Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Ali Salim Khamis

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mwanakwerekwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. ALI SALIM KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, Zanzibar ni visiwa; uchumi wake ni wa huduma kwa ajili ya kusaidia Tanganyika ili iweze kuendelea. Mfano mzuri ni Singapore na Malaysia. Leo Malaysia inakua kiuchumi kwa haraka sana. Gruiz au Meli za kitalii, leo zinaondokea Singapore. Kwa hiyo, watalii wote wanataka kusafiri na meli za kitalii wanakwenda Singapore ndiyo waanze safari yao. Singapore ndiyo nchi ya kwanza iliyorusha Air Bus 380 kutoka Singapore kwenda Australia kwa mafanikio.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, kisiwa cha Penang kinachangia Malaysia kiuchumi kwa asilimia 60. Sasa wakati umefika wa kuiachia Zanzibar itekeleze uchumi wa huduma na baadaye kuisaidia Tanganyika kujitegemea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Account ya Pamoja ni lazima ifunguliwe na ianze kazi na mgawo wa mapato ya Muungano yawekwe wazi kila nchi ipate haki yake. Kuendelea kulipuuza jambo hili litaleta madhara makubwa katika Muungano.