Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutoa pongezi za dhati kwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Watumishi wote. Kwa umakini wao ndani ya Wizara hii, kwa matokeo mazuri hadi sasa kwa wananchi na kuwapa matumaini ndani ya changamoto zao za ardhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na changamoto nyingi za ardhi kwa wananchi wetu na kupelekea miji yetu kuwa na majengo ndani ya ujenzi holela na maeneo yasiyopimwa yanaleta magomvi kwa wananchi wetu, mandhari ya mji itakuwa siyo nzuri kiusalama na malalamiko ya wananchi hayapati ufumbuzi kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunamwomba Waziri kwa umahiri wake aone uwezakano wa kuteua Kamati za Kugawa Ardhi ngazi ya Wilaya haraka iwezekanavyo, kwani Mkoa wa Rukwa unachipukia kukua na wananchi kuwa na kasi ya maendeleo yao na Wilaya moja (Nkasi) tu ndio yenye Kamati ya Kugawa Ardhi. Wilaya ya Kalambo na Sumbawanga tushughulikiwe, hali mbaya hivi sasa, miji yetu itashindikana kupangiwa hapo baadaye.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Rukwa upo pembezoni, lakini kwa mujibu wa taarifa ya Halmashauri zilivyotekeleza katika kutoa Hati miliki, Vyeti vya Ardhi ya Kijji, Hati Miliki za kimila. Ukurasa Na. 109 umedhihirisha kwenye jedwali Na.4 kwa Mkoa wa Rukwa haujafanya vizuri ni kutokana na rasilimali watu na rasilimali fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Mkoa wa Rukwa kuangaliwa kwa ukaribu zaidi, tukifahamu wazi kuwa tupo mpakani mwa nchi mbili (Zambia na DRC) ni vema tukavihakikisha vijiji vyetu na wenye maeneo kuwa na hatimiliki. Ni vema ukawekwa kipaumbele kwa mikoa ya pembezoni inayopakana na nchi mbalimbali, kupimiwa ardhi yao na kuipanga, kuepukana na migogoro ya ndani na nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuona umuhimu wa kupatiwa kibali cha kuajiri Maafisa Ardhi wa kutosha kwenye Halmashauri na vitendea kazi kulingana na mahitaji ya nchi kwa hii bidhaa adimu ya ardhi, kwa kila sekta. Ni vema Wizara ikaweka malengo ya utekelezaji kwenye Halmashauri na kufuatiliwa na kutathminiwa ili kila mmoja aweze kuwajibika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja.