Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Sekta ya Mazao ya Misitu Mafinga/Mufindi vs TRA Mkoa ni kubwa na inakua kwa kasi hasa Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini hususan Iringa na Njombe. Ni Sekta ambayo tulishirikisha wadau katika masuala yanayohusu sekta hii. Serikali itapata mapato na sekta ita-grow. Hata hivyo, hali ilivyo ni kinyume kabisa na hapa naomba niwe open.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hulka yangu kama Mbunge niliyetokea kwenye Utumishi wa Umma, siyo mtu wa kupiga mayowe, lakini ninakoelekea nahisi nitaanza kupiga kelele na mayowe jambo ambalo siyo jema, kwa jitihada zangu kufuatia usumbufu uliokithiri kwenye check point ya Iringa. Niliwasiliana na Waziri na Kamishna Mkuu akiwa Kidatu kuhusu usumbufu na manyanyaso wanayopata wavunaji na wasafirishaji wa mazao ya misitu/mbao pale kwenye check point ya Iringa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nifafanue kidogo. Uvunaji wa mbao uko wa aina kama mbili. Kwenye msitu wa Serikali ule wa Sao Hill ambao mfumo wake uko very clear kwenye misitu na mashamba ya watu binafsi ambapo nako kuna mashamba makubwa kama kuanzia ekari hamsini na kuendelea. Ni wenye mashamba madogo kama ekari moja, mbili mpaka kumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, inatokea mvunaji mdogo ananunua kwa kuungaunga mpaka kujaza semitrailer au Scania ile tunaita kipisi, mtu huyu anasafirisha mbao lakini akifika check point ya Iringa anadaiwa risiti ya mashine ya EFD. Sasa mtu huyu aliyenunua kwa mwanakijiji ambaye hajui chochote kuhusu EFD, itatoka wapi? Maana nimenunua kijijini kwa mkulima na hana mashine, maana yeye kauza nusu ekari ili apate fedha ziende kumlipia ada mtoto au matibabu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mjasiriamali huyu anatozwa faini kati ya Sh.250,000/= mpaka Sh.750,000/= wakati mzigo wake hauzidi Sh.3,000,000/= kabla ya gharama za usafiri. Mbaya zaidi watu wanatishwa, wanalipa fedha na hawapewi risiti. Fedha inaingia mfukoni mwa individual. Mtu huyo huyo akifika Kibaha anabugudhiwa kwa kuwa ni syndicate, wanapigiana simu na wale wa check point ya Iringa kisha wanamruhusu huyo mjasiriamali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilifanya nini? Baada ya mawasiliano na Mheshimiwa Waziri na Kamishna wa Kidatu, nilipewa mawasiliano na Kamishna anaitwa Yusufu tukashauriana TRA Mkoa ikae na wadau tujadili muktadha mzima wa biashara hii ili Serikali ipate chake na wajasiriamali walipe bila kufilisika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, cha kusikitisha (lazima niwe wazi) Meneja wa Mkoa akiwa ana shaka lakini nikawasihi kuwa mkutano nitausimamia na utakuwa wa amani na wa kujenga. Nashukuru tulikaa na tukaafikiana kuunda Task Force ikihusisha TRA na wafanyabiashara wa mbao. Hata hivyo bado uonevu unaendelea. Juzi hapa malori yamezuiliwa siku tatu. Kiuchumi hii ni hasara kubwa mno. Sitetei kuwa wasilipe, hapana tuwe na utaratibu ambao utazingatia mazingira halisi ya biashara hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sina kawaida ya ku- personalize issues, lakini kuna mtu anaitwa Onyango ana damage Serikali kwa vitisho, kauli na hata matusi. He is not coorperative at all. Amegeuka kero kuliko kuwa facilitator, labda kwa kuwa amekaa miaka mingi Iringa watu wa Iringa, Mafinga, Kilolo na Mufindi are very humble hawahitaji vitisho zaidi ya kuelekezwa tu, Mawakala wanawatisha watu, wanachukua rushwa, Onyango akipigiwa simu ni vitisho tu. Please naomba mtushirikishe mtusaidie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nauliza hivi nakisi ya bajeti ni 3.9% au ni 11.9%? Kwa sababu mikopo na misaada ni around trilioni 11 lakini deni la Taifa ni trilioni tisa na mikopo siyo uhakika. Kwa nini tusisimame kwenye kilio chetu? Naona kama we are not realistic.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitachangia zaidi kwenye bajeti; lakini hili la mbao mlitazame. Hii sekta ni uchumi mkubwa na angalieni Mufindi inavyochangia pato la Taifa, one of the source ni mbao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawasilisha.