Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Emmanuel Papian John

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. EMMANUEL P. JOHN: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwanza nimpongeze Rais kwa maamuzi mazuri anayofanya kwa ajili ya nchi yetu.

Jambo la kwanza ninaloshukuru, nashukuru kwamba wale wenzetu wataalam Wakurugenzi wa Acacia wamekuja kuona ni jinsi gani wanaweza ku-negotiate na Serikali kulipa deni lao. Naomba niseme jambo, wakati mnakwenda kwenye negotiation hiyo, naomba wale mabwana walipe kwanza trilioni 35 mezani ili muweze kuanza mazungumzo. (Makofi)

Mhesimiwa Mwenyekiti, kabla ya mazungumzo yoyote yale walipe trilioni 35 kwanza zikae mezani halafu muanze kuchakata maneno, mengine mtazungumza na mtaendelea mbele kujua ni namna gani wanatakiwa kulipa lakini heshima ya nchi yetu kwanza, bajeti yetu ya Tanzania kwa mwaka mzima wailipe mezani down payment kuonyesha kwamba ni commitment fee kwa ajili ya kuilipa nchi yetu gharama zao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, niombe wale wataalam wetu waweze kwenda Ghana wajifunze ni namna gani wao kwenye madini walifanikiwa. Watengeneze ile ripoti waangalie ni namna gani wao wamefanikiwa vipi halafu sasa watakapokaa na hao wenzetu wajue ni techniques zipi za kuwatega na kutengeneza hili jambo likae vizuri ili siku nyingine lisijitokeze na nchi yetu iache kupoteza kwenye suala la madini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Rais kwa kuonyesha jinsi gani ameji-commit katika hili, Rais kutoka nje kwenda Ulaya kila wakati sio zuri, hawa weupe na wao waje hapa wainame pale Ikulu wa-bend kwa Rais wetu, ametujengea heshima. Hiyo ndiyo njia pekee ya kuhakikisha kwamba hawa watu na wao tunaweza kuwamudu, hawa watu kila siku ukienda kuwainamia wanafikiri sisi ni wajinga kwa sababu weusi. Sasa safari hii Rais ametujenga heshima, Bunge hili tumuunge mkono na tuhakikishe kwamba anatutetea kwa jinsi ilivyo, wawe wanakuja wanainama Ikulu, wana-bend wakimaliza wanapanda ndege zao wanaondoka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Rais ameshamaliza kazi, sasa Bunge hili pekee ndiyo chombo pekee kinachoweza kumaliza migogoro iliyobaki. Tukubali tuungane tuwe wamoja tujenge nchi tukiwa serious, nje tucheke lakini ndani we need to be serious ili Tanzania ifike mahali inapotakiwa kwenda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna malipo yanayotakiwa kupatikana kwenye zile Halmashauri ambapo ile mikodi imekuwepo, wamechimba wananchi wetu wameendelea kuteseka, levy hawapati wanadai wenzao wanatimua vumbi. Kabla ya wataalam wetu kukaa kujadiliana na hawa watu wawe wameshalipa zile service levy kule kwenye yale maeneo, wakimaliza ndiyo warudi mezani ili waweze kuanza sasa mazungumzo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukurasa wa 93 wa kitabu hiki kuna Ranchi za Taifa. Ranchi hizi za Taifa zimekuwa zinasakamwa sana lakini naomba niseme National Ranching Company ni eneo pekee ambalo leo watafiti wetu wa Ph.D Program kwenye agriculture na mifugo wanafanyia hapo, moja. Mbili, vijana wetu wa field diploma na certificates wanafanyia field hapo ndiyo jicho pekee unaloweza kutafiti na kuona ukaandikia mwanafunzi alama za field aliyoifanya kwenye maeneo yake vyuoni. Sasa tunaomba NARCO iongezewe fedha kutoka shilingi milioni 126 kwenda shilingi milioni 250 ili iweze kufanya mambo yafuatayo:-

(i) Kuhakikisha kwamba wana-develop production ya mifugo mitamba kwa ajili ya maziwa hapa nchi.

(ii) Kukarabati maeneo ya majengo yao kwa sababu mengi yamechakaa kwenye ranchi zetu zote, ukiangalie zile headquarters, ukiangalia maeneo ya malisho, ukiangalia zile paddocks, kote kumechakaa. Tunaomba Serikali ilione hili lakini itambue haya maeneo kwa beacons kupunguza invasion ya vijiji na watu wanao-cross kutoka maeneo mablimbali ili haya maeneo yawe earmarked yalindwe kwa sababu ya training institutions kwa ajili ya nchi yetu. (Makofi)

(iii) Kuna kiwanda kile cha Ruvu, tunazungumza habari ya mifugo kuwa mingi, tunazungumza habari ya kuvuna mifugo, lakini hakuna meat industry ambayo inaweza kupeleka wale watu wakauza mifugo yao pale. Tunaomba hicho kiwanda kijengwe haraka ili hiyo mifugo ipate mahali pa kuweza kuvunwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la hii barabara yetu ya kutoka Handeni – Kibirashi – Kibaya – Singida; hii ni barabara ambayo inafungua fursa za kiuchumi kwenye ripoti ya kitabu chako hiki. Niombe barabara ya Iringa – Dodoma iko kwenye final touches mnamalizia, barabara ya Dodoma – Babati mko kwenye final touches mnamalizia, tunaomba priority iwe barabara hii kwa sababu zifuatazo:-

(i) Tunakwenda kujenga bomba la mafuta tumefanikiwa jitihada zimefanyika za Serikali, along hiyo barabara tunaomba basi hii barabara wakati bomba linajengwa sambamba na hii barabara ijengwe kiwango cha lami ili kuruhusu mizigo kuweza kupitika kwa urahisi lakini hizo fursa tuzifungue. (Makofi)

(ii) Hiyo barabara peke yake inafungua ile Bandari ya Tanga kuweza kupitisha mizigo inayokwenda Rwanda, Burudi na Kongo. Ile barabara itapunguza msongamano wa Bandari ya Dar es Salaam ili Bandari ya Da es Salaam ipunguze congestion magari yatembee kupita kule ili yaweze kutoka na kwa haraka zaidi na kupunguza mizigo na nchi yetu ipate mapato kwa sababu ya kupunguza msongamano. (Makofi)

(iii) Ikitokea tukawa na production ya kutosha njia pekee inayoweza kupeleka mazao nje kwa maana ya Kenya wakiwa na demand ni njia ya Mombasa, lakini kwa sababu area ya production ni Singida, Dodoma, Manyara na Tanga, njia pekee ni hiyo ambayo itapitisha yale mazao. Tunaomba hii barabara ifunguke kwa lami ili njia hizo ziweze kupitisha mazao magari yaende Mombasa kwa haraka na kuhakikisha kwamba hiyo barabara na gharama za nafuu kwa mkulima na mazao yetu wakulima wetu wakapate faida kutokea Mombasa, nchi jirani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna benki zetu za biashara. Mheshimiwa Waziri tunaomba ufumbe macho hizi benki kuna mahali zilikosea mmeziadhibu vya kutosha, tunaomba ufumbe macho uwasamehe; Benki za CRDB ziko zina shake, NMB ziko zina shake na hizi benki nyingine za biashara, tunaomba tunazidi kusisitiza wafungulieni nafasi wafanye kazi watu wetu waweze kukopa wafanye kazi, ili watu wetu waweze kulipa kodi na sisi tupate mapato kwa maana ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo muhimu la zaidi ninachoomba, Benki ya Kilimo hii ndio njia pekee tunayoweza ku-access wakulima 85% ya Watanzania, wakulima na wafugaji wanaofanya kazi, njia pekee ya kuwafikia ni njia ya Benki hii ya Kilimo, hii benki tunaomba ipewe mtaji. Hawa jamaa katika hizo shilingi trilioni 35 nilizozungumza atakazoweka down payment mezani trilioni tano peleka Benki ya Kilimo, ikae huko ndio wakulima wetu wakafutie jasho kwa kukopa hizo pesa wakafanye kazi za uzalishaji wakaweze kuinua kipato chao cha maisha kwa maana ya benki hii, kupitia hii benki. Hii benki ndio itakuwa njia pekee na mkobozi kwa ajili ya watu wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, tuko kwenye kanda kame, Mkoa wa Dodoma, Mkoa wa Manyara, Mkoa wa Shinyanga na Mkoa wa Simiyu, haya ni maeneo kame sana kwa nchi yetu. Priority iwe ni kuangalia ni namna gani ya kuhakikisha kwamba haya maeneo uanapata maji. Nikuombe Mheshimiwa Waziri, issue kubwa ya maeneo haya ni uwezo wa kupatikana mabwawa makubwa mapana yenye uwezo wa ku-support watu na mifugo yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuombe tunalo Bwawa kubwa la Dongwa ambalo limeingizwa kweye programu ya mwaka 2017/2018, niombe hili bwawa litakapochimbwa lina worth ya shilingi bilioni 24; tunaomba mtusaidie hili bwawa lichimbwe kwa sababu hili bwawa linapeleka maji Wilaya ya Gairo, hili bwawa linapeleka maji Kongwa kwa maana ya Mkoa wa Dodoma, hili bwawa linapeleka maji Kiteto kwa maana ya Mkoa wa Manyara. Kwa sababu hili bwawa litakuwa kubwa sana mkilichimba mtakuwa mmeokoa wilaya tatu kwa wakati mmoja, lakini watu wengi wataweza kuondoka kwenye hiyo shida kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho nikuombe. Nasisitiza nakuomba ile milioni 50 ya kila kijiji, niombe utume wataalam wako wawili/watatu waje pale Kiteto waone tulivyo- strategize namna gani ya kuweza kutumia pesa kwenye VICOBA. Ile timu yako itakapoona inaweza kujua ni wapi pa kuingilia na zile pesa zikaweza kufanya kazi vizuri.

Sisi tunaamini na ninakuahidi na mimi ndio nitakuwa msimamizi na mimi ndio nitakuwa mdaiwa wa kwanza na ninaomba nisaini nikishindwa kurejesha hizo pesa nisigombee Ubunge mwakani na kadi yangu ya chama nirejeshe kwa ajili ya wale wananchi wangu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri nimeji- commit kwamba hizo pesa nitazirejesha kwa sababu nina uhakika kwa nature ya mazingira tuliyotengeneza ya VICOBA pesa ya Serikali haitapotea, wananchi kiuchumi watanyanyuka na sisi tuna uhakika wa kufanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Ahsante sana.