Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia afya njema siku hii ya leo na kutoa mchango wangu kuhusu bajeti ya mwaka 2017/2018. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kabisa kwa moyo mkuu na akili zangu zote kuunga mkono maoni yaliyotolea na Msemaji Mkuu wa Kambi ya Rasmi ya Upinzani Bungeni katika Wizara ya Fedha na Mipango ya Mheshimiwa Halima James Mdee, Mbunge ambayo imewasilishwa Bungeni kama maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na Mheshimiwa Silinde. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, maneno yote yaliyozungumzwa humu yana mantiki na miaka yote bahati nzuri tangu niingie Bungeni hii ni awamu yangu ya pili kuna mambo ambayo tuliyazungumza kama Kambi na nimeona kwamba Chama cha Mapinduzi ndio kinatembea humo humo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwahiyo, pamoja na kwamba yakiletwa yanabezwa lakini utakuta labda wanajifungia chumbani na kuyachukua kuona kweli haya ndiyo maoni ya wananchi. Kwahiyo, ni muhimu sana Waziri mwenye dhamana akachukua, akatendea kazi na Rais wa Nchi, akachukua akayafanyia kazi kama anavyofanya sasa, kwa hiyo, ni muhimu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ingekuwa ni uungwana wa hali ya juu kama Chama Tawala kingekiri na Wabunge wenzetu wa Chama Tawala kingekiri walitukosea, walituzarau, walitubeza, lakini ndio ukweli wenyewe, sasa hivi Awamu ya Tano ndio wanachukua na kuyafanyia kazi. Lakini sisi tunatimiza wajibu wetu kama Kambi tunawapa maoni, pale mnapoyatekeleza tunaona wananchi wetu ndio wanapata nafuu. Kwa hiyo, tutakwenda tu mpaka Watanzania wapate uelewa kwamba watuingize madarakani ili tuyatekeleze yale tunayowashauri. Kwa sababu mtu ukimshauri anaweza akayatekeleza, lakini wazo kwa sababu sio lake, hawezi akalitekeleza sawa sawa kwa mfano kama elimu bure, sisi tungeingia madarakani tungeifanya sawa sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na mambo hayo, nimeona kwenye kitabu hiki cha Waziri nataka niseme kwamba katika ukurasa 85 amezungumzia kuhusu TAZARA na nilivyokuwa naangalia nilizani anazungumzia reli ya TAZARA, lakini kibaya zaidi amezungumzia TAZARA flyover pale Dar es Salaam. Nataka nipate majibu ya Serikali ni namna gani sasa watumishi wa TAZARA walioenea katika Mikoa ya Morogoro mpaka Mbeya ni namna gani hatima yao kwa sababu hali ni tete wengine wamestaafishwa, hawajapewa mafao yao, Serikali imekaa kimya, TAZARA yenyewe ina kizungumkuti, haijulikani namna gani. Jamani hii hali inatisha watu wanateseka wameshindwa kusomesha watoto, wengine wamekufa, hawajui hatma yao, naomba nipate majibu ya Serikali, nini hatma ya TAZARA na wastaafu wa TAZARA na uboreshaji wa reli ya TAZARA. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naenda kwenye barabara, kwenye kipindi cha miezi miwili iyopita hakuna mama aliyetoka Mlimba kwenda kwenye Hospitali ya Wilaya ya Rufaa Ifakara, barabara haipitiki, barabara zimekatika, barabara kilometa 230 Waziri asikie, nasimama hapa kila siku kilio ni barabara, wanaoteseka ni akina mama, watoto, wazee, hivi hata nikisoma hii bajeti inazungumzia flyover, ndege na mambo mengine treni. Mimi wananchi wa Mlimba wanaionaje hiyo bajeti, wanaona kama sio yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeomba sasa watuhakikishie wananchi wa Mlimba Waziri wa barabara amefika kule lakini hali ni tete, na Meneja wa TANROADS nimeongea naye anasema wakati Serikali inajipanga kujenga barabara ya lami, basi tupate hela za kutosha za kujenga angalau kilometa 50 ambazo tunyanyue tuta ili ile barabara ipitike mwaka mzima, lakini hela wanazopangiwa hazitoshi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeomba hebu muwahurumie wananchi wakule na wale tuwe tumepata uhuru pamoja mwaka 1961, lakini mpaka leo wale watu kama hawajapata uhuru. Lakini eneo lile ndio linalotoka mazao ya kilimo, Kilombero Planting Limited iko pale Mngeta lakini hamna barabara. TAZARA haiboreshwi, barabara hakuna, hivi mnataka yale mazao watu wabebe kichwani na kule kuna kilimo kikubwa?(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kuhusu maji, Waziri amesema atakwenda lakini maji Jimbo la Mlimba ni mtihani, hivi mji mzima mdogo wa Mlimba hivi mtu anapata maji kwa siku saba mara moja, hivi kinamama kuna Mawaziri hapa akina mama, hivi mama anaweza akakaa akapata maji siku saba mara moja,huyu mama, msichana anaishi vipi katika mazingira gani. Anaenda kujifungua inakuwaje, kwa hiyo, shughuli za maendeleo kule tunalima, shughuli za maendeleo zinarudi nyuma kwa sababu tumekosa maji. Naomba haya maendeleo twende kwa pamoja, sio wengine wanasonga mbele, wengine tunarudi nyuma, haiwezekani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mahakama, swali linakuja lakini kule hakuna mahakama, kilometa 230 mtu anatoka anakwenda kufuata mahakama ya Wilaya Ifakara, barabara hazipitiki kwahiyo kule haki hakuna. Yaani kule kama dunia ndio imeumbwa leo, yaani ni hatari, sasa vilio vyote ninavyosema ni vya uhakika. Vilevile kuhusu vituo vya polisi Mheshimwia Mwigulu ameenda kule amejionea mwenyewe, hakuna vituo vya polisi kule, hali ni mbaya sasa watu wanakosa mahakama, wanakosa vituo vya polisi, wamekosa barabara, wamekosa maji, hawa watu hebu muwafikirie, hivi wanaishi ishi vipi wale watu kule! Kwa hiyo hivyo ni vilio. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo cha umwagiliaji kule ni ndogo kuna mradi mmoja tu wa Njagi mito mikubwa inapita lakini hakuna umwagiliaji na kule Njagi wanamwagilia wakati wa mvua, wakati wa kiangazi hola, hicho ndio kinaitwa kilio cha umwagiliaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu naenda kwenye makinikia, kwenye hii bajeti inazungumzia flyover, lakini wamegundua wanavyosema kwamba kuna makinikia yana grams chungu mzima za dhahabu na tutapata karibuni trilioni mia moja sijui na ngapi, sasa naomba hebu geuzeni tusubiri hizi za makinikia ambazo tunaenda kuzipata, zije zijenge reli hizo hela ambazo zipo sasa hivi kwenye bajeti hii tukaimarishe miundombinu vijijini kwa wanakijiji huko, ili hizo zinazokuja za makinikia tuweke sasa hiyo miundombinu tununue ndege nini, nini au vipi! Si hela zipo zinakuja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mikataba na sheria, iletwe Bungeni lakini tulipiga kelele nyuma hamna kitu. Kule Mahenge, Ulanga kuna mgodi mkubwa madini ya graphite, madini ya hali ya juu duniani, lakini mpaka leo wananchi wa kule hawajui hatma yao, mikataba yenyewe ndio hivyo imefungwa fungwa, mtuletee hiyo mikataba na sheria hapa Bungeni tuone tunaendaje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, gesi na mafuta, yamegundulika Wilaya ya Malinyi kule Morogoro, Kijiji cha Ipela Asilia, lakini mikataba hata wananchi wa kule hawajui itawafaidisha vipi, kwahiyo ndio haya haya tunayoyasema sasa baadaye ndio mnasema sasa tumeibiwa tumeibiwa sasa si muanze sasa? Kwa nini mnangoja mpaka tuibiwe? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba haya mambo twende kwa pamoja wote ni watanzania tunahitaji maendeleo, hatuhitaji matatizo kama hivi vyanzo vya Halmashauri wameshavipora huko juu, lakini kuna hiyo hoja kwamba ikifika mwaka 2025 Halmashauri zote ziwe zimejitegemea kwa 25% ile hoja mmeifuta au bado ipo? Zisije Halmashauri zikapata hoja za mkaguzi wakati zimenyang’anywa mapato zitashindwa kufikia malengo.
(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika sera vijiji lazima vifanye uchanguzi, nasema hivi Mrimba mpaka leo kuna vijiji vitatu havijafanya uchaguzi tangu mwaka ule wa uchaguzi wanasema kuna mwekezaji, sasa kwenye uwekezaji hakuna uchaguzi. Sasa ninachokiomba ile kesi iliyoko mahakamani.