazi na maeneo ya vijijini tu ndio mashamba. Ardhi ipimwe na imilikiwe na wananchi kama ilivyo kwa South Africa, Kenya na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mashamba ya Mkonge (Amboni Company Limited). Halmashauri ya Jijiji la Tanga lina mashamba makubwa ya Mkonge ya Amboni Company Limited sasa (COTAIL) ambayo imechukua nafasi ya Amboni Limited. Naipongeza Kampuni ya Cotail Limited kwa kuipa Halmashauri ya Jiji la Tanga ardhi kwa ajili ya shughuli za maendeleo yenye ukubwa wa takriban heka 400.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yamejitokeza matatizo baada ya Halmashauri kupata mwekezaji wa China anayetaka kujenga Kiwanda cha Cement. Kuna wakulima ambao wanalalamika kuwa wamepunjwa fidia, hivyo naomba, Mheshimiwa Waziri tukatembelee eneo husika ili kutatua kero ndogo ndogo na kuweza kufanya mradi mkubwa wa Kiwanda cha Cement uanze bila malalamiko ya wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mashamba ya Marungu na Kwamkembe. Sheria inaelekeza kuwa majiji hayana mashamba yenye zaidi ya 50 hectors, lakini Jijji la Tanga katika Kata ya Marungu kuna mashamba tajwa hapo juu ambalo siku za karibuni wameuziwa na wamiliki wenye Hatimiliki, wameondoa wananchi waliokuwa wakilima mazao ya chakula na biashara, yaliyowezesha kupata kipato cha kila siku na kulipia ada za watoto. Waliahidi kuwakatia wakulima baadhi ya maeneo kwa ajili ya kilimo (mashamba yana zaidi ya ekari 2000 – 4000). Namwomba Mheshimiwa Waziri hili pia alishughulikie na kupata ufumbuzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kijiji cha miaka 21-Tanga. Hili ni eneo lililotwaliwa kinyume na taratibu. Nashauri, Mheshimiwa Waziri, Ofisi yake ilirudishe Halmashauri ya Manispaa ya watu wa Tanga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la Ngamiani Kusini Kati na Kaskazini. Eneo hili ni katikati ya mji kuanzia Barabara 1- 21, kuna nyumba zaidi 10,000 na ni eneo la kihistoria lakini wamiliki wake hawana hatimiliki wana Hati ndogo (offers) tu. Ushauri, naomba Wizara ya Ardhi isaidie katika kupima au kutoa Hatimiliki (99 years) ili wananchi waweze kutumia katika shughuli za maendeleo kama kukopa mabenki kwa ajili ya biashara na kilimo. Tukumbuke wananchi hawa wanalipa property tax.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu 30% ya makusanyo, naiomba Wizara irudishe 30% ya mapato ya ardhi katika Halmashauri ili zitumike kwa shughuli za Maendeleo.