Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuishauri Wizara hii na Waziri wake kuongeza uwazi na umahiri katika ukusanyaji wa kodi. Wananchi wetu hawakatai kulipa kodi ila iko mianya mingi ya ukwepaji wa ulipaji wa kodi sahihi. Wapo watumishi wa TRA wanapokisia kodi wanachukua asilimia kubwa na Serikali inapata kidogo. Serikali izibe mianya ya wizi wa kodi ili ipate mapato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bodi ya Maji ya KAVIWASU (Karatu Villages Water Supply) ni chombo cha wananchi (COWSO) kilichosajiliwa kwa sheria ya nchi Cap.375 kutoa huduma ya maji katika Mji wa Karatu na vijiji vinavyozunguka mji huo. KAVIWASU hawafanyi biashara bali wanatoa huduma ya maji kidogo wanachopata kutokana na mauzo ya maji kinatumika kuendeleza mradi katika maeneo ambayo mtandao wa maji haujafika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mshangao wa wengi wameshtuka TRA Karatu wameitaka KAVIWASU ilipe kodi yenye jumla ya Sh.200,000,000/= na zaidi la sivyo watakatiwa huduma na kukamatiwa mali. Mheshimiwa Waziri, DAWASCO, AWASA, DUWASA na bodi nyingine nyingi tena za daraja A hazilipi kodi hiyo iweje KAVIWASU tena chombo cha wananchi ambacho hata hakipati ruzuku yoyote kinalazimishwa kulipa kodi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwombe Mheshimiwa Waziri wa Wizara hii aangalie suala hili kwa kuwaelekeza TRA Karatu wasitishe madai yao hayo yanayokiuka sheria. Ikiwa sheria inawataka KAVIWASU kulipa kodi basi Waziri kwa mamlaka aliyonayo asamehe kodi hiyo ili wananchi wa Karatu waendelee kunufaika kwa huduma ya maji.