Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. DESPERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Pia nampongeza Waziri, Naibu Waziri, kwa kuchapa kazi, wamejitahidi kufanya kizalendo na wametatua migogoro mingi sana. Wananchi wamekuwa sasa na imani na Serikali yao kuhusu namna migogoro ya ardhi inavyoshughulikiwa. Wito wangu waendelee kufanya kazi na kusimamia haki za wananchi katika masuala ya ardhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Nkasi Kusini lina mashamba na hifadhi nyingi za kufanya wananchi kukosa ardhi ya kilimo. Nashauri Wizara kuona kama mashamba yaliyopo Jimboni yanaendeshwa kwa ufanisi au la ili kuweza kutoa uamuzi wa kuongeza ardhi kwa wananchi.

- Shamba la Nkundi linalotumiwa na Mheshimiwa Mzindakaya. Wananchi jirani hawana ardhi ya kutosha na sehemu kubwa halitumiki ipasavyo lipunguzwe wapewe wananchi wangu.

- Shamba la Kalambo Ranchi lina ukubwa wa hekta 23,000, lakini lina ng’ombe 710 tu. linatumika chini ya kiwango eneo kubwa halitumiki. Lipunguzwe wapewe wananchi wangu.

- Shamba la Milundikwa kwa eneo walilopewa JKT mwaka jana ni kubwa lote halitumiki na wananchi wengi wanalima ndani bila kuruhusiwa kwa sababu ya ukosefu wa ardhi ya kilimo, lipunguzwe wapewe wananchi.

- Shamba la China linatumika lakini tuone kama lazima lote liwe kwa mtu mmoja wakati watu wengi hawana ardhi ya Kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mamlaka ya Misitu ya TFS imepora ardhi ya Kijiji cha Kasapa na kufanya kijiji kukosa kabisa eneo la kulima. Naiomba Wizara ione namna ya kuwasaidia wananchi wa kijiji hiki. Maeneo yao ambayo wamekuwa wakilima miaka yote, tangu miaka ya 1956 yametwaliwa na kufyeka mazao yao. Wizara inisaidie kutatua mgogoro huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Vijiji vya King’ombe, Mlambo, Ng’undwe, Mlalambo, Nkata na Kasapa vinadaiwa kuwa Ndani ya Mbuga ya Lwanfi Game Reserve, kwa hiyo, wananchi hawana ardhi na wanapata usumbufu mkubwa. Kamati ya Migogoro ya Ardhi itembelee kuona shida iliyopo.