Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Ester Michael Mmasi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. ESTER M. MMASI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru kwa kunipa nafasi hii ili niweze kufidia muda wangu ambao nilipoteza kwa siku ya Ijumaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda leo niongee na wanawake wenzangu wa Bunge lako. Sisi Wabunge bila kujali itikadi zetu za vyama tunakutana kwenye jukwaa moja la Kibunge la Wanawake. Jukwaa hili linaitwa TWPG yaani Tanzania Women Parliamentary Group. Pia katika jukwaa hili tunakutana kwenye agenda moja kwa kawaida katika kila mwaka tunakuwa na ajenda kama wanawake. Nitawakumbusha wanawake wenzangu ambao mmefika hapa pengine naona wengi wetu sasa tunakata network, tumejitoa kwenye agenda hatujui hata tunachokifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2015 tulikuwa na ajenda kama wanawake wa Tanzania iliyokuwa inasema Orange the World nadhani Mheshimiwa Susan unasikiliza. Siyo hivyo tu, tukasema kwamba agenda hii haijagusa a real context ya Tanzania, tukasema kwamba tubadilishe ajenda. This year ninapoongea kwamba mwaka huu unaoishia tarehe 30 Juni, sisi kama wanawake tumebeba ajenda moja inayosema rudisha rasilimali ya mwananchi kwa wananchi. Uhuru wa uchumi uwasaidie wanawake na wanaume walioko pembezoni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, anachokifanya leo Mheshimiwa Rais ninajiuliza ni nani aliyetutoa kwenye ajenda ya kurudisha rasilimali ya nchi hii kwa wananchi kama siyo sisi wenyewe tumefika mahali hatujielewi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wamekuja hapa ndugu zangu, wameshindwa kukaa na kuangalia, katika nchi ya Tanzania tunazo changamoto nyingi, lakini leo tunakuja hapa tunatoa mustakabali mzima, tunachangia hotuba yetu hii ya Wizara ya Fedha, wenzetu hawa wanakuja na ngonjera mia, 1000 ambazo zinatutoa kwenye ulingo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ngoja niwaambie hawa ndugu zangu, hivi mnatambua kwamba, mpaka Machi 2017 tuna changamoto kubwa ya bajeti ndogo ya Fungu la Maendeleo kwenye Wizara ya Maji? Mnafahamu tuna asilimia
19.8 tu zilizokwenda? Mnafika hapa mnakuja kutuambia Mheshimiwa Rais ameita wezi Ikulu! Ngoja niwaulize ninyi wanawake, hivi najiuliza na mimi ndio na mimi nipo, najiuliza na mimi ni mwanamke ndio, kwa sababu wamesimama hapa watu wanakuja kusema kwamba Mheshimiwa Rais ameita wezi Ikulu! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi Canadian Embassy kama Mheshimiwa Rais ataanza kualika watu Ikulu, Canadian Embassy watafanya kazi gani? Basi tufute hii Embassy ya Canada tuifute, lakini sio hivyo tu, ninaongea na sisi wanawake na mimi nipo katika hilo ninaloliongelea hapa, lakini kama sio hivyo mkaja mkatuambia kwamba tukaombe msamaha! Jamani ngoja niwaambieni, msamaha wa kweli ni msamaha ambao utaambatana na vitendo katika kupeleka tumaini la kweli kwa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Rais anachokifanya ni kupeleka tumaini la kweli kwa wananchi na kama msamaha ungekuwa ni jibu, leo mimi ninakaa pale Dar es Salaam niko Tegeta, ninatarajia ningemuona Mheshimiwa Halima yuko wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, alikuja hapa akatoa kauli nisameheeni, baada ya kuambiwa mpaka na maaskofu, kuambiwa na mapadri kaombe msamaha, akaja akaomba msamaha. Yuko wapi kama kauli ya msamaha ndio jibu? Sio jibu, ni dhamira ya dhati katika kupeleka tumaini la kweli kwa wananchi. Mheshimiwa Rais ana dhamira ya dhati katika kupeleka tumaini la kweli kwa wananchi. Tumpe nafasi, hii nafasi ni ya Chama cha Mapinduzi, hii Serikali ni Serikali ya Chama cha Mapinduzi, tunaongozwa na manifesto, tupeni nafasi tufanye kazi katika nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na haya ninayoyaongea ninapenda tu niwaambie wanawake wenzangu, hebu tusimame katika nafasi zetu. Hebu tuache ngonjera nyingi humu ndani, hazina mantiki, hazitusaidii, tuna mengi. Ukienda kule Jimboni ukamwambie mwanamke nilienda kutafuta gold ni nani aliipiga au nilienda kutafuta, nilienda nikatetea ajenda hii ilikuwa ya UKAWA au ajenda hii ilikuwa ya CCM! Hivi kwa nini tuna haja gani sisi kutoka kwenye ajenda yetu kama wanawake? Tuna kauli moja tu, rudisha uchumi wa Tanzania ukamsaidie mwanamke aliyeko pembezoni, hii ndio ajenda yetu, hiki ndicho tulichotumwa tuje kufanya katika Bunge lako hili Tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa kuchangia hotuba hii ya Mheshimiwa Mpango. Naomba niguse suala la kilimo. Ni kweli ninapenda sana niipongeze sana Wizara yako, Mheshimiwa Waziri kwamba kwa mara ya kwanza Serikali hii imejitahidi katika kumtua mkulima mizigo mizito aliyonayo. Nimeona kwamba kuna produce cess ambazo mmetoa VAT kwenye masuala ya kilimo cha biashara, lakini pia kilimo cha chakula. Sio hivyo tu, nimeona mmetoa msamaha wa kodi hata kwenye capital goods ili kuweza kuhamasisha na kuboresha viwanda vyetu nchini vinavyozalisha ngozi, mafuta na dawa za binadamu, hii ni hatua nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sio hivyo tu, mlitoa kodi 108 katika Bunge hili, kodi 108 kwa mwaka mmoja. Lakini sio kodi 108 za mazao, pia mliweza kutoa kodi kwenye tani moja ya vyakula zinazotozwa na Halmashauri za Wilaya. Siyo hivyo tu mmeleta bulk procurement system katika kupeleka pembejeo kwa wakulima wetu, hizi ni hatua nzuri sana. Lakini Mheshimiwa Waziri bado tuna changamoto kubwa, nimetafuta sana miundombinu ya maji ya umwagiliaji mmeiweka wapi? Nimeenda kwenye Wizara ya Maji sikuona, nimeenda kwenye Wizara ya Kilimo sikuona, fungu hili liko wapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri tunayo changamoto wewe ni shahidi, kwenye hali ya uchumi wa Tanzania mwaka 2015/2016 umeandika wewe mwenyewe kwa maandishi kwamba, bajeti ya Kilimo, Fungu la Maendeleo Vote 43 ilienda asilimia tatu tu, hii ni changamoto kwetu. Mheshimiwa Waziri siyo hivyo tu, kilimo kimechangia asilimia moja kwenye Pato la Taifa, hii ni changamoto ambayo hatuna majibu. Mheshimiwa Waziri ni lazima tuweze kufahamu ili tuweze kupata malighafi za kulisha viwanda vyetu ni lazima Tume ya Mipango ya Taifa isimame katika nafasi yake na iweze kutoa ushauri maridhawa katika kuongoza Taifa lako hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na masuala ya kilimo mimi ninafikiri nasi wanawake wenzetu tufahamu kwamba, ipo haja ya kusemea kwa sababu, mwanamke wa Taifa hili anazalisha kiwango cha …

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)