Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Emmanuel Papian John

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. EMMANUEL P. JOHN: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwanza nimpongeze Waziri kwa hotuba yake aliyoitoa ambayo inaweza kutusogeza na ikatufikisha mahali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza nataka kusema TRA imefanya kazi nzuri, sasa hivi tunaona kuna mahusiano mazuri kuliko nyuma ambako kulikuwa na maneno mengi, vurugu na wafanyabiashara, mvurugano na kukimbizana, sasa kunaonekana kuna lugha ambayo ni mahusiano mazuri yanayofanya watu kulipa kodi kwa usahihi lakini pia kwa mahusiano mazuri ya lugha na wanafanya vizuri zaidi kuliko kipindi cha nyuma ambacho kulikuwa na mivutano mikali baina ya wafanyabiashara na watoza kodi wetu. Hilo ni jambo la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, kuna hii Benki ya Kilimo, benki hii tunadhani sasa ndiyo wakati wake, Awamu ya Nne imejitahidi imeanzisha benki hii, lakini tunaomba Serikali basi ione namna gani ya kuiongezea mtaji. Kuna fedha za nje, Nchi kama za China, leo China tunasema ni marafiki zetu wakubwa sana wa kihistoria kwa nchi yetu, kwa nini benki za China Serikali isikope kwa riba nafuu ikaletea pesa Benki yetu ya Maendeleo ya Kilimo ikaipa mtaji wa kutosha ikaisimamia hii benki ikaenda kwa wananchi wetu ambao ndio asilimia 80 ya Watanzania ambao wanajihusisha na shughuli za kutafuta maisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuimarisha benki hii na kuipa mtaji unasaidia watu wengi kuwa kwenye wigo mpana wa kufanya kazi na Watanzania wengi watakapofanya kazi Serikali itaweza kukusanya kodi ya kutosha. Niishauri Serikali ilitazame hili, ilifanyie kazi na ihakikishe kwamba hii benki inapata mtaji kwa kipindi kisicho kirefu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna hizi benki za biashara, hizi benki sasa hivi zina hali ngumu, zimekopesha watu, watu wameshindwa kurejesha mikopo kwa sababu ya kipindi kigumu, uwezo wa kushindwa kulipa kwa watu umeongezeka, lakini benki hizi zilikuwa na nia njema kwa sababu zimekopesha wakulima ambao hata mahali ambapo kilimo kimeshindikana kwa sababu ya mvua zikajaribu ku-risk zikakopesha hao watu, watu wame-default, sasa benki na zenyewe zinakwenda kuanguka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, yawezekana hizi benki za biashara; CRDB, NMB, zina defaulters, mikopo mingi inachechemea. Tunaomba basi Mheshimiwa Waziri na Gavana watazame hili waone huruma mahali ambapo wamekosea, basi warudishe nyuma kidogo, wasamehe kwa sababu wanaoumia ni wengi Watanzania wetu wanaolipa kodi, basi tuone ni namna gani wanaweza kusonga mbele. Vinginevyo, wakiendelea kukandamiza sana kwa hali ilivyo sasa tutapoteza watu wengi kibiashara, tutapoteza kodi kubwa sana lakini pia na nchi itayumba economically. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali ione huruma hivi vyombo vyetu vya fedha mahali vilipokosea basi wawasamehe, wakae chini mezani wawape guidelines za kufanyia kazi, wawape muda, waone ni namna gani wanaweza kusonga mbele, lakini wawalinde kwa sababu na wao walikuwa ni sehemu ya kuchangia uchumi kwenye nchi yetu. Maana hizi defaulting zote zinazoenda ku-appear ni kwamba bado Serikali na yenyewe inaendelea kupoteza mapato. Sasa ili twende pamoja, kwa sababu tunawahitaji, Serikali tunahitaji isipoteze, hizi institutions tunahitaji zisife wala kutetereka kwa sababu nchi inaweza ku-shake. Sasa ili tufikie hapo, basi tunaomba Serikali ishushe mkono, itoe huruma, itoe maelekezo, iangalie ni namna gani hivi vyombo vinaweza kuendelea kufanya kazi bila mvutano wowote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Benki ya TIB ambayo ni benki ya Serikali. Tunaomba Serikali iione na iipe mtaji kama nchi nyingine zinavyokuwa na benki za Serikali ambazo zinapewa fedha na kuzisimamia ili benki hizo zisife.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna hili suala la milioni 50 kila kijiji. Kwenye Wilaya yangu tumekaa tukafikiri tukajipangia, tukasema ngoja tuisaidie Serikali. Mimi namsaidia Mheshimiwa Waziri. Wilaya ya Kiteto tuna vijiji 63, hivi vijiji ukitaka kuniletea milioni 50 kila kijiji ataniletea 3,150,000,000, mimi hizi zote asiniletee, sizihitaji kwa sababu Tanzania ni kubwa, Kiteto ni Wilaya katika Wilaya mia moja na kitu za Tanzania, namwomba milioni 500 tu. Hii naomba ifanyike kwa nchi iwe ni pilot study, watu waje wajifunze, waone ni namna gani tutakavyotumia hizi pesa zikaenda kuzunguka kwa watu wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumejipangia sisi tuna mpango wa VICOBA Wilaya nzima. Wilaya ya Kiteto inaenda kuwa Wilaya ya kwanza kwenye mfumo wa VICOBA ambapo pesa ya wale wanachama haipotei na mfumo ule haupotezi pesa, watu wanajilinda wenyewe. Akinipa milioni 500 mwezi wa Nane ikaanza kuzunguka kwenye VICOBA katika vijiji kumi tu, nifikapo mwakani mwezi wa Nane nitakuwa nimeshakwenda zaidi ya vijiji 40. Kwa maana ya kwamba zile zitakazokusanywa tunazielekeza kwenye vijiji vingine, kwa maana hiyo pesa itakayozunguka pale tutakapofika 2020 nikisimama kunadi Ilani ya CCM tuliyoiahidi mimi na Mheshimiwa Waziri huko kwa wananchi, nitakuwa nimesha- cover vijiji vyangu vyote 63 kwa hiyo pesa ya milioni 500.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri atakapokuja naomba anipige tafu anipe hiyo ahadi ya milioni 500, anipe mimi na Wilaya nyingine Tanzania zitakwenda kujifunza pale ili tuweze kurudisha pesa. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Waziri mbele yake, hizi pesa akinipa ifikapo 2020 namrudishia 500 ya kwake na wananchi wangu watakuwa wameshapata kazi na Serikali itakusanya kodi kubwa maana hawa wananchi hizi milioni 500 wanapokwenda kufanya kazi, watafanya kaziā€¦..... (Makofi/ Kicheko)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.