Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Riziki Shahari Mngwali

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze kwa kurudia masikitiko yangu niliyoyatoa katika Mkutano wa Bajeti ya mwaka jana kuhusu muda mchache unaotengwa kujadili hoja ya Wizara hii muhimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukumbuke kuwa Bunge lako Tukufu ni Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hivyo si haki kulinyima muda wa kutosha kujadili suala hili muhimu la Muungano. Ifike muda uongozi wa Bunge ubadili utaratibu uliozoeleka wa kutenga muda mchache wa kujadili Wizara za Muungano, zikiwemo Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, pamoja na Wizara ya Muungano, (Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano).

Mheshimiwa Mwenyekiti, inatia uchungu kusikiliza na kusikia yaliyosemwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu hali ya utendaji ya Wizara hii na hali ya Balozi zetu nje ya nchi. Hivi ni kweli Serikali haioni umuhimu wa kuwa na majengo mazuri yenye hadhi kuwakilisha taswira ya nchi yetu? Ni aibu kubwa kwa nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe Waziri husika aisome kwa makini hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani na ayafanyie kazi yaliyomo kwa uadilifu mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni jambo la kusikitisha kuona Wizara na Serikali kwa ujumla kuendelea kufanya kazi kwa mazoea. Bado Wizara hii haiainishi mkakati madhubuti wa kutekeleza Sera yetu ya Mambo ya Nje hasa kuhusiana na diplomasia ya kiuchumi. Hotuba ya Waziri haina taarifa yoyote kuonesha mkakati wa kuhakikisha nchi yetu inapata wawakilishi nje ya nchi na watendaji kwenye Wizara husika wenye sifa na walioandaliwa ipasavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watendaji wa Wizara yetu ya Mambo ya Nje wanatakiwa kuandaliwa katika maeneo mahsusi ya maeneo (regional specialization), kisha watendaji hawa walioandaliwa ipasavyo ndio wapande ngazi Wizarani na hatamae kuwa wawakilishi (mabalozi) wetu nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, inakuwa ni mazoea, kwa Serikali kuteua mabalozi wa kutoka nje ya Wizara. Hii inakatisha tamaa watendaji wa Wizara lakini pia inadhalilisha fani ya mambo ya nje (foreign service). Foreign service ni profession kama zilivyo professions nyingine. Wahusika hupata mafunzo na kukidhi vigezo maalum.

Mheshimiwa mwenyekiti, wengi wamesema kuhusu Chuo chetu cha Diplomasia - Kurasini. Chuo hiki kitendewe haki, kipewe hadhi stahiki kwa kuhakikisha kinawezeshwa kujenga mazingira ya kufundisha maafisa wetu na vijana wetu kwa ujumla. Wizara ikisaidie Chuo kuwa na walimu mahiri na wenye maslahi mazuri.