Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hongera sana Mheshimiwa Waziri, Dkt. Philip Mpango na Naibu Waziri, Mheshimiwa Dkt. Ashatu Kijaji kwa kazi nzuri mnayolifanyia Taifa letu. Kazi kubwa ni pamoja na ongezeko la ukusanyaji wa mapato ambayo yamepelekea kulipa deni la Taifa kwa kiasi kikubwa. Nina ushauri katika eneo la misamaha ya kodi inayotolewa katika sekta mbalimbali kama vile kilimo, mifugo, afya, michezo, elimu na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ingekuwa vema wataalam wakaisaidia Wizara kutaja vitu vyote vionekane katika sheria ili kuondoa usumbufu kwa maafisa wa TRA wanaohusika na utozaji kodi, kwani inapotokea jina la kitu husika hakikutajwa katika sheria wanalazimisha kutoza kodi. Vilevile sera ya michezo inaelekeza kutoa unafuu wa kodi kwa vifaa vya michezo na kutotoza kodi kwa vile vifaa ambavyo vimetolewa kama msaada.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo hili kuna malalamiko mengi kutoka kwa wananchi ambao ni wadau wa michezo kwamba vifaa vya michezo vilivyotolewa kama msaada vinaozea bandarini. Hata hivyo, Mheshimiwa Makamu wa Rais aliahidi suala hili kufanyiwa kazi siku alipokuwa akizindua mazoezi ya viungo ya kila Jumamosi ya pili ya kila mwezi mwaka jana Novemba, 2016. Naomba Wizara ilifanyie kazi suala hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naitakia Wizara kila kheri na naunga mkono hoja. Ahsante.