Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii. Nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri Dkt. Philipo Mpango, kwa hotuba yenye kuleta matumaini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa bajeti ya 2016/2017, taarifa inasema kati ya fedha za maendeleo kiasi cha shilingi bilioni 18.89 kilikuwa kimetumika ambacho ni asilimia mbili tu ya fedha iliyoidhinishwa. Ni dhahiri hiki ni kiwango kidogo sana katika utekelezaji wa bajeti hii. Nimwombe Mheshimiwa Dkt. Mpango utekelezaji wa bajeti ya mwaka ujao wa fedha 2017/2018 uwe wa uhalisia zaidi kuliko kwenye makaratasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi. Ofisi hii ndiyo jicho letu sisi Bunge katika kuisimamia Serikali. Cha kusikitisha, ofisi hii imekuwa ombaomba kwa Serikali. Hili linatia shaka na doa kwenye uhuru wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali kwa kuwa utendaji wake unatakiwa uwe huru bila ya kuingiliwa na yeyote. Uhuru huo unakuwa na mashaka kama iwapo Mkaguzi anaenda kwa mkaguliwa kuomba fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Mkaguzi Mkuu kwa mwaka 2016/2017, iliidhinishiwa kiasi cha shilingi bilioni 44.6 lakini mpaka kufikia mwezi Machi 2017, Ofisi ilikuwa imepokea shilingi bilioni 32.6 ikiwa ni sawa na asilimia 73.05 ya bajeti ya matumizi ya kawaida. Ni dhahiri Ofisi hii itapata shida kama tulivyoshuhudia imeshindwa kufanya kaguzi kwenye baadhi ya Balozi na ofisi nyingine nyeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru na naunga mkono hoja.