Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Itifaki ya Nagoya ya Kusimamia Upatikanaji na Mgawanyo Sahihi wa Faida zitokanazo na Matumizi ya Rasilimali za Kijenetiki.

Hon. Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Itifaki ya Nagoya ya Kusimamia Upatikanaji na Mgawanyo Sahihi wa Faida zitokanazo na Matumizi ya Rasilimali za Kijenetiki.

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi niweze kuchangia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme maneno machache sana kwa leo, hii safari tuliyonayo ya kuibadilisha Tanzania hawa wenzetu hawako na sisi. Kwa hiyo, ni kama tunampigia mbuzi gitaa. Hakuna mtu aliye tayari kusafiri na hii kasi tuliyonayo. (Makofi)


Mheshimiwa Mwenyekiti, amezungumza rafiki yangu hapa amechangia anasema tunaletewa Hati za Dharura, toka nimekuwa Bungeni taarifa zote za Kamati huwa tunapewa hapa, zinasomwa tunaanza kuchangia, sijaona jipya wakisoma taarifa tunagawiwa na sisi hapa tunasoma baadaye tunaanza kuchangia. Sasa kama ninavyowaona hawa, mtu mwenye akili hata kama ungepewa siku kumi huwezi kuelewa ambaye huna akili. Lakini mwenye akili haya masuala tumeshapewa leo na Kamati ya Uongozi imeshakaa imeshauriana sioni sababu ya kushindwa kuendelea na kujadili.

T A A R I F A . . . . .

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Watanzania wamemsikia Mheshimiwa anayejiita shemeji yangu kwa kusema nilisha-declare mimi sijasoma. Ni bora ukasema mimi ni darasa la saba kuliko kuwa na hivyo vyeti ulivyo navyo wakati akili huna. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuzungumza haya maneno yanayozunguzwa humu ndani, yote haya ni propaganda kinacholengwa humu ni makinikia. Hawa watu


wanachokitaka ni safari ya kurefusha mjadala kwamba tusijadili hizi sheria ili tukabanane na wazungu tulipwe pesa, lengo lao ni kurefusha masafara ili wakatafute cross-cross kule Morena walikokuwa wanakaa. Hatukubaliani nayo ngoma imeletwa tupige leo hii hii tumalize.

Nafahamu hawa wenzetu hawana uchungu na hii miswada mara nyingi hawana uchungu, sisi wenzenu tulioumia tunatamani hata ingepigwa siku moja hii sheria ambayo inataka kwenda kumbana mzungu atulipe pesa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri tuende na ile slogan ya juzi kwamba hela zikitoka hawa tusiwape, zije kwenye majimbo yetu sisi wenye shida. Haiwezekani mtu anasimama hapa anazungumza anasema Wabunge tumekaa miezi mitatu tumechoka kutafuta nini wakati tunalipwa pesa, tuongezwe hata wiki mbili. Watu wenyewe njaa humu zimetuua humu watu mkifukuzwa mnatoa macho, halafu unakuja kuanza kuzungumza vitu vya ajabu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nafikiria masuala haya yaende kama yalivyopangwa na hakuna mambo ya kutishana mambo ya Kibiti kuna nini. (Kicheko)

MWENYEKITI: Kuhusu Utaratibu.

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana, unajua Waheshimiwa Wabunge Spika anatuelekeza vizuri uwe na tabia ya kuwasiliza na wenzio huwa tunavumilia, wewe umesema hapa tumekuwa Bunge la vibogoyo, kutoa macho unaumia? Na kweli umeyatoa macho! Tunawaona hapa mkifukuzwa mnavyotoa macho kule mtaani. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo suala la kuzungumza kukodoa macho au watu wamehongwa ni maneno yako tu na vitendo vyako vinadhihirisha kwenye Umma. Hivi kweli unategemea hiyo Serikali ya kuitoa CCM ya ninyi mnaowatetea wezi kwa style hii! Serikali ya ninyi mnaokataa kujadili Miswada ya kwenda kudai pesa zetu. Mimi nilikuwa nashauri tu kwamba hawa wenzetu hawapo pamoja na sisi katika safari ya kuibadilisha Tanzania, hapo wamekaa tu kizungumkuti lakini muda wowote walikuwa wanaondoka nje.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)