Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuchangia kwa niaba ya Wananchi wangu wa Jimbo la Rufiji basi naomba nitoe mchangi wangu kuhusiana na bajeti hii iliyowasilishwa mbele ya Bunge lako hili tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti hii nimpongeze sana Wazari wa Fedha, Mheshimiwa Dkt. Mpango kwa kuja na bajeti nzuri ambayo imezingatia maoni ya wananchi, maoni ya Wabunge na maoni ya wadau mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hivi kwasababu ukiiangalia bajeti hii na ukipitia takwimu zilizowahi kutolewa na Central Intelligence Agency (CIA) katika dondoo zao za World Fact Book ambazo waliwahi kuzitoa ambazo zimeelezea mipango mbalimbali ya bajeti ambazo zinatolewa na ambazo
zinatolewa na CIA katika takwimu zao zinazotolewa mara kwa mara ambazo zinachunguza nchi mablimbali zaidi ya
267. Katika takwimu zilizotolewa na World Fact Book zinaifanya bajeti yetu ya Tanzania kuwa ni miongoni mwa bajeti bora kabisa hapa Afrika na dunia na ukiangalia takwimu hizi zimegawanya bajeti katika maeneo matatu; yaani nchi zinazojitegemea, nchi tegemezi na nchi zingine zikijumuisha nchi za Ulaya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwahiyo, bajeti yetu ni dhahiri kabisa ni stimula to economic sector na imedhamiria ku- alleviate poverty katika nchi yetu hii ya Tanzania. Niipongeze Serikali sana kwa namna ya kipekee kabisa ambavyo imedhamiria sasa kutukwamua Wananchi wa Jimbo la Rufiji. Tukiangalia miradi mbalimbali ya Benki ya Dunia imefika Rufiji leo hii kutokana na maombi ya Mbunge wa Jimbo la Rufiji na tumeweza kupata miradi kadhaa ya kutoka Benki ya Dunia ambapo sasa wananachi wangu wa Kata ya Mbwala wataweza kupata maji ya kutosha katika maeneo ya Nambunju, Tawi, Kikobo lakini pia katika maeneo mbalimbali maeneo ya Miangalaya, Namakono, Tawi, Siasa kule Utete na pia Serikali imedhamiria kuchimba visima viwili katika Kata ya Chumbi na haya yote yalikuwa ni maoni yangu na maombi yangu kwa Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Serikali imekubali kutuchimbia kisima katika shule ya sekondari ya Mkongo pamoja na kusambaza mabomba katika kata hii ya Mkongo lakini pia katika kata ya Ngarambe, Njawanje, Kingulwe na Namakono, Kipugila pamoja na maeneo ya Nyaminywili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilisema niipongeze Serikali kwasababu maeneo yetu mengi wakati Serikali inafikiria kumkwamua Mwanamke au Mwanamama kumtua ndoo kichwani sisi kule wananchi tulidhamiria kuondoa vipara kichwani kwa akina mama kwa sababu wananchi wetu wamekuwa wakibeba maji katika umbali mrefu zaidi ya kilometa saba na yako maeneo na baadhi ya vijiji ambavyo wananchi wamediriki kuhama vijiji vyao kwasbabu tu ya kutokupatikana kwa maji. Kwa hiyo, kwa namna ya kipekee kabisa naipongeza sana Serikali kwa kudhamiria sasa kutatua kero ya maji kwa wananchi wangu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija upande wa pili kuhusiana na suala zima la kilimo kama ambavyo Mwalimu Nyerere aliwahi kusisitiza katika kitabu chake cha Ujamaa kwamba “The hidden story of the sociallist village” kilichowahi kutolewa mwaka 2008 na kikarekebishwa tena mwaka 2014 na Bwana Ibott aliwahi kusisitiza kuhusiana na vijiji vya ujamaa katika kuboresha na kuhakikisha kwamba tunakuwa na uchumi wa kujitegemea sisi wenyewe Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na sisi Wananchi wa Jimbo la Rufiji tunayo ardhi iliyo nzuri yenye rutuba na tunaamini kabisa ardhi ya Rufiji inaweza kulisha Nchi yetu hii ya Tanzania lakini pia inaweza kulisha mpaka Afrika Mashariki, lakini tatizo kubwa tulilonalo ni watu wachache ambao wamejimilikisha ardhi yetu ya Rufiji na imesababisha kwamba wawekezaji wengi wanakosa ardhi wanapokwenda TIC kuomba kufanya uwekezaji katika maeneo yetu ya Rufiji, tunaonekana Rufiji hatuna ardhi kwa sababu tu kuna watu wachache ambao wamejimilikisha ardhi, ardhi ambayo hawaitumii kwa ajili ya kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwahiyo kwa kupitia Sheria ya ardhi sura ya 113 na Sheria ya ardhi sura ya 144, nimuombe Mheshimiwa Waziri wa Ardhi lakini pia Mheshimiwa Rais kunyang’anya Wawekezaj wote Matapeli walioingia Rufiji ambao wamejimilikisha ardhi na hawaitumii ardhi kwa ajili ya kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti iliyopita Waziri wa Kilimo alisimama katika Bunge hili na kuwaambia Warufiji kwamba watapata Kiwanda cha Sukari. Leo hii wananchi wa Rufiji wananihoji, wanauliza hiki kiwanda kimekwenda wapi? Lakini tunajua kwamba yupo Muwekezaji aliyechukua ardhi katika Kata ya Chumbi, Muhoro na maeneo mengine ya Tawi katika Kata yetu ya Mbwala akidhamiria kujenga Kiwanda cha Sukari lakini sisi tunajua kwamba mwekezaji huyu ni tapeli na hana uwezo wa kujenga kiwanda hiki na tunaiomba Serikali kupitia Waziri wetu wa Kilimo, Waziri wetu wa Viwanda asimame hapa atuambie na tunamuomba Mheshimiwa Rais afute hati hizi zote na ikiwezekana hati hizi wakabidhiwe mashirika ya umma kwa mfano PSPF pamoja na Mashirika mengine NSSF na LAPF ili waje Rufiji kutujengea cha sukari. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ardhi ya Rufiji ni ardhi yenye rutuba sana, tunaamini tukipata Kiwanda cha Sukari wananchi wangu wataweza kulima miwa. Nikuombe Waziri wa Kilimo au Waziri wa Viwanda au Mheshimiwa Waziri wa Fedha usimame hapa utuambie. Lakini pia Waziri wa Ardhi usimame utuambie wale wawekezaji matapeli waliokuja Rufiji na kuchukua ardhi ni lini watanyang’anywa ardhi hiyo na ardhi hiyo irejeshwe Serikalini ili sasa wawekezaji wanapokwenda TIC waweze kupata ardhi ya kuja kuwekeza katika maeneo yetu ya Rufiji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunayasema haya kwa sababu wananchi wengi wa Rufiji hawana shughuli za kufanya yaani economic activity kwa wananchi wa Rufiji ni ndogo sana. Na ndio maana leo hii baadhi ya wananchi wanajiingiza kaitka mambo yasiyofaa. Kwa hiyo, ili kulikwamua tatizo hili niombe Serikali sasa kuhakikisha kwamba inawasaidia Warufiji ili sasa wananchi wangu waweze kupata shughuli mbalimbali za kufanya katika uwekezaji ambao utafanywa na wawekezaji watakaoletwa na Serikali kupitia TIC pamoja na Wizara nyingine mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niliona niseme hili kwa sababu ninaamini kabisa kilimo ndio kitaweza kumkomboa Mtanzania na kama tunavyofahamu kwamba asilimia 70 ya Watanzania ni wakulima, tunaiomba Serikali kuwa serious kabisa kwenye jambo hili la kilimo. Ninaamini kabisa kwamba iwapo tunahitaji kujitegemea ni lazima tuzingatie Kilimo hiki ambacho nimekizungumzia hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo lingine tulilonalo kwa wananchi wa Rufiji ambao ninaomba niishauri Serikali kama ambavyo imezungumzwa katika ukurasa wa tisa wa hotuba ya Mheshimiwa Waziri ni tatizo la barabara. Tuna kila sababu ya Rufiji kuomba Serikali sasa itujengee barabara ambazo zitasaidia kuongeza shughuli za uchumi, na barabara hizi ambazo nazizungumzia hapa zimezungumzwa katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ukisoma ukurasa wa 46 wa Ilani yetu ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ambayo inazungumzia uboreshaji wa Miundombinu. Niombe Serikali sasa, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Rais kwa kukubali kutujengea barabara yetu ya Nyamwage kwenda Utete, niiombe Serikali sasa ujenzi wa barabara hii uharakishwe na uanze sasa. Kwani wananchi wana kiu kubwa ya kusubiri ujenzi wa barabara hii yenye kilometa 33.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia barabara ningine ya kutoka Ikwiriri kwenda Mwaseni kule Mloka, itasaidia kufungua shughuli za uchumi. Na ninaamini kabisa wa Rufiji watashiriki kwa hali na mali katika kushiriki katika shughuli za uchumi. Na barabara nyingine ni yakutoka Kibiti kuelekea Mkongo, barabara hii pia ni muhimu sana kwa shughuli za uchumi wa Rufiji. Na barabara ya kutoka Bungu kuelekea Nyamisati ni barabara muhimu sana iwapo barabara hii itajengwa itaweza kuwakomboa Warufiji na Warufiji wengi watashiriki katika shughuli za uchumi na itawaondoa katika fikira za kushiriki katika mambo yasiyofaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitumie dakika mbili tatu kushauri katika suala zima la madini. Nchi yetu imefika hapa kwa sababu ya kuwepo kwa mikataba mibovu kama ambavyo Wabunge wengi wamelizungumza jambo hili. Na mimi nimpongeze sana Mheshimiwa Rais kwa kupambana na ukoloni mamboleo, mimi nauita ukoloni mamboleo kwa sababu hili limezungumzwa na watu wengi Duniani akiwepo Profesa Lumumba. Pia tumeona mfano wa yeye aliyofanya Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli, wameanza kuiga Marais wengi na viongozi wengi wa Dunia wameanza kuiga. Kwa mfano Rais wa Latin America hivi juzi amezuia kilo 1300 ya dhahabu, ni kwa sababu tu mikataba mingi ya dhahabu, mikataba mingi ya madini imekuwa ni mikataba mibovu ambayo inawakandamiza wananchi ambao wanamiliki madini yale. Na tunasema mikataba hii ni detrimental to public interest, mikataba hii ni mibovu na mikataba ambayo haifai. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwanza naomba niishauri sana Serikali yangu, kabla hatujafikia hatua ya kurekebisha mikataba hii, basi tuanze kwa kurekebisha Sera ya Madini, sera hii ya mwaka 1997. Sera hii ya madini inayoiondoa Serikali katika umiliki wa madini yetu hapa nchini na kuyafanya madini kuwa chini ya wawekezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaunga mkono hoja, ahsante sana.