Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Catherine Nyakao Ruge

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. CATHERINE N. RUGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia katika Bajeti Kuu ya mwaka 2017/2018.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchukua nafasi hii kuipongeza Kambi Rasmi ya Upinzani kwa hotuba nzuri. Niiombe Serikali iweze kuchukua muda kusoma hotuba hii na kuangalia mambo mazuri ambayo tumeishauri ili waweze kuifanyia kazi kwa mustakabali wa Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hotuba hii nitajikita kwenye mambo makuu matano. Bajeti hii imekuja wakati kama Taifa tukiwa na changamoto nyingi, mojawapo ikiwa ni ukame ambao umesababisha njaa katika maeneo mbalimbali nchini lakini pia kuyumba na kufungwa kwa biashara nyingi ambapo zimeathiri uchumi wa nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie kufungwa na kuyumba kwa biashara nyingi nchini mwaka 2016/2017. Wakati Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango akiwasilisha hotuba ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2016/2017 alikiri katika kipindi cha mwezi Agosti na Oktoba, 2016 biashara 1,872 zilifungwa katika Mikoa miwili ya Dar es Salaam na Arusha. Kama kwa kipindi cha miezi mitatu, biashara zaidi ya 1,000 zinaweza kufungwa basi ndani ya mwaka mzima ni zaidi ya biashara 7,488 zinaweza kufungwa kwa mikoa miwili tu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii maana yake ni nini? Tunakwenda kupoteza ajira zaidi ya 15,000 kwa maana ya wastani wa wafanyakazi wawili katika kila biashara. Hii haiathiri wafanyakazi tu, lakini pia familia zao ambazo zinawategemea ukizingatia utamaduni wetu wa nchi yetu tunaishi kwa kutegemeana (extended families). (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango alikuwa anatoa mifano ya jinsi gani kumekuwa na mdororo wa uchumi kwa nchi mbalimbali miaka mingi iliyopita. Nadhani ni vizuri Mheshimiwa Waziri ungejikita katika kuangalia sababu zilizofanya kufungwa kwa biashara hizi na suluhisho ili kuzuia na sisi tusije tukapata mdororo wa uchumi kama nchi ambazo ulizitolea mfano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wafanyabiashara wengi wamekuwa wakilalamika kwamba kuyumba kwa biashara zao kumetokana na jinsi ambavyo TRA wamekuwa wakiwakadiria mapato. Niishauri Serikali iweze kuangalia ni jinsi gani inaweza kujenga mazingira rafiki ya wafanyabiashara kulipa kodi na kufanya biashara zao na isiwe chanzo cha wafanyabiashara kufunga biashara zao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili ambalo napenda kuchangia ni import and export. Uchumi wa nchi yoyote hauwezi kukua kama mauzo ya biashara tunayozalisha nchini yanapungua siku hadi siku. Kwa mujibu wa Jarida la Uchumi la Benki Kuu ya Tanzania Machi, 2017, linaonyesha kwamba uwezo wetu wa kuuza bidhaa tunazozalisha nchini kwenda masoko ya nje umepungua kwa asilimia 34.6 ukilinganisha na kipindi kama hicho Machi, 2016. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ni jambo ambalo inabidi tulitazame kwa jicho la tatu na inabidi Serikali ijiulize maswali yafuatayo. Je, ni kwa sababu bidhaa zetu hazina ubora wa kuweza kushindana na bidhaa za mataifa mengine au ni kwa sababu bidhaa tulizokuwa tunaziuza nje kwa mwaka 2016 na miaka iliyopita zimekosa masoko na hivyo basi inabidi tufikirie bidhaa mbadala ili tuweze kuendelea kuuza nje na kuongeza pato la Taifa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mauzo ya nje yakiwa yameshuka kwa kiwango hicho nilichokitaja lakini pia manunuzi yamepanda kwa asilimia 33.5 kwa mwaka 2016/2017. Hii inanipa wasiwasi kwa kuwa tunaelekea Tanzania ya Viwanda kwamba tunanua zaidi kuliko tunavyouza na hivyo kunakuwa na unfavorable balance of payments. Ili tuweze kuvilinda viwanda vyetu, inabidi tu- promote viwanda vya ndani lakini pia tuweze kuzalisha zaidi na kukidhi masoko ya ndani pia kuweza kuuza zaidi nje ya nchi ili tuweze kuongeza pesa za kigeni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la tatu ambalo napenda kuzungumzia ni ajira. Suala hili limeendelea kuwa changamoto especial kwenye kipindi hiki cha Awamu ya Tano ambapo tumekuwa na wahitimu wengi wakiwa wanatoka vyuoni zaidi ya 10,000 kila mwaka, lakini Serikali hii imesitisha ajira pia kuna mazingira magumu ya kufanya biashara na hivyo kampuni nyingi zimepunguza wafanyakazi. Hii imekuwa ni changamoto especial kwa vijana, wamekuwa wakirandaranda mitaani na degree zao na vyeti vyao na kukosa matumaini ya kesho yao na kujiona kwamba wamepoteza muda kusoma degree zao za miaka mitatu mpaka mitano. Mheshimiwa Waziri nikuombe wakati unakuja kuhitimisha hotuba yako uwaeleze vijana wa Kitanzania katika bajeti ya mwaka 2017/2018 unakwenda kuajiri vijana wangapi katika Taifa hili? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, ukisoma kitabu cha bajeti Serikali inaonyesha imelipa madeni ya shilingi bilioni 67.6. Naomba niipongeze Serikali kwa kulipa madeni hayo. Tatizo langu nataka kujua definition ya watumishi katika Taifa hili kwa sababu madeni haya yote ya shilingi bilioni 67.6 wamelipwa walimu. Nikuombe Mheshimiwa Waziri, kuna watumishi wengine ambao siyo walimu wanadai arrears zao za mishahara, stahiki zao za kupanda vyeo, stahiki zao za uhamisho ili uweze kuwalipa kwa sababu kwenye kitabu chako hujaonesha kama kuna ongezeko lolote la mshahara. Hata ile increment ambayo ni kwa mujibu wa sheria wafanyakazi hawa hawajongezewa mishahara yao, namaanisha statutory annual increment kwa wafanyakazi ambayo ipo kwa mujibu wa Labor Laws. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee suala la PAYE kwa maana ya Pay As You Earn. Wafanyakazi wamekuwa wakilipa kodi kwa asilimia 100 kwa sababu hawana loopholes za kukwepa hii kodi ukilinganisha na wafanyabiashara. Kama kuna watu wanalipa kodi genuine katika Taifa hili basi ni wafanyakazi, lakini wafanyakazi wanakatwa kodi kwenye gross pay na siyo net pay. Tukumbuke wafanyakazi pia wana matumizi au expenses mfano na wao pia wanalipa kodi, wanalipa nauli, wanakula chakula pamoja na matumizi mengine katika kutimiza wajibu wao wa kwenda kazini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfanyakazi ambaye yupo kwenye band ya milioni moja na zaidi analipa asilimia 25 au zaidi ya PAYE. Ukiangalia kwa makampuni au corporate companies ambao wanalipa 30 percent kwa net profit kwa maana kuna allowable expenses nyingi ambazo wanakuwa hawazilipii kodi. Kwa hiyo, tunaona kuna burden kubwa sana kwa mfanyakazi wa Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuombe Mheshimiwa Waziri, kama Serikali haiwezi kupunguza Pay As You Earn basi PAYE ikatwe kwa net pay baada ya kutoa housing allowance, food allowance, fuel allowance… (Makofi/Vigelegele)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)