Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia hoja hii ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashairiki kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Wizara ishughulikie suala la Watanzania wanaonyanyaswa katika nchi za nje hasa huko Uarabuni. Kuna mabinti wengi wanateswa na hata wengine wanauawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wengi hawana uelewa wa Wizara, hivyo kukosa fursa. Hivyo naiomba Wizara kutoa elimu kwa wananchi wa Tanzania kazi ya Wizara hii. Pia majengo mengi ya Balozi ni chakavu, naiomba Serikali ikarabati majengo yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la diaspora bado halina nguvu, ninaiomba Serikali ilichukulie kwa umuhimu kwani inachangia katika kukuza uchumi wa nchi yetu kwa kuwapa fursa mbalimbali za uchumi kisheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa bajeti ya Wizara huchelewa, naiomba Wizara kuhakikisha bajeti inatolewa kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, akina mama wengi nchini ni wajasiriamali, mfano akina mama wana viwanda vidogo vidogo kama vile vya kushona vikapu, kutengeneza vinyago, vyungu na vitu vingine, ninaiomba Wizara iwakumbuke akina mama ili waweze kuuza bidhaa zao nje ya nchi na waweze kukuza uchumi wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itoe kipaumbele katika kulipa michango ya nchi yetu kwenye Taasisi za Kimataifa ili kuepusha kukwamisha uendeshaji wa taasisi hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.