Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nitazungumzia mambo mawili tu, la kwanza ni suala la investor confidence ambalo jana Mheshimiwa Lema alilizungumzia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna tatizo kubwa Tanzania la investor confidence kwa sababu ya kauli nyingi ambazo zinatolewa na Serikali, matendo mengi ambayo yanatendwa na Serikali ambayo katika nchi nyingine athari yake inaonekana moja kwa moja, lakini hapa kwa kuwa athari yake hatuioni moja kwa moja kwa sababu stock exchange yetu haifanyi kazi kama vile ambavyo ingetakiwa tunadharau.

Kwa hiyo, napenda niishauri Serikali na Mheshimiwa Waziri kwamba wakae na Serikali na wajaribu kutengeneza namna ambayo shock ya kibiashara, shock ya uwekezaji inaweza kupata nafasi kidogo kwa kuzuia kauli au matendo ambayo yanapoteza investor confidence, hilo moja. (Makofi)

Mheshimiwa MNwenyekiti, lakini lingine nitalizungumzia kwa undani kidogo ni suala la Mfuko wa Pamoja wa Fedha ambapo leo hii halitochacha mpaka nipate majibu, kwa sababu hili lipo Kikatiba, miaka almost 40 hivi sasa halijafanyiwa kazi, kwa nini linashindwa kufanyiwa kazi? Kama vile ambavyo Mahakama ya Katiba ambayo nchi hii imesema iundwe mpaka leo haijaundwa badala yake tunatatua matatizo yetu ya Katiba kwa kupitia kwa Tume ya Pamoja au whatever. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mfuko huu wa Pamoja wa Fedha tokea kuasisiwa hivi sasa tumeshapoteza mamilioni katika kuiendesha na kujaribu kufanya kazi, mabilioni yote ambayo yametumika yamekwenda bure.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mfuko wa Pamoja ni white elephant haujaundwa, haujatumika na kwa hivyo bado matatizo ambayo yameundiwa kwayo yako pale pale kwamba Zanzibar inalaumika haichangii katika Muungano, lakini Zanzibar inasema itachangiaje katika Muungano wakati haijui matumizi yapo vipi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, matumizi ya Bara hayawezi kuwa sawasawa na matumizi ya Zanzibar kwa sababu Zanzibar ni ndogo kama inataka askari, inataka askari kidogo kuliko Tanzania Bara, kama inataka kulinda mipaka Tanzania Bara inapakana na nchi tisa wakati Zanzibar inapakana na Kenya peke yake. Kwa hiyo, kuna mambo mengi ambayo hatuwezi kwenda sawasawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hiyo haitoshi kulikuwa na ripoti nyingi zimefanywa, moja ni ripoti ya black, nyingine ni ripoti ambayo imetengenezwa na Coopers and Lybrand, ikionesha namna gani kunaweza kuwa na formula kwa sababu inaonekana formula ya 4.5 ambayo tunagawana hivi sasa imepitwa na wakati. Kwa hivyo, mfuko huo siyo tu utaonesha Zanzibar ichangie kiasi gani na Tanzania Bara ichangie kiasi gani, kuondoa lawama kwamba Zanzibar inabebwa au Zanzibar inapata bure kila kitu, pia utaonesha namna ambavyo fedha za Muungano, zilizo halali za Muungano hazitumiki kwa Serikali ya Tanganyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tusikatae ukweli, hapa tuna mamlaka tatu, tuna mamlaka ya Zanzibar, tuna mamlaka ya Muungano na tuna mamlaka ya Tanganyika, Tanganyika ipo, haijawahi kuondoka, kwa sababu mfanyakazi wa kilimo wa Tandahimba ni mfanyakazi wa Tanganyika siyo mfanyakazi wa Muungano. Mfanyakazi wa Mbeya, Nachingwea wa Wizara ya Afya ni mfanyakazi wa Tanganyika siyo mfanyakazi wa Muungano, tunajidanganya siku zote. Kwa hiyo, mamlaka ya Tanganyika ipo, imekuwa inatumia fedha za Muungano kwa ajili ya Tanganyika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ukiwepo Mfuko wa Pamoja na hizi ripoti zimeonesha ni kiasi gani fedha za Muungano zinakusanywa na hizo fedha za Muungano zinatosha kuendesha Mamlaka Tatu, Mamlaka ya Tanganyika, Mamlaka ya Zanzibar na Mamlaka ya Muungano. Kwa hiyo, mpaka leo mfuko hauundwi kwa sababu watu walioko Tanganyika wana hofu ya ku-expose hiyo, kwamba kuna fedha za Muungano zinatumika kwa Tanganyika, wana hofu ya kuonesha kwamba Zanzibar inaweza kuchangia iwapo kungekuwa na usawa kwa maana ya kwamba Zanzibar itashirikiana kitu gani na Muungano itashirikiana kitu gani. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri leo hii natangaza kabisa, najua mtashinda kwa wingi…(Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)