Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Fedha za Serikali ina impact gani kwa ukaguzi wa kila mwaka? Ubadhirifu unaoonekana kwenye ripoti ya CAG umefanyiwa kazi gani? Wabadhirifu kila mwaka wanapatikana lakini hakuna hatua zinazochukuliwa, hivyo ni business as usual.

Mheshimiwa Mwenyekiti, CAG kukagua fedha za Vyama vya Wafanyakazi kama vile CWT ni halali? Sheria iliyounda vyama hivyo imetaja Mkaguzi kuwa ni yule aliyetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Wafanyakazi nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokuwepo kwa Ofisi za TRA Kakonko ni jambo linaloleta usumbufu kwa wafanyabiashara kufuata huduma kilomita 300.