Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Peter Joseph Serukamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza nimpongeze Waziri lakini nianze kwa ku- quote maneno aliyoyasema Deputy Managing Director wa IMF Dar es Salaam kuhusu kodi. Pamoja na kutusifia lakini alisema maneno yafuatayo:

“It is crucial to mobilize more private public resource within Tanzania especially by strengthening tax collection and fair and predictable tax regime. Ametumia maneno, strong, fair and predictable tax regime. Anasema, this is an area where Tanzania has fallen behind its neighbours. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kusema la kodi kwa sababu biashara, Waziri wa Fedha naomba hili likae kichwani, wafanyabiashara wote Tanzania ni partner wake, wafanyabiashara wa nchi hii ni partner wa nchi hii na nitasema kwa nini ni partner. Wafanyabiashara wa nchi hii wanatupa asilimia 30 ya corporate tax kila mwaka, kwa hiyo, maana yake na sisi tunazo sababu za kufanya biashara iendelee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, biashara ikienda vizuri, Serikali inapata asilimia 30, Serikali itapata Pay As You Earn, itapata kwenye insurance, itapata kwenye pension funds. Kwa hiyo, tunalo jukumu kama Serikali na niwaombe sana watu wa Wizara ya Fedha, tufanye kazi ya kukuza biashara Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda leo Kariakoo, yuko mfanyabiashara mmoja ni mdogo sana, natoa mfano, mwaka 2005 alikuwa anaingiza makontena manne kila mwezi analipa shilingi milioni 72, leo hii mambo yamekuwa magumu anaingiza kontena moja kila baada ya miezi miwili,
aliyepoteza ni nani? Ni sisi Serikali. Hii nasema lazima niwaombe sana tujitahidi tuwalee wafanyabiashara. Kudhani wafanyabiashara ni wezi, wanatuibia siyo sahihi sana, naombeni sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili wameanzisha task force, task force inakwenda kwa wafanyabiashara imerudi mpaka 2009. Wanajua maana yake ni nini? Kwa sababu walikwepa kodi kule zamani wakiwaambia leo wailipe, yes watalipa lakini hao wanakufa kibiashara. Kwa hiyo, mwezi unaofuata hawataweza kulipa kodi. Ama kitakachotokea ile task force, wanakwenda wanakaa mezani, ni rushwa! Mtu atakuja anadaiwa shilingi bilioni tano hajalipa miaka sita, anaambiwa sasa sikiliza, lipa shilingi bilioni moja, tupe shilingi bilioni moja, shilingi bilioni tatu tunakusamehe, ndiyo kinachoendelea huko mtaani. Niwaombe sana watu wa Wizara ya Fedha, tuamue sasa, tusiende nyuma, tuanzie sasa kwenda mbele kuhakikisha kila mtu analipa kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni Sheria ya VAT. Sheria yetu ya VAT haitambui vivutio tunavyowapa wawekezaji, kwa maana ya capital goods na deemed capital goods. Nimwombe Waziri, tutoze kodi kwenye bidhaa siyo kwenye production. Tukianza kudhani unataka kuwekeza leo unataka uanze kupata, hakuna atakayewekeza. Mimi nasema jamani haya yanayofanyika, duniani wenzetu wanafanya, ukimuachia mtu azalishe, Dangote alienda pale Ethiopia akaambiwa tunakupa umeme rahisi, vivutio, baada ya kuanza kuzalisha bei ya cement ikashuka by 60% maana yake watu wengi wakajenga, utapata kodi kule mbele. Kwa hiyo, niwaombe wenzetu wa Wizara ya Fedha tuyasimamie haya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine naomba tu- harmonise NIC pamoja na Sheria ya Fedha. Kama inatokea NIC inatoa vivutio under TIC, Sheria ya Fedha inakuja hapa haivikubali ni contradiction, hatueleweki. Ndiyo maana tumeambiwa our tax regime is unpredictable, wenzetu ndivyo wanavyotuona. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala la TIB, Waziri wa Fedha, naomba leo atuambie anaihitaji TIB ama haihitaji? Kutoweka fedha TIB mimi sielewi maana yake ni nini. Duniani kote wanaweka hela kwenye Benki zao za Maendeleo ili zisaidie katika maendeleo hasa ya viwanda na kila kitu. Sisi tunasema tuna maendeleo ya viwanda, tunataka kwenda kwenye viwanda lakini hakuna hela TIB. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninacho kitabu cha maendeleo cha mwaka mmoja, TIB imetajwa by the way. Hakuna anywhere imetajwa TIB inawekwa pesa. Tuliambiwa watapewa shilingi trilioni moja, najua mwaka huu wamepanga kuwapa shilingi bilioni 94, watafanya nini kwenye maendeleo? Jamani ukienda China, Brazil, wapi wana embrace Development Banks zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaomba sana watu wa Wizara ya Fedha, waweke commitment hapa. Leo TIB ukimpa shilingi trilioni moja anazi-leverage atapata hata zaidi ya bilioni nyingi tu, anakwenda kwenye masoko nje, analeta through DIF, anachangia kwenye maendeleo yetu. Mimi sijui kuna nini pale Wizara ya Fedha, hawataki kuisaidia TIB. Watuambie, kama hawaitaki tuifunge lakini kila siku ukisoma kwenye vitabu humu inashangaza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala la investment model yetu. Waziri wa Fedha, lazima tuchanganye tax, debt na investment. Kwa nini nasema investment, ili sasa uweze kuleta PPP. Ukisoma kwenye kitabu PPP haisemwi, ukisoma kwenye hii ya maendeleo, hakuna PPP tunaisema by the way. Hivi mbona wenzetu wote, China, Malaysia na kadhalika wana embrace PPP, what is wrong with us? Hatuwezi kujenga nchi hii kwa kodi peke yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzetu barabara, umeme, wanajenga kwa hela za watu, unaweka legal framework yenye clarity. Hata agriculture, mimi nawasikia wenzangu wanasema tuweke hela kwenye agriculture, tusipo-embrace kwenye commercial farming hatutaendelea. Commercial farming ni more capital, itaajiri watu wengi na italeta hela kwenye products za kwenye viwanda lakini wakubwa hawasemi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, deni la Taifa, wanasema linahimilika, linahimilika yes, kwa sababu wanachukua debt sustainability ratio, fine. Mimi naomba, umefika wakati tuliangalie deni la Taifa na revenue base yetu ndiyo watajua kwamba deni letu halihimiliki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni transit trade, VAT. Jamani tumesema mwaka jana, auxiliary VAT kwenye transport inaua hii industry. Waziri hapa anasema uchumi umekua kwa asilimia saba na moja ya mchango ni kwenye transport, Waziri wa Fedha, transport imeshuka. Aende akaulize wenye malori, malori yaliyokuwa yanakwenda nje yalikuwa 23,000 leo yamebaki malori 11,000.

Yakibaki malori 11,000 maana yake ni nini? Mafuta hawanywi, madereva hawana kazi, tairi hakuna, magari 12,000 yako nyumbani, mabenki hayalipwi kwasababu tumeua hii industry. This is our dear country, naombeni tufanye wanavyofanya wengine. Nimesikia auxiliary VAT hawataki kuitoa, hawataki kuitoa kwa sababu gani? Wanapata nini kwa kuiweka? Ni kama vile ambavyo tunasema suala la kuwakusanyia Congo kodi tuache, haitusaidii ni disincentive kwenye economy yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni deni la ndani, Waziri naomba tulipe deni la ndani. Leo hali iliyoko nchini ni kwa sababu hatulipi deni la ndani. Naombeni sana tuhangaike na kulipa deni la ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala la Federal Reserve zimepanda interest rate. Mimi niliisema mwaka jana, naomba leo niiseme, najua watu wa Wizara ya Fedha hili hawataki hata kulisikia. Leo hii Federal Reserve imepanda to
0.75 maana yake ni nini? Kwa sababu mikopo yetu yote ni faulting libel maana yake inakwenda kupanda, maana yake Waziri wa Fedha utakapoanza kulipa deni la Taifa kesho siyo hela uliyolipa mwaka huu, revenue inashuka, deni la Taifa linapanda kwa sababu ya interest rates, what do we do? Wenzetu wana-swap, let us fix this interest. Jamani wote wanafanya, Kenya wamefanya, Uganda wamefanya, wamezi-fix interest rates kwa sababu vitality kwenye economy ya Marekani ni kubwa, inatu-affect sisi ambao tumekopa kwa dola lakini wenzetu hawataki kusema. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mifuko, nasikia mnataka kuunganisha mifuko ya pension fund, jambo jema lakini niwaombe Waziri wa Fedha, kabla hawajaiunganisha tulipe madeni yao yote. Maana hii itakuwa ni kukwepa majukumu yetu. Mifuko inaidai Serikali, hakikisheni mifuko yote inalipwa, tufanye hesabu za mwisho ndiyo tuamue kuiunganisha. Kwa kufanya hivyo, tutafanya vizuri sana kama nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nimalizie kwa kusema suala la mwisho na narudia kwa kweli ni suala la biashara. Nawaombeni sana wakubwa, tu-embrace biashara Tanzania. Ukienda leo Kariakoo jamani siyo Kariakoo ya miaka mitatu iliyopita. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi niwaambieni kwa mtu aliyesoma tax, somebody akiwa analeta makontena 100, akakwepa makontena 50 akalipa kodi ya makontena 50 anaingiza kwenye market, uwe na hakika atakapoenda mwezi ujao ataleta makontena 150. Kwa hiyo, anapokuja anakukuta umejiandaa unampiga kodi makontena 120 maana yake wewe base yako ya kodi imepanda. Akileta 100 ukasema lazima ulipe yote, fine, it is a good idea lakini mwezi unaokwenda ataleta makontena 70, aliye-loose ni wewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima tutengeneza utaratibu wafanyabiashara wakue na sisi tukue. Ukidhani unaweza ukafunga milango kwamba hapa hakitoki kitu ni jambo jema lakini mwisho wa siku we will be a looser as a country. Kwa sababu ukiangalia trend ya kodi imekuwa
inapanda, kama inaanza kushuka lazima tujiulize haraka sana, tatizo kwa vyovyote vile ni suala tunavyo-handle business as a country.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na naunga mkono hoja.