Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza naomba niunge mkono maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kuhusu hoja ya bajeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo ambalo napenda kulizungumza hapa ni ambalo limekuwa likinadiwa sana katika bajeti hii kwamba hii bajeti ni ya kihistoria. Na mimi nimepita kwenye hii bajeti kwa kadri ilivyowezekana nikitazama hiyo historia ya hii bajeti, bahati mbaya sijaweza kuona, labda Mheshimiwa Waziri atanishawishi wakati ana- wind up kunionesha jinsi hii bajeti ilivyo ya kihistoria kwa sababu mimi nilivyoiona hii bajeti ni tegemezi kama zilivyo bajeti nyingine zote ambazo zimepita katika nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti inategemea kukusanya shilingi trilioni 19.9 mapato ya ndani, takribani na inategemea kutumia kutumia shilingi trilioni 19.7 mapato ya ndani kwa matumizi ya kawaida. Sasa najaribu kujiuliza tofauti yake na bajeti zingine ni nini kwa sababu bado asilimia 38 ya bajeti hii inategemea mikopo ama misaada kutika nje. Kwa hiyo, nilikuwa najaribu kutafuta huo uhistoria na mimi siuoni! Naomba sana kushawishiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika shilingi trilioni 11 za maendeleo pesa yenye uhakika wa kupatikana katika bajeti hii ni mikopo ya ndani ya shilingi trilioni 6.1 mikopo ya shilingi trilioni 5.56 tunategemea kutoka wa wahisani au washirika wa maendeleo ama mikopo kutoka nje. Katika kitabu hiki cha Mheshimiwa Waziri anakiri kwamba, mahusiano yetu na washirika wa maendeleo sio mazuri na ndio maana imeundwa timu ya pamoja ya kutoa ushirikiano wa namna gani tume huru inaweza ikasaidia namna ya kujenga mahusiano na washirika wetu wa maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwa nini mahusiano yetu sio mazuri wakati yalikuwa mazuri wakati wa Mheshimiwa Mkapa mpaka tukafutiwa madeni? Ni kwa nini mahusiano yetu sio mazuri wakati wa Mheshimiwa Kikwete mpaka tulikuwa na International PR? Kwa nini kwa sasa hivi mahusiano yasiwe mazuri? Ni lazima Serikali ingetakiwa ijiangalie mmekosea wapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo mlilokosea ni la wazi kabisa, wanazungumza kila siku. Mmekiuka misingi ya demokrasia katika nchi hii, mmekiuka misingi ya utawala bora, mmezuia uhuru wa vyombo vya habari, mmetengeneza sheria mbovu za mitandao, ni vitu vya wazi. Sasa mnatafuta kitu gani cha kuzungumza na hao mnaowaita mabeberu ambao angalau wana-good governance kuliko sisi Watanzania ambao sio mabeberu? Kwa hiyo, nilikuwa natamani nipate sababu ya kwa nini bajeti hii inaitwa bajeti ya kihistoria, ambayo ni bajeti tegemezi kama zilivyo bajeti nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo la pili, bajeti hii haina uhalisia, sio realistic. Kwa sababu, najaribu kuangalia ni namna gani tutapata shilingi trilioni 17.1 kwenye mapato ya ndani wakati tunakwenda kukopa sisi, kama Serikali, kwenye benki za ndani zaidi ya shilingi trilioni sita. Kwa misingi hiyo tunazuia private sector kukopa, hiyo private sector inaposhindwa kukopa italipaje kodi kwa Serikali, ili tupate mapato ya shilingi trilioni 17.1? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini biashara zinafungwa, makampuni yanondoka kwenye biashara tunakuja kuambiana hapa kwamba, kuna makampuni 200,000 yameongezwa katika kujiandikisha kwenye biashara. Sasa najiuliza swali…

TAARIFA ....

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kwa mujibu wa Kanuni, Serikali ndio ilitakiwa ithibitishe kwamba ninayosema siyo ukweli, lakini naomba twende kwenye ukurasa wa 41 mpaka 42. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ulinde muda wangu, Mheshimiwa Waziri anasema; Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2017/2018 Serikali itaendelea kupanua soko la fedha na mambo mengine, lakini 42 anasema; katika jitihada za Serikali kutaka kuimarisha ushirikiano kati yake na washirika wa maendeleo na kuhakikisha fedha zinazoahidiwa zinatolewa kwa wakati, Serikali na washirika wa maendeleo walitafuta washauri elekezi huru, timu hiyo iliongozwa na Dkt. Donald P. Kebaruka aliyekuwa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika. Washauri Elekezi walipewa kazi ya kutathmini na kutoa mapendekezo ya kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na washirika wa maendeleo na muundo wa utoaji fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikasema kwa namna ya lugha yoyote itakayofaa kutumika, kama ni kuimarisha, what so ever mimi sina ubishani katika hilo, hoja yangu ni kwa nini sasa nchi ambayo tumekuwa na uhusiano na hawa washirika siku zote mpaka madeni yakafutwa na Paris Club wakati wa Mheshimiwa Mkapa, mpaka tukawa na mahusiano makubwa ya kusifika wakati wa Serikali ya Awamu ya Nne, kumeingia kitu gani Serikali ya Awamu ya Tano? Ndiyo hoja yangu ya msingi ninayotaka kuuliza? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hiyo hoja ina ukakasi, Serikali itabidi mniwie radhi, lakini ndicho kilichoandikwa hapa ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nataka tu kujua kama yanaimarishwa, yanaimarishwa kwa sababu gani? Nilichokuwa najaribu kusema ni kwamba hata bajeti yenyewe kama nilivyosema sio ya uhalisia kwa sababu hiyo ya kwanza niliyosema kwamba, haiwezekani Serikali mkope kwenye benki za ndani, halafu wafanyabiashara watakopa wapi? Mnajua kabisa kwamba Serikali ina uhakika wa security zake kukopeshwa kuliko wafanyabiashara, private sector. Kwa misingi hiyo kusinyaa kwa private sector haionekani kodi mtapatia wapi ya shilingi trilioni 17. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia biashara nyingi kama nilivyosema zimefungwa, lakini hata matumizi yenyewe ya mashine za EFD bado kabisa hatujaweza kuhamasisha kwa kiasi cha kutosha katika mikoa yote katika nchi hii. Inaonekana hizi mashine za EFD zinakuwa so selective kwa sababu ukienda Kilimanjaro hizi mashine zinatumika mno kuliko kawaida. Kiduka cha shilingi milioni 14 lazima kiwe na mashine ya EFD, lakini njoo katika maeneo mengine ya nchi hii, hazitumiki! Tena hao ndio wanalalamika sana kwamba, hawana maendeleo, lakini hawataki kutumia mashine za EFD. Kwa hiyo, ni lazima haya mambo yafanyiwe kazi kama tunataka kuhakikisha kwamba tunapata hiyo shilingi trilioni
17. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hata wigo wa walipa kodi (tax base), Mheshimiwa Waziri hajaonesha hata kwamba, labda kwenye taarifa atuambie ni walipa kodi wangapi wa makampuni? Walipa kodi wangapi binafsi? Na walipa kodi wangapi ambao ni wa kawaida ili tufahamu kwamba hivi tunatengeneza tax base yetu kupitia wapi, ili tujue uwe…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)