Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Itifaki ya Nagoya ya Kusimamia Upatikanaji na Mgawanyo Sahihi wa Faida zitokanazo na Matumizi ya Rasilimali za Kijenetiki.

Hon. Salum Mwinyi Rehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Itifaki ya Nagoya ya Kusimamia Upatikanaji na Mgawanyo Sahihi wa Faida zitokanazo na Matumizi ya Rasilimali za Kijenetiki.

MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na mimi nashukuru kuweza kupata nafasi hii, ninakushukuru kwa kuweza kupewa haya makabrasha na maazimio haya yote matatu wakati mmoja kuweza kuyapitisha, tatizo moja tu lililokuwepo kwamba uelewa wa Wabunge wengi katika haya Maazimio ndiyo kitu kidogo kinachoonekana ni tatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina-declare interest kwamba nimefanya kazi kwenye Marine Conservation kwenye Mradi wa MACEP chini ya World Bank miaka mitatu, naelewa haya maazimio yaliyokuwa yamepita huku nyuma. Lakini nilitaka kutoa ushauri tu sijui kama muda utatosha katika hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja katika maazimio ambayo yalipendekezwa miaka mingi kwa nchi yetu hii imegeuka dampo la kutupwa takataka nyingi kutoka nchi za nje. Wenzetu Kenya waliridhia mapema, baadae baada ya kuridhia wakawa wanachukua bidhaa kutoka viwandani mwao, zile by products zilizomalizika wanakuja kutupa katika bahari yetu kwa sababu tumeshindwa kuridhia mkataba huu, kwa hiyo shamba hili limekuwa kila mmoja anaweza kutupa na kufanya anavyotaka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili katika bahari kuna mambo mengi, moja katika vitu vinavyokuwa disturbed ni bioanuai iliyopo katika bahari. Mazingira yetu ya bahari yanachafuliwa kwa vitu vingi, hali ya hewa inachangia, lakini mtiririsho wa bidhaa za kikemikali kutoka kwenye viwanda umekuwa ni mkubwa na hasa Watanzania wenyewe tunaufanya. (Makofi)

Mheshikiwa Mwenyekiti, tuna viwanda vingi katika belt hii ya bahari ambayo Wahindi na wengineo wanaomiliki viwanda vile wanatiririsha maji ambayo yana sumu na kemikali kutoka kwenye viwanda vyao, hawana mifumo ya kuhifadhi maji machafu na ya kemikali ambayo wanatengeneza bidhaa mbalimbali. Sasa sheria hii au Azimio hili liende likawabane hawa wote wenye viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajua wazi kwamba wengi wao wanawahonga wale watu wa mazingira wanaokwenda kufanya impact assessment katika maeneo yao na kusababisha uchafuzi wa mazingira uongezeke. Bahari yetu, beach zetu, kila siku, kila mwaka inaongezeka zaidi ya mita moja, bahari inalika kutokana na destruction ambazo zinafanyika za uchafuzi wa mazingira katika maeneo haya, ninaiomba Serikali hili tuweze kulisimamia. (Makofi)

Mheshikiwa Mwenyekiti, jingine ambalo linachangia, tumeweka uwekezaji wa mahoteli, tumezuwia wenye mahoteli kujenga ndani ya bahari, lakini yapo mahoteli wamejenga migahawa ndani ya bahari kitu ambacho vilevile kinachangia kuharibu fukwe na kuharibu ule uoto wa asili wa bahari uliokuwemo katika maeneo yale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi nyingi za nje zinatumia eneo lile la bahari kuu kupitisha na kumwaga bidhaa mbalimbali katika maeneo hayo. Mfano mdogo nilionao ni meli nyingi zilizokuwa zimezuiliwa kipindi kile na Al-Shabab zilikaa na bidhaa zile kwa muda mrefu zikiwa zimezuiliwa katika maeneo yao na bidhaa zile zilimwagwa katika ukanda huu wa bahari yetu sisi.

Kwa hiyo, athari iliyotokea samaki wengi waliokuweko katika maeneo yale waliathirika, lakini watu ambao walitumia wale samaki walipata matatizo ya ngozi na wengine walipata matatizo ya cancer. Haya matatizo imekuwa sasa kwetu bila kuridhia mikataba kama hii au maazimio kama haya hatutaweza kuweza kufanya usimamizi wa mazingira yetu. (Makofi)

Mheshikiwa Mwenyekiti, lingine lililokuweko katika nchi pamoja na rasilimali nyingi tulizokuwanazo katika eneo letu lakini hakuna doria ambazo zinakwenda kuangalia kitu gani kinafanyika katika ukanda wa bahari kuu, kitu ambacho kila mmoja ana uwezo wa kufanya anachokitaka, mpaka silaha mbalimbali…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)