Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. RUTH H. M0LLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru Mungu kwa kunipa nafasi ya kuchangia hoja iliyopo mezani. Pamoja na kazi nzuri inayofanywa na Waziri pamoja na Makamu wake, ninayo machache ya kushauri upimaji wa ardhi yote ya Tanzania ambayo ni 950,000 square kilometres, matumizi yake yajulikane na vile vile wamiliki halali wajulikane na kudhibiti wageni kumiliki ardhi nchini mwetu. Maeneo ya mlimani Usa Arusha kuna mashamba makubwa, mengine yana farasi kwa ajili ya burudani. Je, wenyewe hawa ni wamiliki halali? Je, matumizi yake ndiyo yaliyokubaliwa na Wizara au Kituo cha Uwekezaji?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itumie sekta binafsi katika upimaji na kupanga matumizi ya ardhi, kwa sababu wataalam Serikalini hawatoshi, vinginevyo itachukua miaka mingi sana zoezi hilo kukamilika. Serikali isitumie udhaifu wake kuumiza wananchi kwa mujibu wa sheria na kanuni. Kodi hulipwa kufuatana na eneo na matumizi ya ardhi, haiyumkiniki kusikia Tamko la Waziri kwamba, kodi italipwa kwa maeneo yote ambayo hayajapimwa. Je ni kosa la nani kwamba ardhi hiyo haijapimwa? Je, kodi hiyo italipwa kwa kigezo gani? Hakuna mtu wala taasisi iliyo juu ya sheria. Serikali yenyewe ndio imetunga Sheria ya Ardhi na lazima izingatie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kwamba kuna improvement kwenye mchakato wa kupata hati miliki ya ardhi, bado juhudi zaidi inahitajika, bado kuna watumishi wanaojivuta. Napendekeza utoaji hati miliki zisizo na migogoro kwa wakati kiwe kigezo cha kupima utendaji wa watumishi wanaohusika na utoaji wa hati miliki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali sasa ifanye maamuzi magumu ya kutatua kero ya migogoro ya ardhi iliyodumu kwa miaka mingi Serikali sasa iepuke kukwepa kufanya maamuzi ya kero hii kwa kuunda Tume na Kamati za kutoa mapendekezo miaka nenda, miaka rudi. Pamekuwepo na Kamati/Tume zaidi ya tatu na bado migogoro hii haijapatiwa ufumbuzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.