Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumshukuru Mwenyezi Mungu na kiti chako na katika Wizara hii ya fedha naomba kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kodi ya Majengo (Property Tax), naomba sana irudishwe kwenye mamlaka ya mwanzo ambayo ni Halmashauri ili ziweze kukusanya ipasavyo. Tangu Serikali Kuu ichukue kodi hii ya majengo, Halmashauri zimekosa mapato na kodi hii haikusanywi tena. Serikali Kuu irudishe kodi hii Halmashauri kwa maendeleo ya nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti iliyopita, kuna fedha nyingi sana hazijapelekwa Halmashauri ili miradi mingi iende kama ilivyopangwa. Ucheleweshaji wa fedha za maendeleo kama ilivyopangwa ni kurudisha nyuma kasi ya maendeleo nchini. Naomba suala hili liangaliwe ipasavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kitendo cha Serikali kukopa ndani ya nchi na hasa mashirika ya Hifadhi za Jamii kama vile PSPF, LAPF, NSSF na nyingine, kunaleta ushindani na wananchi wa kawaida ambao huweka fedha zao huko kwa wakati maalum hivyo wanapotaka kujitoa huwekewa vigingi vingi kwa kuwa mifuko hii inakosa fedha. Pia Serikali inachukua muda mrefu sana kulipa madeni ya mifuko ya Hifadhi ya Jamii, hivyo mifuko hii hudumaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu kwa Serikali ni kwamba, kwa kuwa inakopesheka nje ya nchi, basi ifanye hivyo ili mzunguko wa fedha ndani ya nchi kupitia mifuko hii ya Hifadhi za Jamii na mabenki yetu ziendelee kutoa mikopo kwa wananchi wa kawaida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mabenki hutoa riba kubwa sana kwa wananchi wanaowakopesha. Wananchi hawa hushindwa kulipa mikopo hiyo na hatimaye kufilisiwa mali zao na vitu vyao vya ndani, hivyo kuwafanya kuwa maskini zaidi badala ya kuwainua kiuchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mbunge kila mwezi analipa fedha nyingi sana ya VAT na kodi ya mapato kupitia mshahara wake kila mwezi. Kitu cha ajabu, Wizara imeweka kodi nyingine kwenye kiinua mgongo kilicholipiwa kodi kabla hakijawekwa kutunzwa. Hali hii ni mbaya sana na siyo ya kuvumilika kuweka kodi juu ya kodi kwenye gratuity ya Wabunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Mashirika ya Umma yakaguliwe na CAG kwani matumizi yao, mfano kuna taasisi ya AICC iliyopo Arusha ambayo kazi yake kubwa ni kujenga Vituo vya Mikutano kwa mujibu wa sheria iliyoanzisha Sheria ya Taasisi hii ya AICC. Bahati mbaya badala ya kufanya kazi yao, wanatumia shilingi bilioni 3.5 kwa kukarabati ukumbi wa Simba na huku wakijenga nyumba kubwa yenye ghorofa sita kwa shilingi bilioni 1.8 tu. Haiwezekani ukarabati uzidi majengo makubwa. CAG akague Arusha AICC.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vema Wizara ikaweka katika bajeti zake shilingi milioni 50 za kila Kijiji ambazo ziliwekwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Kwa nini haziwekwi kwenye bajeti?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nashauri fedha za Mfuko wa Jimbo ziongezwe Mtwara Mjini, watu ni wengi, hazitoshi.