Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Upotevu wa Mapato ya Serikali: Waziri wa Fedha akichukua mapendekezo ya Kambi Rasmi ya Upinzani, naamini tutapiga hatua. Upotevu wa mapato ya Serikali upo wa kutosha katika vyanzo vyetu. Mfumo wa machine za EFD lengo lake ni zuri kabisa lakini bado kuna upotevu mkubwa japo machine hizo chache zilizopo pia baadhi ya wafanyabiashara huidanganya Serikali. Ni lini mtaongeza machine za EFD kila Wilaya nchini ziwepo za kutosha?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha inasimamia wafanyabiashara ambao wanafanya udanganyifu katika biashara zao? Unakuta mfanyabiashara tayari ana risiti za bidhaa ambazo zinakuwa na bei ya chini. Je, kupitia hili ni wafanyabiashara wangapi wanakwepa kuandika katika machine bei ya halali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukadiriaji wa kodi kwa wafanyabiashara ni kero na jambo hili linafanyika siyo kwa maslahi ya kuwasaidia wananchi, bali inawaumiza. Unawezaje kumlipisha kodi mfanyabiashara kabla ya biashara yake haijasimama? Je, hamwoni kuwa ule mkakati wa kupunguza umaskini kupitia kupungua makato makali ya kodi umefeli? Je, mpango wa kupunguza umaskini umefeli? Shilingi milioni 50 kila kijiji nadhani sasa ni muda muafaka wananchi wapewe fedha walizowaahidi katika Ilani ya CCM, watekeleze ili Watanzania wapate ahueni ya kiuchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna baadhi ya Taasisi za Fedha zimekuwa zinakwepa kodi na kumekuwa na ufinyu wa ufuatiliaji wa matumizi ya fedha katika Taasisi za Serikali; TBI, TANAPA, TANESCO, DAWASCO: Je, nani anafuatilia hili na kutoa taarifa kwamba matumizi ni sawa na kinachofanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo ni kwenye Taasisi zisizo za Serikali baadhi zimekuwa zikipunguza gharama, hivyo hazisemi ukweli na hivyo Serikali inashindwa kupata kodi ambazo ni halisi. Nini mkakati kuelekea Bajeti Kuu ili kusimamia taasisi hizi ili zilipe kodi halali na siyo kuiibia Serikali?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mifuko ya Jamii ya PSPF na NSSF ilikuwa na lengo zuri sana lakini katika kuwasaidia watumishi na wastaafu, changamoto ni moja kubwa katika mifuko hii ya jamii. Unakuta mtumishi amestaafu na anaishi mkoani na ni kijijini; ili apate mafao yake inampasa afuatilie mafao yake na inamlazimu kufika Makao Makuu na ukizingatia mifuko hii mingi iko mikoani. Kupitia bajeti hii, huu usumbufu utakwisha lini ili wananchi wapate huduma hizi kwa wakati, lakini pia wasisafiri umbali mrefu kufuata haki zao?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni kuhusu ubadhirifu wa mapato na matumizi katika Halmashauri (Mpanda). Kulikuwa na ununuzi wa gari la taka zaidi ya shilingi milioni 100, gari halipo;Kumekuwa na ununuzi wa mashine ya kusaga na kukoboa zaidi ya shilingi milioni 90, haipo; vile vile kuna matumizi mabaya ya ardhi nje ya makubaliano na mikataba (shamba la Benki NBC – Kakese (Mpanda).