Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. CAN.RTD Ali Khamis Masoud

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mfenesini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. KAN. MST. MASOUD ALI KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, umefika wakati sasa kuweka kipaumbele kutekeleza miradi ya ujenzi wa ofisi za balozi zetu nchi za nje ili kupunguza gharama za kukodisha nyumba kwa watendaji wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni muhimu sana kuibana Wizara ya Fedha ili ikamilishe fedha za ujenzi wa ofisi ikiwa pamoja na ukarabati wa jengo la Msumbiji ambalo endapo litamalizika basi litakuwa na tija na ukombozi mkubwa kwa nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado kuna utata wa fedha zilizopelekwa Msumbuji na fedha iliyotolewa na Wizara ya Fedha. Je, shilingi milioni 900 ndiyo iliyotolewa au bado ipo fedha iliyobaki Wizarani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba utaratibu uliotumika Msumbiji wa kukarabati jengo la Balozi kwa kutumia fedha za pango ambazo zilikuwa zipangishiwe nyumba ya Balozi kufanyiwa ukarabati ni jambo jema sana, sehemu nyingine ifanyiwe ukarabati.