Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nina wasiwasi na taarifa yake kama ni sahihi kwa sababu mimi nimefanya kazi na Mheshimiwa Lowassa kwa karibu sana yeye labda hamjui. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naendelea, kutoka Pangale hadi Matagata kuna kilometa 416 sawasawa na kutoka Dodoma hadi Chalinze hivi ni Wilaya gani katika nchi hii unaipata ya namna hiyo, Wilaya gani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaye Mkuu wa Wilaya mchapa kazi, tuna Mkurugenzi mchapa kazi safi kabisa, lakini kuna maeneo tangu waje hawajawahi kufika na huwezi kuwalaumu kwa sababu kwenda kama Matagata lazima ajaze full tank gari na bado kuna mafuta mengine yanatakiwa yawe kwenye dumu. Sasa gharama za uendeshaji wa namna hiyo nani ataziweza. Tumekubaliana kwamba tuanzishe ajenda ya kisheria iende kama sheria inavyotaka, kwamba tupitishe kwenye Kamati za Vijiji, kwenye Kata, iende Wilaya, iende Mkoani halafu ije kwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais alipokuwa Nzega alisema kwamba yeye hatarajii kuanzisha Wilaya mpya wala Mkoa mpya, kwa hiyo, hapo viongozi wanakuwa na kigugumizi kidogo namna ya kutekeleza hii.

Naomba kwa makusudi kabisa namuomba Mheshimiwa Rais huko aliko kwa makusudi kabisa, Sikonge tupate Wilaya mpya na ninajua hili Mkuu wangu wa Wilaya na Mkuu wangu wa Mkoa wananisikia hapa na nimeishazungumza na Mheshimiwa Waziri Mkuu suala hili ni muhimu sana, kama mwananchi wa Matagata anahitaji kumuona Mkuu wa Wilaya anatakiwa atumie siku tano, siku tatu za kusafiri, siku tatu za kurudi nyumbani, siku sita, kwa uchache kabisa siku nne, sasa kwa nini wananchi katika nchi hii moja wawe wanapata adhabu na wananchi wengine hawapata adhabu kama hizo. Kwa hiyo, tunaomba sisi Sikonge tupate Wilaya mpya, Mheshimiwa Rais akubali tupate Wilaya mpya. (Makofi)

La mwisho tuna sababu nyingi lakini sababu kubwa...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.