Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa fursa. Kwanza nitumie fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutufikisha wote hai na salama, tuliopata bahati ya kufika kwenye Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Mwenyezi Mungu atujalie tuweze kufunga kwa amani na utulivu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze hotuba yangu na mchango wangu kwa maneno yafuatayo:-

Jukumu la msingi la Wizara ya Fedha kama Wizara ni administrator anayesimamia utekelezaji wa kitu kinachoitwa Fiscal Policy. Fiscal Policy ndiyo instrument inayotumika na Serikali kukusanya fedha na inayo-guide Serikali sehemu ya kutumia fedha hizo kwa lengo moja tu la msingi, kusaidia na kuchochea ukuaji wa uchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimefanya tathmini yangu kwa kina. Leo tuna mwaka mmoja, nimekaa najiuliza maswali na naongea kwa polepole sana, nini dhamira ya wataalam walioko katika Wizara ya Fedha?

Mheshimiwa Mwenyekiti, usimamiaji na utekelezaji wa jambo hili una vehicle mbili tu, moja yenye dhamira ya kupambana na mfumuko wa bei. Hapo ndipo Serikali itaweka kodi ili kupunguza purchasing power ya watu, lakini katika kuchochea uchumi nyingine ni Serikali kutumia Sera yake ya Kodi ili kupunguza sehemu mbalimbali wanazotoza kodi na kukuza uchumi na hasa pale ambapo biashara zinapokuwa chini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitamtolea mfano mlipa kodi mmoja mkubwa anaitwa TBL. TBL baada ya mabadiliko ya kodi ya mwaka jana, kodi anayolipa kwa Mwaka huu wa Fedha wa 2016/2017 tunaomaliza, imeshuka kwa bilioni 50. Huyu ni TBL kwa nini, kwa sababu ya imposition of Excise Duty.

Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa za Wizara ya Fedha zinaonesha kushuka kwa makusanyo ya kodi ya PAYE, taarifa ya makusanyo ya fedha ya Wizara ya Fedha inaonesha kushuka kwa VAT on import goods. Taarifa ya TPA inaonesha kushuka kwa mapato kwa asilimia 13 ya bandari yetu, kwa nini? Kwa sababu ya imposition ya VAT on transit goods. Najiuliza swali, wataalam wa Wizara ya Fedha wanafikiri nini? Mwalimu wangu wa uchumi yumo humu ndani, I am not an economist, lakini nimesoma basics, najiuliza wao wanatoa wapi hizi thinking wanazo-impose?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa taarifa za Wizara ya Fedha biashara 7,700 zimefungwa nchi hii, ajira zimepotea! Najiuliza maswali, what is the bottom line? Bottom line ni kukuza uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wataalam wa Wizara ya Fedha wameweka kodi maeneo mbalimbali kwa mwaka wa fedha na ukisiliza business community inalalamika juu ya imposition ya kodi nyingi zinazowekwa na Serikali na huoni dhamira ya Serikali kupunguza kodi hizi, huoni kabisa. A large tax payer ambaye ananunua mazao ya kilimo kutoka kwa Watanzania kama TBL, anaenda Serikalini anapeleka proposal ya kuwaambia jamani, mnavyoweka kodi hii mnapoteza fedha hizi na Serikali at the end of the day inapoteza kiwango hiki cha fedha! Alisema Mheshimiwa Serukamba hapa ni lazima Serikali ijue katika kila biashara ya kila Mtanzania Serikali ni share holder kwa asilimia 30, kwa sababu inachukua siku ya mwisho corporate tax. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nitoe mifano michache, nimeitaja; Domestic VAT imeshuka, VAT on import imeshuka, domestic ya excise imeshuka, PAYE imeshuka, withholding tax imeshuka, corporate tax imeshuka! Where are they going to collect? Wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba kaka yangu Mheshimiwa Mpango nilisema mwaka jana na narudia leo ndani ya Bunge hili. Naheshimu sana his academic back ground, either kuna mambo mawili, kuna slow move ndani ya Wizara ya Fedha juu ya wataalam kuishauri Serikali sawasawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa za Wizara ya Fedha zinaonesha zimefunguliwa biashara mpya laki mbili, unajiuliza swali biashara elfu saba zilizofungwa impact yake kwenye kodi zimeonekana. Hizi laki mbili zilizofunguliwa kwenye uchumi hazionekani, nashindwa kuelewa wapi tunataka kwenda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niiombe Serikali kwa heshima kabisa, kuna njia mbili za kutengeneza bajeti, anao large tax payer wake Mheshimiwa Waziri, awaite awaambie kutoka wewe TBL anataka corporate tax ya this amount mwaka huu wa fedha amfanyie nini kama Serikali, atamwambia ili a-grow productivity yake atasema nipe one, two, three, four, because the bottom line una-tap mwisho. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo vinywaji baridi wiki iliyopita CocaCola Kwanza imepunguza wafanyakazi 130. Jamani ninyi wataalam mliokaa huko nataka niwaambie jambo moja na niseme kwa kuwa mimi ni Mbunge wa Chama cha Mapinduzi, sitavumilia kutoka moyoni kuona technical mistake ambazo haziitaji PhD wala u-professor. We will not allow this! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, dhamira ya Rais iko very clear, ku-grow uchumi wa nchi hii, kujenga viwanda, ku- create ajira, hatuwezi ku-attain namna hii. Nataka niwape mfano, ukisoma taarifa ya Port Authority ya Kenya mwaka 2014/2015 asilimia 1.4 ya mizigo ya Tanzania ilipita pale. Mwaka 2016/2017 asilimia 2.7 ya mizigo ya Tanzania imepita Mombasa, ina-grow, maana yake wafanyabiashara wanahama, wanaenda kupitishia mizigo yao kwingine, why! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, principal ziko wazi, Serikali inakusanya kodi, haiwezi kukusanya kodi kwa watu maskini, haiwezi kukusanya kodi, nataka niwape mfano, Bunge lililopita Waziri wa Fedha alisema humu ndani Dkt. Mpango tutagawa EFD machines kwa wafanyabiashara Serikali haijagawa to-date, unajua kinachoendelea site, wafanyabiashara wameandikiwa barua waikopeshe Serikali hela…. (Makofi)

(Hapa muda wa kengele ililia kuashiria muda wa mzungumzaji kuisha)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.