Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi hii ya kuchangia bajeti ya Serikali. Kama walivyosema wenzangu bajeti ya mwaka huu kwa kweli ni bajeti ya kimapinduzi, (transformation) imeelekeza nguvu zote kuwasaidia wanyonge wakiwemo wakulima ambao ni wengi katika Tanzania yetu hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika bajeti hii kodi za mitaji zimesamehewa (Capital goods budget), kodi imeondolewa ya kuondoa kodi ya thamani ya usafirishaji (ancillary transport services), kodi ya maeneo ya ufugaji nayo imeondolewa na kuwapa unafuu sana wakulima wetu huko vijijini.

Mheshimiwa Spika, vilevile kufutwa kwa road licence kwa kweli hii kodi ilikuwa ni kero, ilikuwa haitusaidii kabisa. Nina imani kuwa hii kodi mapato yake ukilinganisha na gharama zilizokuwa zinatumika zilikuwa haziendani sawa sawa. Nashukuru baada ya kuisoma vizuri bajeti hii kuwa ongezeko la Sh.40/= linaongezwa kwenye pato, hii sio mbadala wa road license.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimeilewa vizuri sana kwa sababu hata ile notion ya kwamba hii inakwenda kuwaumiza wakulima kwa sababu wanalipia road license. Road license imefutwa kama inasomeka vizuri kwenye bajeti hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala la ujenzi wa reli kwa standard gauge, hayo ni mapinduzi makubwa sana ya kiuchumi. Vilevile mpango wa kujenga reli kutoka Tanga mpaka Musoma, hayo ni mapinduzi makubwa sana katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, bomba la mafuta toka Uganda kwenda Tanga kwa kweli hayo ni mapinduzi makubwa sana. Pamoja na hayo tusisahau vilevile kwamba hizi investments

tulizokuwa nazo kama TAZARA, bomba la mafuta kwenda Zambia nazo ziboreshwe kuhakikisha zinafufuliwa na zinafanya kazi inavyotakiwa.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, nalisema hilo kwa makusudi kwa sababu punguzo la mbolea litawapa nafuu sana wakulima, lakini tusipoboresha usafirishaji hilo punguzo wakulima hawataliona, kwa sababu kodi nyingi zimeondolewa katika mbolea. Hata hivyo, ukiangalia value chain ya mbolea kutoka huko tunakoagiza nje asilimia 53 ni CIF ambayo ni gharama ya kununua mpaka bandarini lakini asilimia 47 ni ya kumplekekea mkulima, bila kuipunguza hiyo kwa kweli wakulima wetu hawataona huo unafuu. Kwa hiyo naiomba sana Serikali ijaribu kuelekeza ni namna gani tuondoe urasimu pale bandarini, ni namna gani tuboreshe TAZARA, reli ya kati ili mbolea zote zisafirishwe kwa reli na hiyo italeta ushindani mzuri kwa mazao yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nchi yetu ni ya kilimo kwa asilimia kubwa sana, Mbeya tunalima pareto. Pareto ni zao ambalo linatumika kutengeneza sumu, madawa kwa ajili ya kuulia wadudu, inatokana na maua, halihitaji mbolea. Hili zao kwa sasa hivi lina soko kubwa mno, tunazalisha tani 2000 lakini mahitaji sasa hivi ni karibu tani 10,000. Kwa kuangalia hili zao linaweza kutuletea foreign exchange kama tutapeleka nguvu huko, nguvu tunayoihitaji ni kidogo hatuhitaji kuongeza bajeti, tunachotakiwa kuongeza hapo ni usimamizi wa kumsaidia mkulima kwenye masuala ya masoko.

Mheshimiwa Spika, leo hii wakulima wanalima pareto lakini soko limekuwa dominated na mtu mmoja, wengine wanapokuja wananyimwa nafasi ya kwenda kununua. Mwaka huu Bodi ya Pareto hata ule mkutano wa wadau wameahirisha, hatujui mkutano utakuwa lini kwa sababu ule ndio tulikuwa tunaangalia changamoto nyingi za hili zao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, zao letu lingine la kahawa halifanyi vizuri ukilinganisha bei za Tanzania na bei za majirani zetu Kenya. Wote tunalima kahawa aina ya Arabica, Kenya

inalimwa huku kwa wenzetu Kilimanjaro na Mbeya lakini kwa Nairobi coffee exchange bei ya sasa hivi ni dola 300 kwa kilo 50, kwa sisi ni chini ya dola 150. Sasa hii yote hii inatokana na nini, kwa nini kahawa ile ile na wanunuzi ni wale wale, kahawa ya kwetu Tanzania bei iwe chini? Inanikumbusha kwamba matatizo tuliyonayo kwenye madini ni yale yale matatizo waliyonayo wakulima wa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali iangalie ni namna gani tutawasaidia wakulima ili tuwe na masoko ya uhakika ya kipindi chote ikiwemo masoko ya kahawa, pareto, viazi, ndizi, ndizi zetu kule Mbeya zinabebwa na magari kupelekwa nchi jirani for export na hata siku moja hutaona kwenye kumbukumbu zetu kuwa tuna export ndizi. Sasa yote haya tukiboresha masoko yetu nafikiri nchi yetu itapata forex nyingi kutokana na kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa tozo za mazao ya kilimo. Nashukuru sana kwa kweli kuna unafuu wa wakulima lakini je, hili punguzo la tozo tutazisaidia vipi Halmashauri kwa vile zilikuwa zimejumuishwa kwenye bajeti za Halmashauri. Kwa Halmashauri ya Mbeya mapato tunategemea zaidi kwenye kilimo na tunapata karibu nusu bilioni na hii nusu bilioni yote kama nilivyokuwa naiangalia leo kwenye bajeti ni kwamba hiyo imeenda na hiyo ni karibu asilimia 50 ya bajeti ya mapato ya ndani ya Halmashauri.

Mheshimiwa Spika, tusipoyakusanya hayo mapato Halmashauri itawajibika na kuadhibiwa. Sasa labda ningeomba Mheshimiwa Waziri atakapokuja kujumuisha hayo mapato ambayo yameondolewa kwenye Halmashauri yatafidiwa vipi ili Halmashauri zetu ziendelee kufanya kazi kama kawaida. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kilimo bila miundombinu mizuri kwa kweli hatuwezi kufanikiwa, naomba sana kuboresha miundombinu vijijini ikiwemo umaliziaji wa ujenzi wa kiwanja cha Songwe, ambacho mpaka leo hakina taa za kuongozea ndege na hakuna wigo kwa usalama wa uwanja...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, ahsante na naunga mkono hoja.