Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Bahati Ali Abeid

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mahonda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. BAHATI ALI ABEID: Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Wizara iondoe kodi na tozo ya mitambo na vifaa vya miradi ya gesi ili miradi hii iweze kuendelea na utekelezaji wake kama ilivyopangwa kwani wakati mwingine miradi hii huwa ina mitambo mizito na mikubwa. Kama TANROADS huwa wanataka sheria iliyowekwa kwa ajili ya tozo hizi ziendelee kama zilivyo. Ni sawa, lakini miradi hii au mashine hizi ni za muda mfupi, siyo za kila siku. Naomba tuondoe tozo hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.