Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. George Mcheche Masaju

Sex

Male

Party

Ex-Officio

Constituent

None

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nikushukuru kwa kunipatia hii fursa na mimi nichangie. Nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa mimi kupata fursa kipindi hiki lakini niwapongeze sana Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa hotuba yao nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua nafasi hii kuwatakia heri ya Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani Waislamu wote wa Tanzania wanaofunga. Mwenyezi Mungu atubariki, mnapokuwa mnashiriki toba hii mshiriki na sisi waovu wengi mtuombee pia. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Magufuli kwa hatua aliyochukua kuhusiana na mchanga. Unajua Katiba yetu, Ibara ya 27 imeeleza vizuri wajibu wetu kama Serikali kuhusu matumizi ya maliasili tulizonazo na hii ni maliasili. Naomba Waheshimiwa Wabunge wote kwenye hili tushirikiane na Serikali kuhakikisha kwamba tunalinda maslahi ya Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hili hakuna sababu ya kulaumiana, ni mapema sana kuilaumu Serikali kwa hatua ilizochukua. Zimeundwa Kamati mbili, hii ya kwanza na Kamati nyingine ya sheria ambayo inaangalia pia na mikataba. Kati yetu hakuna hata aliyewahi kuona mikataba hii au aliye na hii mikataba. Kwa hiyo, naomba tutambue kwamba sisi ni familia moja, tunayoyasema leo yatakuja kuturudia, hatuwezi tukaanza kuilaumu Serikali yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii pia kuwashauri Waheshimiwa Wabunge wenzangu kwamba tunapochangia tuchangie kwa hekima, kwa heshima na kwa nidhamu kubwa kwa maslahi ya Taifa letu na kwa viongozi wa Taifa hili na kwa lugha ya Kibunge. Tunazo kanuni
zinazotuongoza, mimi sioni hii ina maslahi gani kwa watu, kwa sababu tusichangie kana kwamba tunachochea watu wengine watuchukulie hatua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba sana Waheshimiwa Wabunge waiunge mkono Serikali kwenye suala hili. Ni suala ambalo lilipaswa lituunganishe sisi kama watu wamoja kwa ajili ya maslahi ya Taifa letu. Hii baadhi yetu mnayoshabikia kwamba tukishtakiwa, hakitashtakiwa Chama cha Mapinduzi kama ni liability itakuwa ni ya Serikali nzima. Hapa hawachagui kwamba ni huyu au ni yule. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana kwa kunipatia nafasi ya kuchangia, naomba tuendelee kuipatia Serikali ushirikiano, Wizara inafanya vizuri, wawekezaji kwa kweli wataendelea kuja. Nimerudi asubuhi hii kutoka Uganda kusaini mkataba ule wa bomba la mafuta na ninyi wenyewe mmeona Waziri wa Viwanda na Biashara amewasilisha hapa bajeti yake wiki moja iliyopita na mwitikio umekuwa mkubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba Waheshimiwa Wabunge tunapochangia, tusichangie kwa kuogopesha watu kwamba mambo ni mabaya sana. Kila kilichofanyika kwenye hatua hii ya michanga ni halali kisheria na kimikataba. Kwa hiyo, tutakapokamilisha ile ripoti ya Kamati ya Sheria tutaona tufanye nini kwa sababu Sheria ya Madini inatoa fursa ya ku-review mikataba ile kila baada ya miaka mitano. Sasa mnawezaje ku-review kama hamko well informed? Yaliyotokea sasa kwenye taarifa hii yanatusaidia sisi kuwafuata wenzetu na kuwaambia jamani hiki ndicho tulichoona, turekebishe hapa, sasa kosa lake ni nini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya, naunga mkono hoja asilimia mia moja.