Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipatia nafasi hii ya kuchangia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza natoa pongezi kwa Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri na Wafanyakazi wote wa Wizara hii. Pili, naomba kutoa pongezi kwa kazi wanayoifanya nzuri hasa Mkoa wa Morogoro kuhusu migogoro ya wakulima na wafugaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nyote mnafahamu kuwa Mkoa wa Morogoro ulikuwa na matatizo sana hasa kwa upande wa wakulima na wafugaji mpaka mapigano na mauaji yakatokea kwa upande wa watu na mifugo. Nashukuru Serikali kwa sababu Mawaziri walifika kwa kusaidiana na uongozi wa Mkoa pamoja na Wilaya waliweza kufanya kazi kadri walivyoweza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa sababu dawa muhimu ya kumaliza hii migogoro ni upimaji wa ardhi. Upimaji wa ardhi ambao sasa hivi umefanyika kwenye Wilaya ya Malinyi, Ulanga pamoja na Kilombero kwa baadhi, nashukuru kwa sababu wametoa hata hati miliki na hiyo ndiyo ingekuwa mkombozi. Tufahamu kuwa hawa wanaopewa hati miliki ni wachache, naomba kwa sababu tumepata ufadhili kutoka Serikali ya Uingereza pamoja na Sweden na Denmark kupitia kwenye mashirika yao ya maendeleo ya DANIDA, DFID pamoja na SIDA nashauri Wizara kama inawezekana waweze hata watu wengine kupimiwa kwa sababu hata registry ambayo ni masjala wameweza kujenga lakini watu wangeweza kumilikishwa wote ingekuwa vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Mkoa wa Morogoro ifahamike kuwa ni Wilaya zote zilikuwa na matatizo ya mifugo. Wilaya zote Mvomero nashukuru mmeweza kupima kiasi, Kilosa mmeweza kupima kiasi, lakini mfahamu kuwa watu walikufa Mabwerebwere, watu walipigwa na hasa wanawake ambao walikuwa wanalima mpunga wao, wengi walikimbizwa hawawezi kulima.

Naomba sana tena sana kwa kusaidiana jinsi mlivyoweza kupata ufadhili kutoka kwa mashirika hayo, Mheshimiwa Waziri una wataalam wazuri ambao wanaweza kuandika maandiko ya kuweza kuomba project pamoja na kusaidiana na Halmashauri zetu za Wilaya ya Gairo, Kilosa, Mvomero, Morogoro Vijijini hata Manispaa pamoja na kule ambako tayari mmeshaanza kupima tuweze kupata kupimiwa ardhi kwa sababu ni majaribio yaweze kuwa majaribio ya Mkoa mzima watu wote mlikuwa mnajua kuwa Mkoa wa Morogoro ndiyo umeweka historia kwenye migogoro ya wakulima na wafugaji, kuweza kupimiwa ardhi kusudi tupate hatimiliki watu waweze kumiliki pamoja na tuweke historia ya kumaliza migogoro ya wakulima na wafugaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nashauri kuwa kwa Wilaya zingine Mikoa yote ya Tanzania ambayo inajulikana kwa migogoro hii ya wakulima na wafugaji pamoja na migogoro ya ardhi, dawa ni kupima ardhi, kupata hati miliki, hati miliki ambayo inaweza kukusaidia hata kupata mikopo lakini kujua kuwa ni ardhi gani mifugo itaweza kuwa, ni ardhi gani wakulima wataweza kuwa na ni ardhi gani wafugaji wataweza kuwa na hii tutakuwa tumepanga mipango mizuri ya matumizi bora ya ardhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujua kuwa kwa sababu wataalam ni wachache na kuna vyuo, Chuo Kikuu cha Ardhi, Chuo cha Ardhi Morogoro pamoja na Chuo cha Ardhi Tabora, udahili uweze kuongezwa ili kusudi tuweze kupata watumishi wengi wataalam wa ardhi huko kwenye Halmashauri zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kabisa niongelea kuhusu mipango ya miji. Bila ya kupanga miji itakuwa kuna ujenzi holela kama tunaoushuhudia watu wanajenga mpaka milimani na ninyi Wizara mpo, naomba na hilo mliangalie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie kwa kushukuru sana nyumba za National Housing zimejengwa pamoja na nyumba za watumishi ardhi hata Mkoa wa Morogoro tumepata lakini tatizo kama wenzangu wanavyosema gharama bado ni kubwa. Naomba muiangalie hiyo gharama ili kusudi hata wale vijana wanaoanza kazi sasa hivi, waweze kupata nyumba zao wakalipia kidogo kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.