Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nichukue fursa hii kuipongeza Serikali, kumpongeza Rais wetu, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri sana anayoifanya pamoja na Serikali yake yote. Nimpongeze Waziri wa Fedha na Mipango pamoja na timu yake nzima kwa kazi nzuri wanayofanya, tunaendelea kukuombea na tunasema endelea na mfumo huo huo ili tuweze kusonga mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ningeomba kushauri; pamoja na kuwa kazi inayofanyika ni kubwa na nzuri lakini bado kuna nafasi kubwa ya kuboresha na hayo ambayo tutayasema ili mjitahidi kuboresha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, ninaomba lile suala la Serikali kurudisha madaraka ya Waziri wa Fedha na Mipango ya kusamehe kodi, tulifuta huko nyuma kwa ajili ya matumizi mabaya ya msamaha huo. Mimi naomba haya madaraka yarudi ili miradi mingi ambayo tunapata msaada katika Serikali Kuu, Halmashauri zetu na taasisi mbalimbali iweze kuisaidia Serikali. Leo hii inashindwa kupata msamaha wa kodi na miradi mingi inakwama kutokana na suala hilo.

Kwa hiyo, mimi naamini kwenye hii Serikali ya Awamu ya Tano hakuna atakayethubutu kutumia hayo madaraka vibaya. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri naomba mje na mpango huo tuirudishe ili miradi ambayo inakwama kutokana na suala la kusamehewa kodi, basi na yenyewe tuweze kufaidi misaada hiyo ambayo tunapata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, ninapenda nikupongeze kwa kuondoa kodi ya Motor Vehicle Licence, Sheria ya Traffic Act. Hapa tunajichanganya, zile ni sheria mbili tofauti, Traffic Act umeondoa kwa kulipa kila mwaka, haijaondolewa kwa ujumla, umeondoa utalipa mara moja tu kwa gari inaposajiliwa. Hii nyingine ni excise duty ilikuwepo, shilingi 400 umeongeza hii shilingi 40, hongera sana kwa sababu fedha hizo hizo ndizo zitakazoboresha barabara na huduma nyingine ambazo hawa ambao tunalalamika kwamba mafuta ya taa na nini, kwamba wanafanyaje, kwa sababu hiyo barabara ambayo inaenda huko kijijini ndiyo inalipiwa na fedha hiyo. Mimi nasema ungeongeza zaidi ili huduma hizi nyingine zote ziendelee kuboreshwa huko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba katika ule wigo ulipotaja vile viwanda ambavyo vitapata msamaha umetaja sekta kama nne; ya mafuta, ya ngozi, lakini ninaomba mtanue wigo zaidi ili sekta nyingine pia kama za kilimo, mifugo, uvuvi pia viwanda vidogo vidogo. Hao wakubwa watakuja watapitia TIC watapata huo msamaha, lakini hivi viwanda vidogo vidogo vya Watanzania wenye mtaji mdogo pia na wenyewe mngewapatia huo msamaha kwenye capital goods na wakati wanataka kuanzisha. Hiyo kodi ikiondoka nina uhakika kwamba huko tunakotaka kuelekea kwenye uchumi wa viwanda tutaweza kufika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine, tutakapoelekea kwenye Finance Bill nitaomba maeneo mengi yale niliwapongeza kwamba mmeondoa kodi nyingi kwenye sekta ya kilimo; lakini kwenye sekta ya mbegu bado kuna kodi nyingi ambazo zimeachwa, lakini pia tuangalie mfumo mzima kwamba tunafanyaje. Tumesamehe, kwa mfano kwenye mbolea inayotoka nje ya nchi, pongezi kubwa kwa hilo, lakini je, kiwanda cha ndani, huyu wa nje kama amesamehewa yote na wa ndani anaendelea kulipa je, si kwamba tunaendelea na mfumo ule ule kwamba tutaua viwanda vya ndani kwa kuruhusu vitu kutoka nje kuingia bila kodi? Kwa sababu huyu wa ndani hawezi kutoza VAT, inputs zake hawezi kudai, kwa hiyo bado utaendelea kuumiza viwanda vya ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado mimi naona kwenye sera yetu panatakiwa kufanyika mabadiliko makubwa na wigo wa kukusanya kodi bado ni mdogo. Nikupongeze kwamba mmesema kila Mtanzania ambaye anafanya biashara hata kidogo aendelee kulipa kodi, elimu kubwa iendelee kutolewa ili kila Mtanzania aweze kulipa kodi. Muhimu ni kwamba sekta isiyokuwa rasmi bado ni kubwa na inaendelea kukua; mimi ninaomba, sijaona kabisa kwenye bajeti nzima sehemu ambapo mtaweza kufanya sekta isiyokuwa rasmi ihamie kuwa rasmi kwa sababu ile sera haijakaa vizuri na incentives zile hazipo, na muhimu kwenye uwekezaji wa aina yoyote ni zile incentives.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia ningependa kuona kwamba vyanzo vingine vyote vipya tuendelee kuviangalia na tuweze kupata kodi ambapo badala ya kutegemea hao wenzetu ambao wanatupa misaada kwa sababu ile pia ni kodi ambayo wamelipa kule kwao. Tanzania kwa rasilimali tuliyonayo tunaweza kujitegemea na inawezekana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, mimi naunga mkono hoja na ningeendelea…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)