Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga hoja mkono kwa asilimia mia moja. Baada ya hayo, natoa pongezi kwa Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wote wa Wizara na taasisi husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ardhi ni rasilimali muhimu kwa kilimo, ufugaji, viwanda, misitu, hifadhi na kadhalika, hatimaye kwa kutuhifadhi sote tutakapokufa. Bahati mbaya sana, Mungu alishamaliza kuumba ardhi. Kwa namna hii lazima usimamizi wa ardhi ufanyike kwa uangalifu mkubwa sana. Mpango wa matumizi bora ya ardhi unahitajika sana na Serikali ina wajibu wa kuziwezesha na kusimamia Halmashauri zote nchini, vijiji vyote na mpango wa matumizi bora ya Ardhi ya Vijiji chini ya Sheria ya Ardhi Na. 4 ya mwaka 1999.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto, yako mashamba makubwa katika maeneo mbalimbali ambayo hayaendelezwi vizuri na baadhi kuwa mashamba pori. Kwa kuwa baadhi ya mashamba haya; umiliki umebatilishwa na Hati kufutiwa, ni lini sasa mipango ya matumizi ya mashamba hayo itafanyika? Ushauri wangu ni kwamba, hayo mashamba yagawiwe vyama vya ushirika na vijiji, badala ya kugawa kwa watu binafsi. Kwani ni wengi na itasababisha migogoro zaidi, mbaya zaidi wananchi wengine huuza maeneo waliyogawiwa. Katika mashamba hayo yatengwe pia maeneo ya uwekezaji wa viwanda, ujasirimali wa vijana, shule, vituo vya afya na mahitaji mengine ya shughuli za Jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maamuzi yaliyofanywa mwaka 1973 kumilikisha mashamba makubwa ya kahawa kwa Vyama vya Msingi vya Ushirika huko Kilimanjaro, tunaona faida zake hadi sasa. Baadhi ya wawekezaji wanalipa kodi ya pango kwa Vyama vya Ushirika, lakini pia wanatoa maeneo kwa shughuli za jamii. Muhimu zaidi ni kwamba bado wanaendeleza zao la kahawa. Ombi, wawekezaji hawa washauriwe kuelimisha jamii inayowazunguka jinsi ya kuendeleza zao la kahawa kupitia CSR –Corporate Social Responsibility.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.