Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. KHATIB SAID HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi nichangie katika hoja iliyoko mbele yetu inayohusu Muungano na mazingira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote napenda nami kwanza kumwomba Mwenyezi Mungu atujaalie Wabunge na Viongozi wetu afya njema na wale ambao afya zao zimetetereka miongoni mwao hata mimi, tujiombee Mungu atupe uzima ili tuweze kulijenga Taifa hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti namwombea kwa dhati tu Mheshimiwa Magufuli kama anavyopenda kusema tumwombee na mimi namwombea. Pia, namwombea kipenzi cha Wazanzibari, Mheshimiwa Seif Sharrif Hamad
MHE. KHATIB SAID HAJI: Mungu ampe afya njema na nawaombea hao wengine walioko huko pia Mungu awajaalie afya njema ili tutakapochukua madaraka halali Zanzibar waone namna tunavyoendesha nchi Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kwenye maombi yangu niweke upande wa pili. Pamoja na kwamba tumejiombea dua tupate uzima, lakini ikiwa Mwenyezi Mungu mwenyewe aliowajaalia maradhi ni kwa ajili ya dua zetu tulizoomba wale tuliodhulumiwa, Mwenyezi Mungu awaongezee maradufu maradhi hayo, ili wajue kama Mwenyezi Mungu yuko na Mwenyezi Mungu ndiye mwenye uwezo wa kutenda kila jambo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nianze kuchangia kwa kushukuru kuniweka mtu wa tatu na kulishukuru Bunge lako leo kutupanga wa upande huu tuwe wa mwanzo kuchangia, hii ina maana kubwa, hata Rais anapolihutubia Bunge hupewa yeye nafasi kwanza halafu sisi tukaja mwisho kuchangia. Kwa hivyo, leo wale mliowaweka badala yangu wote, najua hawana la kusema watalisema baada ya nitakayoyasema mimi, kaeni wanafunzi mjifunze. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kusema juzi Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakati anatoa mchango wake hapa alijinasibu sana na akasema mengi sana kuhusu uhalali wa kilichofanyika 20/3/2016 Zanzibar. Wanasema wajuzi wa mambo uongo unapoendelea kusemwa na usipokanushwa unaonekana ukweli. Bahati mbaya sana hayupo nilitaka niyaseme haya akiwepo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar, Kifungu cha 71 na Kifungu cha 72 ambacho kwa kuokoa muda nitasoma Kifungu cha 72. Kinasema hivi: “Mahakama Kuu ya Zanzibar ndiyo pekee yenye mamlaka na uwezo wa kusikiliza na kuamua mashauri yote yanayohusiana na uchaguzi wa Zanzibar.” Hicho ni kifungu.
MHE. KHATIB SAID HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiona wanawashwa ujue sindano inawapata.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wanaosema hata sisi hatukwenda Mahakamani, lakini Tume ya Uchaguzi ilitakiwa izingatie Kifungu hiki. Kwa hivyo, tunachosema hapa ni kwamba, uchaguzi wa Zanzibar uliofanyika mara ya pili ulikuwa ni uchaguzi wa haramu na umewapa madaraka ambao haukustahiki kuwepo, maana yetu ni Katiba hii. Sasa kama Katiba hii hamuikubali na Katiba hii ndiyo alioapia Rais wa Zanzibar na ndiye muapaji wa kwanza kushika Katiba hii, maana yake ni kwamba Katiba hii ni haramu hata kuishika. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, yamesemwa na tutaendelea kusema kwamba mnadhani limekwisha lakini ninalowaambia halijakwisha, la Zanzibar halijapita! Lipo na litaendelea kuwepo. Mambo ya Zanzibar ni wale wanaosema ni sawa na mchuzi wa mbwa, ukiukosa kuunywa wa moto ukipoa haunyweki tena! Utakuwa ni uvundo na subirini soon uvundo wa mambo ya Zanzibar mtaanza kuuona. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru katika Mkutano wa 15, Bunge la mwaka 2010, Bunge lililopita, nilinyanyuka hapa nikasema kwamba hakuna haja kusheherekea na kutumia mabilioni ya Tanzania kwa ajili ya sherehe za Muungano, nilisema hapa ndani, mwenye kukariri Hansard iko aende akatafute najua nilisema mimi. Nilisema tunapoteza pesa nyingi kusheherekea kitu kisicho na maana yoyote. Muungano wa Tanganyika na Zanzibar Mheshimiwa Waziri uliouremba na kuupaka kila aina ya poda, lipstick, manukato au udi, hakuna kitu!
Muungano wa Zanzibar na Tanganyika tuliungana kwa madhumuni makubwa ya kusaidiana kiuchumi, kudumisha amani na kuleta maendeleo ya nchi zetu hizi. Leo kama nchi hizi zimekuwa ni katika mstari wa mwisho kwa umaskini duniani mnajivunia nini na Muungano huu? Kipi cha kujivunia? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naona aibu sana kwamba Muungano huu umekuwa ni silaha tu ya kukidhi matakwa ya watawala kuendelea kuitawala Zanzibar kimabavu, hili ndilo lililoko! Nataka nikuhakikishie, Wazanzibari wamefikia mahali pamoja na unyonge wao, lakini siku ya hukumu tunaiandaa kwa ajili ya wote wanaodhulumu haki za Wazanzibari. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania ilikuwa ni nchi ya mstari wa mbele katika ukombozi wa nchi za Kusini mwa Afrika, lakini Tanzania hiyo leo imekuwa ni nchi ya mwanzo inayokandamiza washirika wa Muungano wa Zanzibar na watu wake. Hili halikubaliki, lakini tunakokwenda siyo kuzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo mnajifariji hapa kwa kuona kwamba sisi hatuna uwezo wa silaha lakini tuna silaha kubwa kuliko zenu ninyi na silaha yetu ni umoja wetu na Wanzazibari kwa umoja wetu tumekubali kufanya mabadiliko ili kuviondoa visiwa hivi pale vilipo viende mbele pamoja na wale wasakatonge wenu mliowaweka Zanzibar ambao wanakuja hapa wakitetea matumbo yao na siyo kutetea maslahi ya Wazanzibari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo ni aibu gani wakati Marekani wanafikiria kuondoa gereza la Guantanamo bay kule Cuba, leo Watanganyika mmeligeuza gereza la Seregea kuwa Guantanamo bay ya Wazanzibari. Mmewachukua Masheikh wa Zanzibar ndani ya miaka mitatu wako hapa kesi zao hata ushahidi tembe moja hamjapeleka wa kuthibitisha ugaidi wao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Brussels pametokea ugaidi juzi, wamekufa watu within one week, yule mwanamme mmoja ameachiwa huru kwa kusema hakuna ushahidi unaoonesha alihusika vipi na ugaidi wa pale. Leo ninyi hata aibu wala haya hamna, wanazuoni wa Zanzibar three years mnawanyima kukaa na watoto wao na wake zao, mmewaweka wake wajane ilhali waume zao wako, mmewaweka watoto mayatima ilhali baba zao wako. Haki gani, Muungano gani? Alaysa-Allah biahkami lhakimina hakika Mwenyezi Mungu atalipa juu ya udhalimu wote mnaowafanyia watu wa Zanzibar. Hatuna nguvu za vifaru, lakini nguvu zetu ni umoja wetu na iko siku Mwenyezi Mungu atatusikia kilio chetu cha kuona haki iko wapi mtaifuata mtake msitake! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda niseme wazi msimamo wetu wa kutoitambua Serikali ya Zanzibar. Wako wengine wanasema hapa kwamba, kama hamuitambui Zanzibar mbona mmekuja hapa? Katika busara ya kawaida unapokwenda porini ukakutana mbwa mwitu utafanya vyovyote ujinasue na mbwa mwitu, lakini ukitembea mtaani ukakutana na mbwa anakubwekea na mwenye mbwa unamuona yaani mfugaji wake, huna haja ya kuparuana naye, mtafute mwenye mbwa u-deal naye.
MHE. KHATIB SAID HAJI: Utaweza kumwambia mwenye mbwa, kwa hivyo tunajua kwamba Zanzibar mpiga filimbi wake yuko hapa na tunajitahidi kusema….
MWENYEKITI: Muda wako kwanza umekwisha;