Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaunga mkono hoja ya Wizara hii, hata hivyo nina ushauri kwa Serikali kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, issue ya wakimbizi katika Mkoa wa Kigoma tangu tupate uhuru, Mkoa wetu wa Kigoma umekuwa ndiyo makazi ya wakimbizi watokao DRC, Burundi, Rwanda. Ni vizuri sasa Serikali yetu ikaanza mkakati wa kuwarejesha wakimbizi hawa kwao, kwa kiwango kikubwa DRC ipo salama katika maeneo mengi, kwa nini raia wao waliopo Nyarugusu mkoani Kigoma wasirejeshwe kwao na/ au kulindwa katika nchi yao? Kwa nini makambi haya yasifunguliwe ndani ya nchi zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, athari za wakimbizi ni nyingi sana ikiwa ni pamoja na usalama wa wanavijiji wetu, kusambaziwa maradhi mengi ikiwemo maradhi hatari ya Ebora na mengine mengi, Kigoma sasa inahitaji utulivu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jumuiya ya Kimataifa kusaidia maeneo yaliyoathirika na ujio wa wakimbizi katika Mkoa wa Kigoma, lazima Serikali sasa ibuni na ije na mkakati wa namna bora wa kusaidia wananchi wa Kigoma ambao wamehifadhi wakimbizi tangu enzi ya Uhuru miaka ya 1960. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kusaidiana na Wizara ya Mambo ya Ndani kaeni pamoja ili mjenge programu ya aina hii; “Refugees Host Area Program” Mheshimiwa Waziri do something on Kigoma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.