Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali itoe msamaha kwa wafanyabiashara wote wa magari na pikipiki ambao waliuza vyombo hivyo vya moto lakini wanunuzi hawakubadilisha majina. Natoa ushauri huo kwa sababu mbili kuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja, Sheria ya Annual Motor Vehicle License haimlazimishi muuzaji kulazimisha mnunuzi kufanya mabadiliko ya umiliki. Sheria inampa mnunuzi siku saba mpaka thelathini za kufanya mabadiliko ya mmiliki (Transfer of Ownership), hivyo hata asipofanya mabadiliko ya umiliki hakuna namna ambavyo muuzaji anaweza kufahamu kwa haraka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali hiyo inafanya vyombo vingi vya moto kubaki na majina ya wauzaji kwenda muda mrefu, hivyo kusababisha wafanyabiashara wa magari na pikipiki kudaiwa madeni makubwa kupitia TIN zao. Mheshimiwa Waziri, akitaka kuwasaidia wafanyabiashara hao, ni jambo la busara kutoa msamaha wa madeni wanayodaiwa ili wasifilisiwe na TRA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, madeni hayo yamekuwa ya muda mrefu sana kutokana na Mamlaka ya TRA kutokumbusha wafanyabiashara wa magari na pikipiki kwamba wanabeba jukumu la kulipa Motor Vehicle License kwa vyombo ambavyo walikwishauza, lakini wanunuzi hawakubadilisha umiliki wake. Makampuni mengi yameshafanyiwa ukaguzi zaidi ya mara moja na wakalipa kodi ya Serikali. Nadhani siyo jambo la afya sana kuwabebesha wafanyabiashara hao mzigo huo mkubwa wa deni ambao siyo wa kwao moja kwa moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, msingi wa hoja yangu ni kwamba Serikali ni lazima ijenge mazingira rafiki kwa wafanyabiashara kwa vile ndiyo wateja wao. Hivyo, kutokana na ukweli kwamba kuna eneo ambalo mamlaka yenyewe ya TRA ilijisahau kuwakumbusha wafanyabiashara wajibu wao katika kufuatilia mabadiliko ya umiliki wa vyombo vya moto kwa wanunuzi, ni vema Mheshimiwa Waziri wa Fedha kwa mamlaka aliyonayo akaona busara ya kutoa msamaha wa madeni hayo makubwa wanayodaiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri aelewe kwamba madeni mengine yana miaka 10 au zaidi, hivyo ni vigumu sana kwa wafanyabiashara kuweza kulipa madeni hayo. Nashauri Mheshimiwa Waziri atoe msamaha wa hayo madeni ya Motor Vehicle Licence ili waanze ukurasa mpya na wafanyabiashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri mambo mawili muhimu katika suala la mashine za EFD. Kwanza, kuna maeneo mengi katika mikoa ya nchi hii ambayo hayajalazimishwa kutumia EFD machine. Mikoa kama ya Dodoma na mingineyo, biashara nyingi kubwa hazina EFD machine wakati Mkoa kama wa Kilimanjaro biashara ndogo tu zinatumia EFD machine. Naishauri Serikali ihakikishe EFDs machine zinatumika sawasawa na kwa haki nchi nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, EFDs machine zinaharibika mara kwa mara, hivyo kuwafanya wafanyabiashara wabebe mizigo mikubwa katika kuzirekebisha au kufanyia matengenezo; na gharama za matengenezo ni kubwa kuanzia kati ya Sh.50,000/= mpaka Sh.150,000/=.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.