Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nimpongeze Rais wangu kwa kazi kubwa anayoifanya kwa kuwatumikia wananchi hasa wale wanyonge. Pia nimpongeze Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi pamoja na timu yake kwa hotuba yake nzuri iliyojaa matumaini makubwa yenye nia ya dhati na yenye kugusa na kuondoa kero zote za Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nishauri Serikali iwape fedha Wakala wauzaji wa vifaa vya ujenzi vya bei nafuu. Kama kweli Serikali inataka Watanzania wenye kipato cha chini wawe na uwezo wa kununua nyumba za bei nafuu. Basi tuwawezeshe Wakala wa vifaa vya Ujenzi. Pamoja na hayo, wakala wawe wanatoa elimu ya ufundi. Kwa hiyo, wakala wale wapewe uwezo ili wafike mkoani hadi wilayani kutoa elimu kwa vijana wetu wa Kitanzania ili vijana wetu wakishapata elimu waweze kujiajiri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia niishauri Serikali yangu, iharakishe na kutoa mafungu katika Wilaya ili mafungu haya yaendane na kasi ya upimaji na upatikanaji wa hati kwa haraka. Kwa mfano, Wilaya ya Lushoto wananchi wapo tayari kupimiwa na kupewa hati lakini kuna ukiritimba katika idara ya ardhi. Kwa hiyo, tunaomba Mheshimiwa Waziri afuatilie hili suala katika Ofisi ya Ardhi Lushoto ili wananchi wangu wasinyanyasike pindi tu wanapotaka kupimiwa shamba na hao wananchi wameshajua umuhimu wa kupima ardhi na ukizingatia watu wanahitaji kupata mikopo kwenye mabenki. Pamoja na hayo kuna rushwa sana katika Idara ya Ardhi, maana wananchi wengi wametoa fedha zao ili wapate hati lakini fedha zinaliwa na hati hawapati. Naomba Mheshimiwa Waziri aondoe tatizo hili katika Wilaya ya Lushoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niishauri Serikali yangu Tukufu ili migogoro katika nchi hii iishe ni kupima ardhi yote ya nchi hii. Naamini maeneo yote yakipimwa na kila mtu akamiliki ardhi kihalali migogoro hii itakwisha. Pia niiombe Serikali yangu itenge mafungu ya kutosha yaende katika kupima ardhi kuliko kutegemea wafadhili. Mheshimiwa Waziri nimependa sana zoezi lile linaloendelea katika Mkoa wa Morogoro, Wilaya ya Kilombero. Kwani ni mpango mzuri na wenye tija. Kikubwa wapewe mafungu ya kutosha ili kuharakisha zoezi lile. Pamoja na kuwaongeza wataalam ili kumaliza zoezi kwa haraka na ikiwezekana ifikapo 2020 Ardhi yote ya Tanzania iwe imeshapimwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga hoja kwa asilimia mia moja.