Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa hotuba nzuri ya bajeti. Nianze na mgogoro wa shamba la Tumaini lenye ukubwa wa ekari 4,000 ambalo Mheshimiwa Waziri, kwa uzalendo wa hali ya juu wa kuthubutu alifuta hati miliki ya shamba lile. Hicho ni kitendo cha kijasiri kabisa na chenye kuendana na utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM).

Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua kuwa suala hili lipo mahakamani, lakini wananchi wa Mafia wanaunga mkono uamuzi wa Mheshimiwa Waziri wa kuifuta hati na kulirejesha shamba miliki kwa wananchi. Ombi letu ni mara baada ya shauri lililopo Mahakamani kumalizika tunaomba mgao wa shamba hili ufanywe na Halmashauri yetu ya Mafia kulingana na vipaumbele vyetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii pia kumwomba Mheshimiwa Waziri alifute shamba la ng’ombe ambalo limebaki pori kubwa na ongezeko la watu limepelekea ongezeko kubwa la mahitaji ya ardhi kisiwani Mafia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la Nyumba la Taifa (NHC); Halmashauri ya Mafia tumetenga eneo kubwa la kutosha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba kupitia Shirika hili. Nimwombe sasa Mheshimiwa Waziri, aagize uongozi wa Shirika hili kuanza mradi huu haraka sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na naunga mkono hoja.