Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Itifaki ya Nagoya ya Kusimamia Upatikanaji na Mgawanyo Sahihi wa Faida zitokanazo na Matumizi ya Rasilimali za Kijenetiki.

Hon. Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Itifaki ya Nagoya ya Kusimamia Upatikanaji na Mgawanyo Sahihi wa Faida zitokanazo na Matumizi ya Rasilimali za Kijenetiki.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tunawashukuru sana Wabunge wote waliopata nafasi ya kuchangia ambao wamechangia vizuri sana kuhusu hoja hii na bahati nzuri wote Mkataba pamoja Itifaki zote mbili zimeungwa mkono na Bunge hili na kwamba hakuna upande wowote ambao umepinga, tunaahidi kwamba yale mapendekezo waliyoyatoa Waheshimiwa Wabunge tutayazingatia katika kuhakikisha kwamba tuna usimamizi bora wa mkataba pamoja na itifaki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme moja la nyongeza katika hayo kwamba Serikali hapa imelaumiwa katika kuleta nyaraka. Serikali inaonewa kwa vipi katika jambo hilo? Siyo kazi ya Serikali kugawa nyaraka Bungeni. Kazi ya Serikali tulipoingiza kazi za Serikali katika Mkutano huu wa Saba tuliainisha kazi zote na nyaraka zote tuliwasilisha.

Kwa hiyo, siyo kazi ya Serikali tena kulaumiwa kuhusu nyaraka na kwa Wabunge wanaojua kufuatilia nyaraka kama rafiki yangu hapa amekuwa akilalamika na ni mkongwe kabisa anajua, Serikali ikishaorodhesha kazi zake document zipo kwa Katibu wa Bunge. Hivyo, Serikali haihusiki tena katika hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapoleta mikataba hii na itifaki hizi, haimaanishi kwamba Serikali haijafanya lolote katika utekelezaji wa majukumu yake. Serikali tumefanya mambo mengi katika usimamizi wa Bahari Kuu pamoja na Ukanda wa Pwani, hilo lazima lifahamike. Sheria na kanuni nyingi zimetungwa na usimamizi wa usiku na mchana kuhakikisha kwamba Ukanda wa Pwani unalindwa katika uchafuzi, unalindwa katika uharibifu wa mazingira ambayo yanaweza yakafanyika Ukanda wa Pwani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ufupi pia iongelee kuhusu baadhi ya hoja ambazo zimetolewa na Waheshimiwa Wabunge. Tumeshauriwa kwamba mali zetu zimekuwa zikiibiwa kwa utaratibu huu, wizi wa rasilimali za kijenetiki kwa mfumo wa watu wanajifanya ni watafiti na wafanyabiashara na tukaombwa kwamba tuweke mwongozo mahsusi ambao utalinda rasilimali zetu zisiweze kuporwa tena.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuwaambia kwamba Kambi zote bahati nzuri imezungumzwa na Kamati yenyewe ya Viwanda, Biashara na Mazingira na imezungumzwa na Kambi ya Upinzani na Serikali haina tatizo katika hili. Tutaandaa mkakati mahsusi ambao unadhibiti wizi wa aina yoyote katika eneo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, maisha ya Pwani yamekuwa bora vipi toka mwaka tulivyoridhia. Amezungumza Makamu Mwenyekiti wangu enzi hizo wa Kamati ya Uchumi, Viwanda na Biashara kwamba wamenufaika vipi Pwani pamoja kuridhia mwaka 1996. Wamenufaika kwa mengi, moja ni kwamba miradi mingi sana inayojengwa sasa hivi tuna ujenzi wa kuta katika Pwani kwa maana ya Pangani, Rufiji, Zanzibar, Pemba na Kilimani zinajengwa. Tunapanda mikoko katika maeneo yaliyoharibiwa ya pwani, tunaanda mikoko Rufiji, Zanzibar na maeneo mengine ili kuhakikisha kwamba tunanusuru. Pia tunajenga mifereji maene ambayo yanaathiriwa na kuongezeka kwa kina cha bahari ili kuweza kuhimili pia maji ya mvua ambayo yanaleta mafuriko makubwa kwa wananchi, kama kwa rafiki yangu hapa Mheshimiwa Mtolea kule miradi mbalimbali inaendelea kujengwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia hatujakaa, tunacho chuo kikubwa sana ambacho wamekisifu sana Kamati hapa, hiki chuo chetu cha Taasisi ya Sayansi ya Bahari ambacho kinafanya kazi kubwa na kimejengwa Zanzibar kwa maana hiyo hiyo ya kuhakikisha kwamba ukanda wa pwani unalindwa kwa nguvu zote na tafiti zinapatikana kwa wakati na kutumika kwa wakati. Sio hivyo tu, tumeanzisha sheria mbalimbali nyingi za kulinda mazingira yetu katika ukanda wa bahari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, taasisi za tafiti zinafanya vizuri tu, COSTECH na IMS katika kuhakikisha kwamba Ukanda wa Pwani unanufaika hasa katika maeneo ya ufugaji wa samaki, mwani pamoja na mazao mengine ya bahari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchangiaji mmoja alisema kwamba Tanzania imegeuzwa kuwa dampo na sisi hatusimamii. Ni kweli tuna haja tu ya kuongeza usimamizi, lakini ni kweli kabisa mipaka yetu yote tunailinda, ndani ya eneo la bahari yetu tunalilinda kwa nguvu zote na taasisi za Serikali zipo kazini. NEMC, SUMATRA na TPA wapo kazini kuhakikisha kwamba kwa namna yoyote meli zinapongia ndani katika eneo letu hili udhibiti wa uchafuzi wa mazingira hauruhusiwi kwa aina yoyote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata upande wa kemikali tupo vizuri, sawa zinaweza zikatokea kesi mbalimbali ambazo zipo hapa nchini za umwagaji wa sumu katika bahari yetu na katika kingo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)