Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa muda huu mfupi niliopewa nitakuwa na jambo moja tu la kulielezea, nalo ni hali halisi ya balozi zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama na takribani wiki mbili zimepita tulipata fursa ya kutembelea Balozi mbalimbali ikiwemo Sweden, South Africa na Maputo. Mimi binafsi nilipata kutembelea Ubalozi wa Maputo, kwa hiyo, saa hizi nitaelezea hali halisi ambayo tumeiona kwenye Ubalozi wetu na mradi ambao unaendelea pale. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutambua mchango mkubwa ambao Taifa letu liliutoa kwa nchi ya Msumbiji, Serikali hiyo ilitupa jengo la Ubalozi, nyumba ya Balozi na uwanja ambao uko mkabala na jengo hili la ghorofa tisa. Mwaka 2012 Serikali iliamua kufanya matengenezo ya Ubalozi huu kwa sababu hili jengo limeanza kutumika toka mwaka 1975. Sasa kwa kuwa mradi huu ulikuwa viable tukapitisha kuwa jengo hili lifanyiwe ukarabati. Mradi huu umechukua muda mrefu sana, sasa hivi ni takriban miaka mitano na imeisababishia Serikali hasara kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka sasa hivi tunatumia dola za Kimarekani 240,000 kila mwaka kuhakikisha tunalipia nyumba ya Balozi na watumishi kwa ajili ya kuendesha shughuli za Ubalozi nchini Msumbiji. (Makofi)

Mheshimiwa Waziri, you know this is not reflecting well on our part. Haiwezekani tukawa tumepewa jengo, tumepewa kiwanja, tumepewa nyumba ya Balozi na sisi tunaendelea kupoteza pesa hizi kila mwaka kulipia pango.

Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri, wewe umekuwa ni mwanadiplomasia mzuri, nakuomba, hizi pesa ambazo zinaombwa kuhakikisha tunamaliza jengo hili zipelekwe kwa wakati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati tuko Msumbiji tuliweza kuonana na Mkandarasi akasema anadai dola za Kimarekani 888,000. Akipewa pesa hizi, ataweza kukamilisha jengo hili within two months. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kulinda heshima ambayo nchi ya Msumbiji ilitupa Tanzania, tuhakikishe tunaendeleza hata kile kiwanja ambacho kiko pale. Kama Serikali inashindwa kujenga kiwanja hiki, basi iwashirikishe Shirika la Nyumba waweze kwenda ku-develop lile eneo kwa sababu demand ya real estate Mjini Maputo ni kubwa sana. Tukimaliza ghorofa hili tuna uwezo wa kuiingizia Serikali shilingi milioni 600 kwa mwaka ambayo itatusaidia sisi ku-service ule Ubalozi wetu na kusaidia balozi mbalimbali ambazo zinazunguka Kusini mwa Afrika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maelezo haya, namwomba Mheshimiwa Waziri ahakikishe ule Ubalozi wa Msumbiji unatengenezwa kwa wakati, image yetu pale haionekani vizuri. Nina uhakika miezi miwili ijayo tutaweza kufungua Ubalozi huu ili uweze kutumika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi.