Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Ahmed Ally Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Solwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. AHMED A. SALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi, kwanza kabisa naunga hoja bajeti hii kwa asilimia 100. Katika hoja ya mpango aliyoleta Mheshimiwa Waziri wa Fedha, tulimshauri mambo mengi, tulimshauri suala zima la bandari kachukua, kaweka mezani kafanyia kazi, tukamshauri masuala haya ya leseni za magari, kachukua, kaweka mezani na kafanyia kazi, tumemshauri mambo mengi sana kwa wakati ule na tuliongea kwa hisia na ndio maana nasema leo Mheshimiwa Waziri wa Fedha naomba nikupongeze sana umekuwa msikivu, umesikiliza ushauri wa Bunge na umelinyia kazi kwa maslahi mapana ya Taifa letu. Hongera sana nakuunga mkono kwa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuna mawili machache madogo sana naomba nikudokeze, kuna wenzetu hawa wa bodaboda ambapo SUMATRA wamewaambia mpaka tarehe 30 wasipolipa 22,000 kutakuwa na operation moja kali sana na vijana hawa ndio wanaanza maisha katika Taifa letu hili, hebu lione hili katika kufata kodi hii, ili vijana hawa wa bodaboda waweze kufanya kazi kwa raha zao zote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile sekta utalii, nilikuwa na rafiki yangu mmoja yuko Ulaya pale London na Marekani wakasema inakuwaje watalii wengi wanakwenda Kenya, tatizo ni nini, ukitazama kwenye records za watu wanaosafiri kutoka nchi za Ulaya ni asilimia kubwa sana wanaokwenda Kenya, zaidi ya kuja kwetu Tanzania. Kwa research ndogo tuliyofanya inaonekana, bado tatizo la VAT on tourism sector linaathiri mapato makubwa. Kwa hiyo Mheshimiwa Waziri wa Fedha litizame hili, lichukue nina imani kabisa kwa hekima zako unaweza ukalifanyia kazi, ama kama sio mwaka huu, kwa mwaka wa fedha ujao, lichukue ondoa kabisa wenzetu wa Kenya wanatuingiza mkenge kila mwaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala hili tulikaa pamoja na Kenya, Wakenya wakaondoa wakasema sisi hatukujipanga, matokeo yake ni kwamba wametuacha sisi tumeweka VAT wao wameondoa VAT wameongeza watalii wengi sana katika nchi yao ya Kenya. Na hii Mheshimiwa Thailand inachukua asilimia 30 ya mapato yao katika utalii, naomba sana suala hili ni kubwa mno katika kuingizia mapato ya nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru sana Mheshimiwa Rais, huwezi kuongea bajeti hii kama huongei suala zima la makinikia. Makinikia ndiyo fedha na tunatarajia sana baada ya negotiation hii kwenye bajeti ya 2018/2019 tutakuwa na fedha nyingi sana itaweza kutekeleza mradi wa reli bila mkopo, anaweza akaongeza ndege, tunaweza tukaongeza miundombinu mikubwa ya nchi yetu tukaweza kufanana na nchi zote katika nchi za Afrika zilizopiga maendeleo. Kwa hiyo, nampongeza sana Mheshimiwa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru tena kwa mara nyingine Mheshimiwa Rais katika Kijiji cha Nyaligongo, Kata ya Mwakitolyo aliweza kufuta leseni ya mwekezaji na kusema kwamba wachimbaji wadogo wa Kata ya Mwakitolyo wasiondolewe, wachimbe, wanufaike na raslimali zao, kwa bahati mbaya sana mwekezaji aliyefutiwa leseni yake akafutwa akabakizwa mmoja mwekezaji Mchina, Mchina huyu amepewa leseni zaidi ya miaka nane, hakuna alichokifanya, ni utapeli, anachukua leseni anakwenda nchi za nje anapata pesa, anachukua mkopo na kuuza hisa katika mabenki ya nje. Tarehe 08 mwezi uliopita, Ofisi ya Mkoa kwa bahati mbaya sana ni masikitiko makubwa sana, imekwenda Mwakitolyo kwenye Kitongoji cha Mahiga wamewafukuza wachimbaji wadogo wadogo kwa mtutu, kwa polisi kwa kuwatisha na risasi zililia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wamekimbia, wachimbaji wadogo wadogo wamekimbia, watoto watano wamepotea mpaka leo baada ya siku tatu, tathimini inafanywa kwa mtutu. Polisi anakwenda kwa familia anamuambia wewe kama haukubali hii, shauri yako itakula kwako, kwa mtu ambaye hajaja hajakuwepo ananyang’anywa hiyo haki.

Kwanza kabisa nimuombe Waziri wa Mambo ya Ndani kwa hekima na busara zote, polisi siwalaumu kwa sababu wale wanaamuliwa tu, siwalaumu sana Jeshi la Polisi ila namuomba Mheshimiwa Waziri aondoe Jeshi la Polisi kule kwa hekima zote, wananchi hawana raha Kata ya Mwakitolyo, wanakaa kama wakimbizi na nimuombe Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, kama alivyowasaidia wanyonge hawa katika Kijiji cha Nyaligongo aendelee kuwasaidia kwenye Kitongoji cha Mahiga, ninaomba sana Mheshimiwa Rais afanye hivyo, namuomba sana Mheshimiwa Waziri Mkuu, namuomba sana Mheshimiwa Makamu wa Rais na wote wenye maamuzi ya maeneo haya wawasaidie wachimbaji wadogo wadogo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la njaa linapotokea katika nchi hii au upungufu wa chakula Mkoa unaoathirika ni Mkoa wa Shinyanga, namba moja, kwa hiyo kwa bajeti ijayo ninaomba sana, Mheshimiwa Waziri wa Fedha kwa sababu wewe ni Waziri wa Fedha na vilevile una mpango wa nchi nzima, suala zima la kukabiliana na tatizo la upungufu wa njaa ni kwenye irrigation scheme (kilimo cha umwagiliaji). Kwa mfano mimi nina kilimo cha umwagiliaji pale Nyida, nina kilimo cha umwagiliaji katika Kata ya Bukande ni kubwa zinaweza zikalisha Mkoa wa Shinyanga na mikoa mingine mitatu/minne mitano, kwahiyo ninaomba sana fedha ziweze kutengwa ili kukabiliana na hali ya njaa hii kwa miaka ijayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanda, Mheshimiwa Magufuli anataka aitoe nchi hii yaani ingewezekana katika miaka mitano hii, tungeweza kufika mbali sana, lakini kwa bahati mbaya sana yako maeneo ni vikwazo katika speed ya Magufuli, Mheshimiwa Rais ana speed, kuna maeneo yanazuia. Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara, chukua report ya REPOA, chukua report ya CTI wanafanya kazi nzuri, kutaneni na wawekezaji ili mpate matatizo yanayofanya uwekezaji katika suala zima la viwanda kwenda kwa mtindo wa kinyonga. Ukipata hii Mheshimiwa Waziri wa Fedha, utakuja na bajeti ijayo ambayo utaisaidia na tutarekebisha sheria, ili speed ya Magufuli kwenye suala zima la Tanzania viwanda iende vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tazama mfano wa Ghana, Ghana leo wame demolish VAT on everything on the industry on the manufacture industry wamefuta kila kitu, ukitizama hapa hapa juzi tu Rwanda hawa, wanasajiri kampuni leo masaa manne on line, masaa manne wanasajiri kampuni hawataki kukuona wanakujibu wanakupa registration card wanakupa TIN number, wanakupa VAT, wanakupa kila kitu kwa masaa manne, juzi tu hawa, leo wanatushinda kwa namna gani. Ndiyo maana nasema tufanye research, tupate ukweli mzima kabisa wa namna gani kuweze kwenda speed ya Magufuli kwenye suala zima la viwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, TIB tuwaongezee fedha benki hii ili iendelee kutoa mikopo na mnaweza mkawa specifically kabisa Mheshimiwa Waziri wa Fedha unajua ukawa specifically kabisa kwamba tunatoa fedha hizi ziende kusaidia mikopo ya viwanda na utoa riba kutoka asilimia 18 mpaka asilimia nane kama mlivyofanya kwenye kilimo, tunakwenda, tunatoka tu. Kwa hiyo, ni suala la ku-negotiate ni suala la kubadilisha sheria na kuiweka vizuri ili watanzania waweze kunufaika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, majengo, katika Jimbo la Solwa nina majengo mengi sana, mimi na wananchi tumejenga na tumefikisha kwenye usawa wa renta, na suala hili nazani ni la Taifa, la nchi nzima, hakuna Mbunge anaweza akasimama hapa akasema mimi nimekamilisha majengo kwa asilimia 100 hayupo. Mimi nina zahanati zilizofika renta 45, nina Hospitali ya Wilaya moja ambayo imefika renta, nina maeneo mengi ambayo ninahitaji msaada wa Serikali Kuu, sasa kwenye bajeti ijayo, najua bajeti hii itakuwa ni ngumu lakini weka tu kwamba kuwepo na mwongozo kwa majengo yote yaliyo tayari kwenye majengo yote yaliyofika renta vyumba vya madarasa, nyumba za walimu, hospitali za wilaya, vituo vya afya vyote viwe observed kwenye bajeti ya mwaka ni ili tuweze kumaliza tatizo kwa sababu hayo ndiyo maendeleo ya wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukijenga vyumba vya madarasa, tukajenga nyumba za walimu zilizokuwa zimefika renta, tutakamilisha angalau kupunguza kwa asilimia 50 tutakuwa tumefika.