Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nimpongeze Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa anayoifanya kutumikia Watanzania hasa wanyonge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niishauri Serikali yangu tukufu itoe ajira kwa Balozi zetu hasa wachumi, kwani inavyoonesha kwenye Balozi zetu wachumi ni wachache mno, hii itapelekea kukuza na kuitangaza nchi yetu kiuchumi katika mataifa ya nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna vijana wengi wanaomaliza Chuo cha Diplomasia lakini wanakaa kwa muda mrefu bila kupata ajira, ni ushauri wangu vijana hawa Serikali iwachukue kwa mkataba wa muda wakati huo huo wakiendelea kupata uzoefu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niishauri Serikali yangu, kuna hawa wageni kutoka nje na wamekaa kwa muda mrefu na kuwekeza hapa nchini na wakati huo wanasaidia misaada mbalimbali. Mfano kujenga shule, kujenga zahanati na kujenga hosteli kwa njia ya kusaidia wananchi wanaoishi maeneo yanayowazunguka. Pamoja na hayo wafadhili hawa kwa sasa wamezuka na wanataka kurudi makwao, sababu ya kurudi kwao wanasema kwa sasa wamezeeka na pia kodi ya makazi ya kuishi nchini ni kubwa hivyo labda Serikali iwasaidie kupunguza fee hiyo au kuondoa kabisa kwa sababu bado wanaendelea kusaidia jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu kwa Serikali watu hawa wangepewa uraia wa Tanzania ili waweze kusaidia jamii yetu, ukizingatia watu hawa wamechoka na wamezeeka.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu mbariki Rais wetu, uzidi kumpa afya na nguvu na umzidishie umri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.