Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi nami nichukue dakika tano kuchangia bajeti. Nilimsikiliza sana Waziri wakati akiwasilisha bajeti ile, suala la kufuta motor vehicle na kurudisha shilingi 40 kwenye mafuta ni kama umeiba kutoka mkono huu na kupeleka mkono wa kushoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni nani asiyefahamu kwamba ukigusa mafuta umegusa kila mahali. Ni nani asiyefahamu umuhimu wa mafuta kwa nchi hii mnatuambia tunakwenda kwenye nchi ya viwanda. Hiyo motor vehicle ambayo imefutwa sijui Waziri alifanya research kiasi gani nakuona kwamba labda iwe compansated na shilingi 40 na ni kwa nini 40 tunataka kufahamu, kwa nini isiwe shilingi 10 au tano?.

Mheshimiwa Mwenyekiti kuna mambo ya msingi ambayo lazima niyaangalie. Ukizungumza habari ya mafuta unazungumza maisha ya watu. Hatuwezi kwenda kwenye viwanda kama mafuta bado yako juu. Huwezi kugusa uzalisaji wa namna yoyote kama mafuta bado yako juu. Kwa hiyo, ni lazima Waziri aangalie upya suala hili la kuongeza shilingi 40 kwenye mafuta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeangalia pia katika kitabu cha bajeti ya Waziri. Anazungumzia kwamba kufutwa kwa hizi road licence pengine zitasaidia na hakutakuwa na shida na itawezesha watu wengi wenye magari waweze kuendelea kufanya kazi zao vizuri. Lakini ninachotaka kukuambia analysis ambazo tumezifanya shilingi 40 kwa mtu mwenye scania au basi anatoka Dar es Salaam anakwenda Mbeya anatumia may be lita 600, go and return lita 600 ukizidisha mara arobani tunazungumzia shilingi 24,000 kwa siku. Kwa mwezi tunazungumzia shilingi 720,000, kwa mwaka nzima tunazungumzia shilingi 8,640,000 wakati hiyo motor vehicle ilikuwa haizidi shilingi 500,000. Kwa hiyo, tunachoona ni kwamba watakaokwenda kuumia ni Watanzania, kwa sababu kila mtu lazima atumie usafiri kwa vyovyote vile iwe kusafirisha mazao, kwenda kokote anakoweza lakini tutakwenda kuwaumiza Watanzania, kwa hivyo naona hii shilingi 40 haina tija. Otherwise angetuambia ni kwa nini shilingi 40 na isiwe shilingi tano au isiwe shilingi moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeangalia kwenye bajeti ya Waziri kila mwaka sigara, pombe zinapanda. Siku Watanzania watalala waamke, wamwelewe vizuri Naibu Waziri Kigwangalla na Waziri wa Afya, Mheshimiwa Ummy Mwalimu kuhusu suala la no smoking hatutakuwa na bajeti. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunasema sigara hizi ndiyo zinaleta madhara, ndiyo zinazotuletea kansa, kifua kikuu, tunakiwa na maadhimisho ya siku kifua kikuu. Fedha hizi hizi zinazosema tunazosema tuna-save huku tunakwenda kutibia watu wetu ambao wanaugua magonjwa yanayotokana na sigara na pombe. Kwa hiyo, ifike mahali tutatafute sources nyingine ambazo zinaweza zikasaidia Watanzania na siyo kucheza na afya za Watanzania, kuendelea kupandisha kila wakati haizuii mtu kutumia sigara. Lakini tungetafuta vyanzo mbadala ambavyo ni reliable vitakavyosaidia Taifa hili kupata mapato halali bila kuwa na athari kwa wananchi wanaotumia vitu hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala lingine la bandari, ni aibu. Hotuba ya Kambi ya Upinzani imesema kwamba lazima kuwe na vyanzo vingine ambavyo vitalisaidia Taifa hili. Tukiangalia nchi zingine zinafanya vizuri, angalieni Bandari ya Beira, angalieni Mombasa wanavyofanya vizuri na World Bank wamewahi kusema endapo tutatumia vizuri bandari, zaidi ya asilimia 30 tunaweza tuka-save kwenye bajeti yetu. Sasa hivi bandari imegeuka siasa. Viongozi wa Serikali wanaamka asubuhi na vyombo vya habari wanakwenda bandarini kutumbua watu.

Mheshimiwa Waziri kwa nini tusikubali kwamba tunahitaji watu professional watusaidie tufanye nini ili bandari zifanye kazi vizuri. Tuna Bandari ya Dar es Salaam, Tanga na Mtwara yenye kina kirefu lakini bado hazisaidii mchango kwenye hii bajeti yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima tuangalie haya mambo...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru lakini siungi mkono hoja.