Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kwa kuunga mkono hoja. Mchango wangu ni kama ifuatavyo:-

(i) Wizara ya Fedha iangalie sera zake za kutoa fedha za miradi iliyopitishwa na Bunge, fedha zinachelewa na wakati mwingine hazitolewi kabisa na miradi ya maendeleo haikamiliki.

(ii) Wizara ya Fedha ilitazame kwa makini suala la road licence ni kero kwa wananchi. Naomba kodi hiyo iwekwe kwenye mafuta ambako kila mtumiaji chombo kinachotembea barabarani ataweza kulipa na itakusanywa kiurahisi sana.

(iii) Huduma kwa wastaafu, kwanza wanacheleweshwa kupewa stahili zao na nashauri maslahi yao yaongezeke kwani hali ya maisha inapanda na wanahitaji mlo mzuri kuweza kukabiliana na hali zao.

(iv) Mgawanyo wa fedha za ruzuku uangalie maeneo yaliyo nyuma zaidi ili kuyavuta mkono kwa makusudi ili wasogee maana kuna changamoto nyingi zaidi.

(v) Mikopo ya fedha ielekezwe zaidi kwenye kukuza kilimo kama tegemeo la wananchi wengi nchini na mchangiaji mkubwa wa pato la Taifa.

(vi) Walipa kodi ni wadau muhimu wa maendeleo, naomba pawepo staha zaidi katika kufuatilia kodi na wananchi waelimishwe zaidi kwa makala na matangazo mbalimbali juu ya umuhimu wa kulipa kodi kwa hiari.

(vii) Benki ya Kilimo iwezeshwe, kilimo kitakua kama mitaji itaelekezwa huko.

(viii) Sheria itungwe kuwasaidia watumishi ambao hujikuta wamelazimika kukopa fedha kwa wakopeshaji wasio rasmi wanaotoza riba kubwa inayofikia 30% kwa mwezi yaani ukikopa Sh.10,000,000/= tarehe 1 - 31 Desemba wanalipa Sh.13,000,000/= ongezeko la Sh.3,000,000/= na akichelewa inalipa pamoja na Interest kwa Sh.3,000,000 ni Sh.300,000, watu wanaibiwa sana.